• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
Kinondoni Municipal Council
Kinondoni Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Kinondoni

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Maadili ya Msingi
    • Wasifu wa Halmashauri
  • Utawala
    • Divisheni
      • Miundombinu, Vijijini na Mijini
      • Huduma za Afya, Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Elimu ya Awali na Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Usimamizi wa Rasilimali Watu
    • Vitengo
      • Usimamizi wa Taka na Usafi wa Mazingira
      • Uhifadhi wa Maliasili na Mazingira
      • Michezo, Utamaduni na Sanaa
      • Fedha na Mahesabu
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Usimamizi wa Manunuzi
      • TEHAMA
      • Mawasiliano Serikalini
    • Kata
      • Bunju
      • Hananasif
      • Kawe
      • Kigogo
      • Kijitonyama
      • Kinondoni
      • Kunduchi
      • Mabwepande
      • Magomeni
      • Makongo
      • Makumbusho
      • Mbezi Juu
      • Mbweni
      • Mikocheni
      • Msasani
      • Mwananyamala
      • Mzimuni
      • Ndugumbi
      • Tandale
      • Wazo
    • Muundo wa Taasisi
    • Ofisi ya Mtendaji wa Kata
    • Ofisi ya Mtendaji wa Mtaa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya utalii
      • Fukwe na Visiwa
      • Sehemu za kitamaduni, ngoma za asili na sanaa za mikono
    • Utalii
      • Matukio ya Utalii
      • Royal Tour Bus
  • Huduma zetu
    • Biashara
    • Huduma za Elimu
    • Ujasiriamali
    • Ushauri katika Kilimo
    • Vituo vya Ukusanyaji Mapato
    • Vibali vya Ujenzi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Uongozi
      • Mipangomiji na Mazingira
      • Maadili
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhibiti UKIMWI
    • Ratiba ya Vikao
    • Ratiba ya Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Sera
    • Makala
    • Mpango mkakati
    • Taarifa mbalimbali
    • Mkataba wa huduma kwa mteja
    • Fomu za maombi
    • Vibali vya Ujenzi Vilivyotolewa
    • Nyaraka za Elimu

ZAIDI YA NYUMBA 100 ZIMEBOMOKA NA NYINGINE 700 KUZUNGUKWA NA MAJI WILAYA YA KINONDONI.

Tarehe iliyowekwa: October 30th, 2017

 NI KUFUATIA MVUA ZINAZOENDELEA KUNYESHA NA KUSABABISHA ATHARI KUBWA IKIWEMO WATU WAWILI KUPOTEZA MAISHA. 

 Watu wawili Wilaya ya Kinondoni wanasadikiwa kupoteza maisha kufuatia mvua kubwa zinazoendele kunyesha katika jiji la Dar es salaam 

 Hayo yamethibitishwa na Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni Mh Alli Hapi alipofanya ziara katika maeneo mbalimbali ya Wilaya hiyo kwa lengo la kujionea hali halisi ya athari zilizosababishwa na mvua.

 "Leo kama mnavyofahamu kumekuwepo na mvua ambazo zimeleta madhara makubwa katika Wilaya yetu ya Kinondoni, ziko taarifa ambazo zimethibitisha mpaka sasa tunao wananchi wawili ambao wamepoteza maisha kutokana na mvua ambazo zinaendelea, tunaendelea kukusanya taarifa kutoka maeneo mengine kupitia jeshi la polisi lakini mpaka sasa idadi iliyothibitika ni wawili," Amebainisha Hapi 

 Amesema takribani nyumba mia moja zimebomoka kufuatia mvua hizo na nyingine  mia saba kuzungukwa na maji kitu ambacho kimeleta  athari  kwa wananchi waliowengi katika maeneo hayo.

 "Tunazo nyumba ambazo ni zaidi ya mia saba ambazo zinakadiriwa zimezungukwa na maji lakini kadhalika tunazo nyumba zaidi ya  mia moja ambazo zinasadikika zimebomoka katika kata zetu zote na katika mitaa mbalimbali ya Wilaya ya Kinondoni, mvua ambazo zimenyesha zimeleta madhara makubwa sana "Amesema Hapi .

 Aidha amewataka Maafisa Mipangomiji wa Manispaa kuhakikisha wanafuatilia uhalali wa maeneo hayo kwa ramani za Mipangomiji na kujiridhisha kama maeneo hayo yaliyoathirika yalitengwa kwa ajili ya makazi ya watu. 

 "Maafisa Mipangomiji, angalieni uhalali wa maeneo haya, yalitengwa kwa matumizi gani "Alisisitiza Hapi 

 Ameongeza kuwa kwa mujibu wa sheria, Mwananchi yeyote anapaswa kujenga umbali wa mita 60 kutoka  chanzo cha mto.

 Katika hatua nyingine amewataka wananchi waliojenga maeneo hatarishi kuhakikisha wanachukua tahadhari ili kuepukana na madhara yanayoweza kutokea kufutia mvua hizi zinazoendelea kunyesha. 

 "Wako baadhi ya wananchi wetu ambao wamejenga katika meneo yasiyoruhusiwa kisheria, kule mbezi kunawanchi wamejenga kandokando ya mto na sheria yetu inasema mita 60 kutoka chanzo cha mto haparuhusiwi kujengwa nyumba yeyote, wako baadhi ya wananchi wamejenga kwenye mabonde, maeneo ya mkondo wa maji maeneo ya mabonde na mabwawa hawa ndio wananchi ambao wamekuwa wahanga wakubwa sana wa mvua hizi ambazo zinaendelea kwa hiyo nitoe wito tu kwa wanachi wote ambao wako katika meneo hatarishi, waondoke haraka kupisha yanayoweza kujitokeza, wenzetu wa hali ya hewa wanasema mvua hizi zinaweza kuendelea na zinaweza kushika kasi zaidi ya hapa tuliposhuhudia"Amesisitiza Hapi. 

 Ametoa wito kwa wananchi kuvuta subira wakati Serikali inajipanga kutatua changamoto zilizotokana na mvua hizo na mamlaka husika kupiga dawa kwenye mabwawa, na madimbwi ikiwa ni pamoja na kusafisha mitaro kama hatua za awali za kujilinda dhidi ya mgonjwa ya mlipuko kama vile kipindupindu. 

 Maeneo aliyoyatembelea Mkuu huyo wa wilaya ni Boko basihaya lililopo kata ya Bunju, Mto Nyakasangwe, Mto Mpiji ulioko Kata ya Mbweni, Daraja la Mbezi, eneo la Msisiri b,  lililoko Kata ya Mwananyamala. 

 Imetolewa na
 Kitengo cha Uhusiano
 Manispaa ya Kinondoni

Matangazo

  • UTOAJI WA MIKOPO KWA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU April 01, 2025
  • TANGAZO March 22, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI October 05, 2024
  • MATOKEO YA USAILI WA VITENDO KADA YA AFISA TEHAMA MSAIDIZI ULIOFANYIKA TAREHE 25/03/2024 March 25, 2024
  • Tazama zote

Habari mpya

  • ZAIDI YA MITI 1200 YAPANDWA KUADHIMISHA MIAKA 63 YA UHURU

    December 09, 2024
  • MAAMBUKIZI UKIMWI YAPUNGUA

    December 01, 2024
  • MAAMBUKIZI YA VIRUSI VYA UKIMWI YASHUKA KINONDONI

    November 29, 2024
  • WENYEVITI NA WAJUMBE WAPYA WAPEWA MAELEKEZO YA MAJUKUMU YAO

    November 28, 2024
  • Tazama zote

Picha Jongefu

IFAHAMU KATA YA MZIMUNI, MANISPAA YA KINONDONI
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • MWONGOZO WA NAMNA YA KUTUMIA MFUMO WA TAUSI
  • UJASIRIAMALI NA UTOAJI MIKOPO
  • MAKTABA YA PICHA
  • TAARIFA KWA UMMA
  • HOTUBA
  • ORODHA YA WAHESHIMIWA MADIWANI
  • MKATABA WA HUDUMA KWA MTEJA
  • MIRADI ILIYOKAMILIKA

Viunganishi Linganifu

  • TOVUTI KUU YA IKULU
  • TOVUTI YA UTUMISHI
  • TOVUTI YA OR-TAMISEMI
  • TOVUTI YA OFISI YA TAKWIMU YA TAIFA
  • TOVUTI YA IDARA YA HABARI MAELEZO
  • TOVUTI KUU YA SERIKALI

Idadi ya Wasomaji

world map hits counter

Waliotembelea tovuti

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    2 Barabara ya Morogoro, 14883 Dar es Salaam

    Anuani ya Posta: S.L.P 31902

    Simu ya mezani: +255222170173

    Simu ya mkononi: +255733241052

    Barua pepe: md@kinondonimc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya tovuti

Hatimiliki © 2017 Halmashauri ya Manispaa ya Kinondoni. Haki Zote Zimehifadhiwa.