• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
Kinondoni Municipal Council
Kinondoni Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Kinondoni

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Maadili ya Msingi
    • Wasifu wa Halmashauri
  • Utawala
    • Idara
      • Utawala na Utumishi
      • Afya na Usafishaji
      • Mipangomiji na Maendeleo ya Makazi
      • Kilimo na Mifugo
      • Elimu Sekondari
      • Elimu ya Awali na Msingi
      • Fedha na Biashara
      • Mipango na takwimu
      • Maendeleo ya Jamii
    • Vitengo
      • Sheria
      • Manunuzi
      • Ukaguzi wa ndani
      • TEHAMA
    • Kata
      • Bunju
      • Hananasif
      • Kawe
      • Kigogo
      • Kijitonyama
      • Kinondoni
      • Kunduchi
      • Mabwepande
      • Magomeni
      • Makongo
      • Makumbusho
      • Mbezi Juu
      • Mbweni
      • Mikocheni
      • Msasani
      • Mwananyamala
      • Mzimuni
      • Ndugumbi
      • Tandale
      • Wazo
    • Muundo wa utawala
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya utalii
      • Uwanda wa bahari, fukwe na visiwa
      • Sehemu za kitamaduni, ngoma za asili na sanaa za mikono
      • Matukio ya Utalii
    • Ufugaji
    • Kilimo cha mijini
  • Huduma zetu
    • Biashara
    • Huduma za Elimu
    • Maji na Usafishaji
    • Ujasiriamali na utoaji wa mikopo
    • Ushauri katika Kilimo
    • Elimu ya ufugaji, mifugo na uvuvi
    • Vituo vya Ukusanyaji Mapato
    • Vibali vya Ujenzi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Uongozi
      • Mipangomiji na Mazingira
      • Maadili
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhibiti UKIMWI
      • Baraza la Madiwani
    • Ratiba ya Vikao vya Kisheria
    • Ratiba ya Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Makala
    • Mpango mkakati
    • Taarifa mbalimbali
    • Mkataba wa huduma kwa mteja
    • Fomu za maombi
    • Vibali vya Ujenzi Vilivyotolewa
    • Nyaraka za Elimu
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video

Historia

 1 UTANGULIZI

1.1 TASWIRA YA MANISPAA YA KINONDONI

Halmashauri ya Manispaa ya Kinondoni ni moja kati ya Halmashauri tano (5) zinazounda Mkoa wa Dar es Salaam. Zingine ni Halmashauri ya Manispaa ya Temeke, Ubungo, Kigamboni na Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam.

Halmashauri ya Manispaa ya Kinondoni ilianzishwa kwa Sheria ya Serikali (Mamlaka za Miji) sura ya 288 kupitia Tangazo la Serikali (Government Notice No. 4) ya mwaka 2000 na Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa kama chombo huru, hivyo kuipa mamlaka ya kuongeza ubora wa utoaji huduma kwa wananchi wake.

1.2 MIPAKA YA ENEO

Halmashauri ya Manispaa ya Kinondoni inapakana na Bahari ya Hindi kwa upande wa Mashariki, Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam kwa upande wa Kusini, Wilaya ya Bagamoyo kwa upande wa Kaskazini na Wilaya ya Ubungo kwa upande wa Magharibi. Halmashauri inaunganishwa na sehemu nyingine za miji na nchi kwa mtandao wa barabara za mawasiliano. Barabara kuu ni pamoja na barabara ya Morogoro, Bagamoyo, Kawawa, barabara ya Sam Nujoma, Mwai Kibaki na Ally Hassan Mwinyi.

1.3 HALI YA HEWA:

Hali ya hewa ya Manispaa ya Kinondoni ni ya joto la wastani wa nyuzi joto 290C kwa mwaka. Kipindi cha joto huanzia kati ya miezi ya Oktoba hadi Machi, wakati kipindi cha baridi chenye kadirio la nyuzi joto 250C huanzia kati ya miezi ya Mei hadi Agosti na nyuzi joto 29 – 330C kwa miezi iliyosalia katika kipindi cha mwaka. Wastani wa mvua kwa mwaka ni mm 1,300 katika misimu miwili ambayo ni vuli miezi ya Oktoba – Desemba na Masika ambayo huanza miezi ya Machi – Mei.

1.4 ENEO NA IDADI YA WATU

Halmashauri ya Manispaa ya Kinondoni ina ukubwa wa kilomita za mraba 321. Kwa mujibu wa Sensa ya Taifa ya idadi ya watu na makazi ya mwaka 2012, Manispaa ya Kinondoni ilikuwa na idadi ya watu wapatao 929,681. Kutokana na ongezeko la ukuaji wa idadi ya watu ya asilimia 5.0 kwa mwaka, Manispaa inakadiriwa kuwa na idadi ya watu wapatao 1,373,562 ifikapo mwaka 2020, hivyo kila kilometa ya mraba kuwa na ujazo wa watu 4,279.

1.5 UTAWALA

Kiutawala Halmashauri ya Manispaa ya Kinondoni imegawanyika katika Tarafa mbili (2) ambazo ni Kinondoni na Kawe, Kata ishirini (20) na Mitaa ni mia moja na sita (106) ya utawala. Idadi ya Majimbo ya Uchaguzi ni mawili (2) ambayo ni Majimbo ya Kinondoni na Kawe. Mkuu wa Wilaya ni Msimamizi Mkuu wa shughuli zote za Serikali katika Wilaya. Manispaa inaongozwa na Baraza la Madiwani lenye wajumbe ishirini na tisa (29) ambapo kuna Madiwani 26 na Wabunge 3 ambapo Mstahiki Meya ni Kiongozi Mkuu na Mkurugenzi wa Manispaa ni Mtendaji Mkuu kwa upande wa Serikali za Mitaa.

1.6 MAJUKUMU YA HALMASHAURI YA MANISPAA YA KINONDONI

Majukumu hayo ni kama ifuatavyo:-

  • Kuimarisha na kuwezesha amani, maagizo na utawala bora ndani ya eneo la utawala wake.
  • Kuweka msisitizo kwenye shughuli za ustawi wa kijamii na kiuchumi kwa watu wote waliopo ndani ya eneo la Halmashauri kulingana na Mipango na Sera ya Taifa kwa maendeleo ya Halmashauri, Halmashauri ina jukumu la kuendeleza maendeleo katika nyanja za kijamii na kiuchumi ndani ya eneo la Halmashauri.
  • Kuweka msisitizo na kuhakikisha ushirikishwaji wa kidemokrasia katika kutoa maagizo yanayohusu watu wenyewe.
  • Kuanzisha na kuimarisha vyanzo madhubuti vya mapato na vyanzo vingine ili kuwezesha Serikali za Mitaa kutekeleza kazi nyingine kikamilifu.
  • Kusimamia ujenzi wa miundombinu ya barabara, majengo, umeme na maji.
  • Kuimarisha na kuendeleza shughuli za biashara, viwanda, masoko na sekta zisizo rasmi.
  • Kutoa huduma za afya tiba, kinga na uboreshaji wa maendeleo ya jamii na ustawi wa jamii.
  • Usafi na udhibiti wa taka ngumu na maji taka katika eneo la Halmashauri.
  • Kusimamia na kutoa elimu ya Msingi na Sekondari katika eneo la Halmashauri.
  • Kusimamia na kuratibu mapambano ya kupunguza maambukizi ya UKIMWI na kudhibiti maambukizi mapya.
  • Kusimamia utekelezaji Sera, Sheria za nchi na Sheria ndogo za Halmashauri.

Matangazo

  • MABADILIKO YA VITUO VYA KUFANYIA MAFUNZO YA SENSA July 30, 2022
  • MABADILIKO YA SIKU YA MAFUNZO YA WASIMAMIZI WA MAUDHUI, WASIMAMIZI WA TEHAMA NA MAKARANI WA SENSA YA WATU NA MAKAZI 2022 July 28, 2022
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE MAFUNZO YA SENSA KWA MAKARANI, WASIMAMIZI WA MAUDHUI NA TEHAMA TAREHE 27 JULAI, 2022 WILAYA YA KINONDONI July 27, 2022
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI WA NAFASI ZA KAZI ZA MUDA SENSA 2022 July 19, 2022
  • Tazama zote

Habari mpya

  • "AHIMIZA UADILIFU WAKATI WA SENSA" DC GONDWE KINONDONI

    July 28, 2022
  • KAMATI YA HUDUMA ZA UCHUMI AFYA NA ELIMU KINONDONI IMEFANYA ZIARA KATA YA KAWE

    July 28, 2022
  • ZIARA YA KAMATI YA KUDHIBITI UKIMWI KINONDONI YATEMBELEA KATA YA TANDALE NA ASASI YA PHSRF

    July 27, 2022
  • ZIARA YA KAMATI YA KUDHIBITI UKIMWI KINONDONI YATEMBELEA KATA YA TANDALE NA ASASI YA PHSRF

    July 27, 2022
  • Tazama zote

Picha Jongefu

UTEKELEZAJI WA MIRADI YA MAENDELEO
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • TARATIBU ZA KUPATA KIBALI CHA UJENZI
  • MKATABA WA HUDUMA KWA MTEJA
  • UJASIRIAMALI NA UTOAJI MIKOPO
  • VITUO VYA KUKUSANYIA MAPATO
  • ORODHA YA WAHESHIMIWA MADIWANI
  • RATIBA YA MSTAHIKI MEYA
  • TAARIFA KWA UMMA
  • MIRADI ILIYOKAMILIKA

Viunganishi Linganifu

  • TOVUTI KUU YA IKULU
  • TOVUTI YA UTUMISHI
  • TOVUTI YA OR-TAMISEMI
  • TOVUTI YA OFISI YA TAKWIMU YA TAIFA
  • TOVUTI YA IDARA YA HABARI MAELEZO
  • TOVUTI KUU YA SERIKALI

Idadi ya Wasomaji

world map hits counter

Waliotembelea tovuti

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    2 Barabara ya Morogoro, 14883 Dar es Salaam

    Anuani ya Posta: S.L.P 31902

    Simu ya mezani: +255 22 2170173

    Simu ya mkononi:

    Barua pepe: md@kinondonimc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya tovuti

Hatimiliki © 2017 Halmashauri ya Manispaa ya Kinondoni. Haki Zote Zimehifadhiwa.