• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
Kinondoni Municipal Council
Kinondoni Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Kinondoni

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Maadili ya Msingi
    • Wasifu wa Halmashauri
  • Utawala
    • Divisheni
      • Miundombinu, Vijijini na Mijini
      • Huduma za Afya, Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Elimu ya Awali na Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Usimamizi wa Rasilimali Watu
    • Vitengo
      • Usimamizi wa Taka na Usafi wa Mazingira
      • Uhifadhi wa Maliasili na Mazingira
      • Michezo, Utamaduni na Sanaa
      • Fedha na Mahesabu
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Usimamizi wa Manunuzi
      • TEHAMA
      • Mawasiliano Serikalini
    • Ofisi ya Mtendaji wa Kata
    • Ofisi ya Mtendaji wa Mtaa
    • Kata
      • Bunju
      • Hananasif
      • Kawe
      • Kigogo
      • Kijitonyama
      • Kinondoni
      • Kunduchi
      • Mabwepande
      • Magomeni
      • Makongo
      • Makumbusho
      • Mbezi Juu
      • Mbweni
      • Mikocheni
      • Msasani
      • Mwananyamala
      • Mzimuni
      • Ndugumbi
      • Tandale
      • Wazo
    • Muundo wa Taasisi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Fukwe na Visiwa
    • Sehemu za kitamaduni, ngoma za asili na sanaa za mikono
    • Matukio ya Utalii
  • Huduma zetu
    • Biashara
    • Huduma za Elimu
    • Ujasiriamali
    • Ushauri katika Kilimo
    • Vituo vya Ukusanyaji Mapato
    • Vibali vya Ujenzi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Uongozi
      • Mipangomiji na Mazingira
      • Maadili
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhibiti UKIMWI
    • Ratiba ya Vikao
    • Ratiba ya Meya
  • Miradi
    • Iliyopangwa
    • Inayoendelea
    • Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Sera
    • Makala
    • Mpango mkakati
    • Taarifa mbalimbali
    • Mkataba wa huduma
    • Fomu za maombi
    • Vibali vya Ujenzi
    • Nyaraka za Elimu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video
    • Habari
    • Matukio

Bunju

HISTORIA FUPI:

Kata ya Bunju ni miongoni mwa Kata kongwe ndani ya Manispaa ya Kinondoni. Jengo la ofisi ya Kata hii lilizinduliwa tarehe 29/06/2001 na kiongozi wa mbio za Mwenge Kitaifa wa Mwaka huo ambaye ni Ndg. Fatma Juma Shomari.

Bunju imetokana na neno samaki anayeitwa jina la Bunju. Hapo awali wakazi wa eneo la Kata ya ya Bunju walikuwa wafugaji ambao walitekeleza shughuli zao za uvuvi katika bahari ya Hindi.

Eneo la kati la Kata ya Bunju lilikuwa na kijiji ambacho kulikuwa na vitongoji ambavyo mojawapo ni Mabwepande ambapo kwa sasa ni Bunju B. Lakini pia Mabwepande ilikuwa inasimamiwa na Kata ya Bunju na ilikuwa na Mitaa miwili ambayo ni Boko na Bunju A.

Kuna mchanganyiko wa makabila mbalimbali ndani ya Kata ya Bunju ikiwemo Wakwere, Wazaramo na Wandengereko.


IDADI YA MITAA:

Kata ya Bunju ina jumla ya mitaa sita (06) kama ifuatavyo:-

1.    Mtaa wa Basihaya

2.    Mtaa wa Boko

3.    Mtaa wa Dovya

4.    Mtaa wa Kilungule

5.    Mtaa wa Mkoani

6.    Mtaa wa Bunju A


HALI YA ELIMU:

Hali ya elimu katika Kata ni ya kuridhisha na wanafunzi wake hujitahidi kufikia lengo la ufaulu kwa asilimia zinazotakiwa. Kata hii inazo shule za awali, msingi na sekondari ambazo ni za serikali na za binafsi. Pia Kata ina vyuo vya elimu ya kati.


SHULE ZA AWALI NA ZA MSINGI ZA SERIKALI:

Kata ya Bunju inazo shule za awali na msingi saba (7) za serikali kama ifuatavyo: -

  1. Bunju A
  2. Kheri Missinga
  3. Ally Hapi
  4. Boko
  5. Boko NHC
  6. Mtambani
  7. Bunju Mkoani


SHULE ZA AWALI NA ZA MSINGI ZA BINAFSI:

Kata ya Bunju inazo shule za awali kumi na tano (15) za binafsi kama ifuatavyo: -

Moga, Faith, Gosheni, Siya Modern, New Hazina, Abel Memorial, Prestige, Mt. Sinai, Stamarial Salome, Daystar, Locee, Turkish Maarif, Jubilation, Rev. Fr. Jagques, Mareisuvat.


SHULE ZA SEKONDARI ZA SERIKALI:

Kata ya Bunju inazo shule tatu (03) za sekondari za serikali kama ifuatavyo: -  

  1. Boko
  2. Boko Mtambani
  3. Bunju A


SHULE ZA SEKONDARI ZA BINAFSI:

Kata ya Bunju inazo shule nane (08) za sekondari za binafsi kama ifuatavyo: -  

  1. Destine
  2. Fanaka
  3. Mianzini
  4. Stamaria
  5. Salome
  6. Lyceum
  7. John the Baptist
  8. Faith


VYUO VYA ELIMU YA KATI VYA BINAFSI:

Kata ya Bunju inavyo vyuo viwili (02) vya elimu ya kati vya binafsi.


HALI YA AFYA:

Hali ya Afya katika Kata ya Bunju ni ya kuridhisha kwani ina Vituo vya Afya na Zahanati za serikali na binafsi.


KITUO CHA AFYA KILICHOPO KATA YA BUNJU:

Kituo cha Afya kilichopo ni kimoja ambacho ni cha serkikali ambacho kinaitwa Kituo cha Afya Bunju.


ZAHANATI ZA SERIKALI KATA YA BUNJU:

Kata ya Bunju ina Zahanati mbili (02) za serikali kama ifuatavyo: -

  1. Zahanati ya Boko inayohudumia wakazi wa Mtaa wa Boko, Basihaya na maeneo ya jirani.
  2. Zahanati ya Bunju inayohudumia maeneo yote yanayozunguka Bunju na Vitongoji vyake.


ZAHANATI ZA BINAFSI KATA YA BUNJU:

Kata ya Bunju ina Zahanati nane (08) za binafsi kama ifuatavyo: -

Tobson, St. Joseph, Sandary, Med Check, Agakhan Cilinic, Arafa Vigen, Burumawe Specilied Clinic Honest, Nyota Njema


HALI YA MIUNDOMBINU YA BARABARA NA MIFEREJI:

Kata ya Bunju inazungukwa na barabara za lami nne ambazo ni Barabara ya Boko Chama kwenda Ununio na kutokea Kunduchi ambayo pia ina mifereji ya maji ya mvua, pia kuna barabara ya njia panda Mbweni kwenda Malindi Mbweni na ambayo pia ina mifereji na barabara nyingine kuanzia Kilungule kwenda Mbweni. Lakini pia Kata ya Bunju inapitiwa na barabara kubwa ya Bagamoyo kwa mitaa yote sita.


HALI YA USAFI NA MAZINGIRA:

Hali ya usafi wa Kata ya Bunju ni wa kuridhisha, kwani mitaa yote sita inayo Wakandarasi wanaozoa taka na kusafirisha kwenda dampo.


MAHUSIANO NA WADAU:

Katika Kata ya Bunju, mdau mkubwa wa maendeleo ni kiwanda cha saruji cha Wazo ambacho mara kadhaa kimekuwa kikisaidia maendeleo katika mitaa ya Basihaya na Boko hasa katika kusaidia vifusi vya barabara, vyandarua na mazingira. Wadau wengine wanaosaidia katika Kata ni pamoja na: BARRIEL SHELI,  ATN SHELI, APC, OILCOM SHELI, GUDAL SHELI, TOOTHPICK INDUSTRY LTD, DSN ENERGY (T) LTD (KIWANDA CHA MKAA), COLD BREWERIES  ARIES, PRODUCT AZURA  KIWANDA  CHA POMBE), KIWANDA CHA GYPSUM.


MIRADI YA KUJIVUNIA:

Kata ya Bunju inajivunia hasa katika miradi ya elimu kwani pamoja na kuwa na shule nne za msingi na shule mbili za Sekondari bado imeanzisha ujenzi mpya wa shule ya msingi katika mtaa wa Mkoani.


HALI YA MAENDELEO YA WATU NA MAKAZI:

Hali ya maendeleo ya watu na makazi inakua kwa kasi kwa kuwa watu wengi wamejenga nyumba za kisasa hasa katika eneo la mradi wa viwanja 2000 (Bunju Beach), na eneo la Boko beach ambako kuna miundombinu yote ya mipangomiji.

Pia katika maeneo yasiyopimwa ujenzi unafanyika kwa kasi.

Matangazo

  • KUFUTA TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI March 14, 2023
  • TANGAZO LA AJIRA YA MKATABA March 13, 2023
  • TANGAZO KWA WASIOLIPIA VIWANJA BOKO DOVYA (KWA SOMJI) NA SALASALA February 15, 2023
  • MABADILIKO YA SIKU YA MAFUNZO YA WASIMAMIZI WA MAUDHUI, WASIMAMIZI WA TEHAMA NA MAKARANI WA SENSA YA WATU NA MAKAZI 2022 July 28, 2022
  • Tazama zote

Habari mpya

  • JAPAN YAIPATIA MSAADA MZIMUNI SEKONDARI

    March 15, 2023
  • VIKUNDI VYAASWA MATUMIZI SAHIHI YA MIKOPO

    February 18, 2023
  • "HAKUNA TIMU KUBWA ZAIDI YA KMC FC"

    February 18, 2023
  • ULINZI NI KIPAUMBELE KINODONI-DC SAAD

    February 12, 2023
  • Tazama zote

Picha Jongefu

VIKUNDI VILIVYOSEPA NA BILIONI 11 VYAKALIWA KOONI MANISPAA YA KINONDONI. REJESHENI...
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • MWONGOZO WA NAMNA YA KUTUMIA MFUMO WA TAUSI
  • UJASIRIAMALI NA UTOAJI MIKOPO
  • TARATIBU ZA KUPATA KIBALI CHA UJENZI
  • TAARIFA KWA UMMA
  • RATIBA YA MSTAHIKI MEYA
  • ORODHA YA WAHESHIMIWA MADIWANI
  • MKATABA WA HUDUMA KWA MTEJA
  • MIRADI ILIYOKAMILIKA

Viunganishi Linganifu

  • TOVUTI KUU YA IKULU
  • TOVUTI YA UTUMISHI
  • TOVUTI YA OR-TAMISEMI
  • TOVUTI YA OFISI YA TAKWIMU YA TAIFA
  • TOVUTI YA IDARA YA HABARI MAELEZO
  • TOVUTI KUU YA SERIKALI

Idadi ya Wasomaji

world map hits counter

Waliotembelea tovuti

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    2 Barabara ya Morogoro, 14883 Dar es Salaam

    Anuani ya Posta: S.L.P 31902

    Simu ya mezani: +255 22 2170173

    Simu ya mkononi:

    Barua pepe: md@kinondonimc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya tovuti

Hatimiliki © 2017 Halmashauri ya Manispaa ya Kinondoni. Haki Zote Zimehifadhiwa.