• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
Kinondoni Municipal Council
Kinondoni Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Kinondoni

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Maadili ya Msingi
    • Wasifu wa Halmashauri
  • Utawala
    • Divisheni
      • Miundombinu, Vijijini na Mijini
      • Huduma za Afya, Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Elimu ya Awali na Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Usimamizi wa Rasilimali Watu
    • Vitengo
      • Usimamizi wa Taka na Usafi wa Mazingira
      • Uhifadhi wa Maliasili na Mazingira
      • Michezo, Utamaduni na Sanaa
      • Fedha na Mahesabu
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Usimamizi wa Manunuzi
      • TEHAMA
      • Mawasiliano Serikalini
    • Ofisi ya Mtendaji wa Kata
    • Ofisi ya Mtendaji wa Mtaa
    • Kata
      • Bunju
      • Hananasif
      • Kawe
      • Kigogo
      • Kijitonyama
      • Kinondoni
      • Kunduchi
      • Mabwepande
      • Magomeni
      • Makongo
      • Makumbusho
      • Mbezi Juu
      • Mbweni
      • Mikocheni
      • Msasani
      • Mwananyamala
      • Mzimuni
      • Ndugumbi
      • Tandale
      • Wazo
    • Muundo wa Taasisi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Fukwe na Visiwa
    • Sehemu za kitamaduni, ngoma za asili na sanaa za mikono
    • Matukio ya Utalii
  • Huduma zetu
    • Biashara
    • Huduma za Elimu
    • Ujasiriamali
    • Ushauri katika Kilimo
    • Vituo vya Ukusanyaji Mapato
    • Vibali vya Ujenzi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Uongozi
      • Mipangomiji na Mazingira
      • Maadili
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhibiti UKIMWI
    • Ratiba ya Meya
    • Ratiba ya Vikao
  • Miradi
    • Iliyopangwa
    • Inayoendelea
    • Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Makala
    • Mpango mkakati
    • Taarifa mbalimbali
    • Mkataba wa huduma
    • Fomu za maombi
    • Vibali vya Ujenzi
    • Nyaraka za Elimu
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video
    • Habari

WITO WATOLEWA KWA WANANCHI WAISHIO NA WATU WENYE ULEMAVU WILAYA YA KINONDONI

Tarehe iliyowekwa: September 12th, 2018

KUHAKIKISHA WANASHIRIKIANA NA NIDA WILAYANI HAPO, KUWASAJILI KATIKA DAFTARI LA TAIFA NA KUWATAMBUA KWA LENGO LA KUPATIWA VITAMBULISHO VYA TAIFA.

Wito huo umetolewa leo na Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni Mhe.Daniel Chongolo, alipokuwa mgeni rasmi kwenye zoezi la usajili na utambuzi wa watu wenye ulemavu kwenye daftari la Taifa, lililofanywa na NIDA, kwa kushirikiana na SHIVYAWATA, pamoja na Ofisi ya Ustawi wa Jamii Manispaa ya Kinondoni, kwa lengo la kupatiwa vitambulisho vya Taifa.

Amesema zoezi hili ni zuri, kwani kwa kufanya hivi ni kutekeleza haki ya msingi kikatiba na pia ni kutoa fursa ya watu wenye ulemavu kusajiliwa na kupatiwa vitambulisho vya Taifa, na kuwataka wananchi wanaoishi nao majumbani, kuhakikisha wanawaleta kwa ajili ya zoezi hilo la siku tatu la utambuzi na uandikishaji linaloendelea katika shule ya Ndugumbi Manispaa ya Kinondoni.

"Wito wangu kwa wanakinondoni, wito wangu kwa wale wanaoishi na watu wenye ulemavu, naomba sana ndani ya siku tatu hizi, muwashawishi, wawalete, wawape fursa watu wenye ulemavu kutumia haki yao ya msingi waliyopewa ya kujisajili kwenye daftari la Taifa, kwa ajili ya kupata vitambulisho vya Taifa".Amesisitiza Chongolo.

Awali akitoa taarifa ya zoezi hilo, Afisa Msajili wa NIDA Wilaya ya Kinondoni Ndg. Dickson Mmbaga amesema, kwa kushirikiana na Ofisi ya Mkurugenzi Kinondoni kupitia zoezi hili tumetambua, tumesajili, tumeweka mazingira wezeshi na kupata takwimu zitakazosaidia kuboresha maendeleo ya watu wenye ulemavu, ikiwa ni pamoja na kupatiwa vitambulisho vya Taifa vitakavyowasaidia katika shughuli zao mbalimbali.

Aidha amezitaja faida za kupatiwa vitambulisho vya Taifa kuwa ni kurahisisha upatikanaji wa huduma zote za msingi, kumtambulisha mtu mwenye ulemavu anapohitaji huduma, kumuwezesha kujidhamini kama anahitajika kufanya hivyo, kurahisisha zoezi la kuhesabu watu, pamoja na kuimarisha ulinzi na usalama wa watu wenye ulemavu.

Naye Mwenyekiti wa SHIVYAWATA Wilaya ya Kinondoni, Bi.Subira Semsimbazi alipokuwa akitoa salaam za shukrani kwa Mkuu huyo wa Wilaya, ameainisha changamoto zinazowakabili kuwa ni ukosefu wa ofisi, ukosefu wa wakalimani, kutopatiwa huduma za bima afya, na pia kutopatiwa mikopo ya wanawake na vijana ili waweze kujishughulisha na shughuli za ujasiriamali.

Zoezi hili la utambuzi na usajili wa watu wenye ulemavu kwenye daftari la Taifa, kwa ajili ya kupatiwa vitambulisho vya Taifa linafanyika kwa siku tatu katika shule ya msingi Ndugumbi iliyoko Manispaa ya Kinondoni.

Imeandaliwa na

Kitengo cha Uhusiano na Habari.

Manispaa ya Kinondoni.

Matangazo

  • PONGEZI June 07, 2023
  • TANGAZO LA UUZAJI WA VIWANJA May 19, 2023
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI-DEREVA DARAJA II April 24, 2023
  • MABADILIKO YA SIKU YA MAFUNZO YA WASIMAMIZI WA MAUDHUI, WASIMAMIZI WA TEHAMA NA MAKARANI WA SENSA YA WATU NA MAKAZI 2022 July 28, 2022
  • Tazama zote

Habari mpya

  • AFISA ELIMU MSINGI KINONDONI APONGEZWA

    May 19, 2023
  • JAPAN YAIPATIA MSAADA MZIMUNI SEKONDARI

    March 15, 2023
  • VIKUNDI VYAASWA MATUMIZI SAHIHI YA MIKOPO

    February 18, 2023
  • "HAKUNA TIMU KUBWA ZAIDI YA KMC FC"

    February 18, 2023
  • Tazama zote

Picha Jongefu

VITUO VITANO VYA MSAADA WA MFUMO WA TAUSI, KITUO CHA MIITO YA SIMU KUBORESHA UKUSANYAJI WA MAPATO
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • MWONGOZO WA NAMNA YA KUTUMIA MFUMO WA TAUSI
  • UJASIRIAMALI NA UTOAJI MIKOPO
  • TARATIBU ZA KUPATA KIBALI CHA UJENZI
  • TAARIFA KWA UMMA
  • RATIBA YA MSTAHIKI MEYA
  • ORODHA YA WAHESHIMIWA MADIWANI
  • MKATABA WA HUDUMA KWA MTEJA
  • MIRADI ILIYOKAMILIKA

Viunganishi Linganifu

  • TOVUTI KUU YA IKULU
  • TOVUTI YA UTUMISHI
  • TOVUTI YA OR-TAMISEMI
  • TOVUTI YA OFISI YA TAKWIMU YA TAIFA
  • TOVUTI YA IDARA YA HABARI MAELEZO
  • TOVUTI KUU YA SERIKALI

Idadi ya Wasomaji

world map hits counter

Waliotembelea tovuti

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    2 Barabara ya Morogoro, 14883 Dar es Salaam

    Anuani ya Posta: S.L.P 31902

    Simu ya mezani: +255 22 2170173

    Simu ya mkononi:

    Barua pepe: md@kinondonimc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya tovuti

Hatimiliki © 2017 Halmashauri ya Manispaa ya Kinondoni. Haki Zote Zimehifadhiwa.