• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
Kinondoni Municipal Council
Kinondoni Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Kinondoni

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Maadili ya Msingi
    • Wasifu wa Halmashauri
  • Utawala
    • Divisheni
      • Miundombinu, Vijijini na Mijini
      • Huduma za Afya, Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Elimu ya Awali na Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Usimamizi wa Rasilimali Watu
    • Vitengo
      • Usimamizi wa Taka na Usafi wa Mazingira
      • Uhifadhi wa Maliasili na Mazingira
      • Michezo, Utamaduni na Sanaa
      • Fedha na Mahesabu
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Usimamizi wa Manunuzi
      • TEHAMA
      • Mawasiliano Serikalini
    • Kata
      • Bunju
      • Hananasif
      • Kawe
      • Kigogo
      • Kijitonyama
      • Kinondoni
      • Kunduchi
      • Mabwepande
      • Magomeni
      • Makongo
      • Makumbusho
      • Mbezi Juu
      • Mbweni
      • Mikocheni
      • Msasani
      • Mwananyamala
      • Mzimuni
      • Ndugumbi
      • Tandale
      • Wazo
    • Muundo wa Taasisi
    • Ofisi ya Mtendaji wa Kata
    • Ofisi ya Mtendaji wa Mtaa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya utalii
      • Fukwe na Visiwa
      • Sehemu za kitamaduni, ngoma za asili na sanaa za mikono
    • Utalii
      • Matukio ya Utalii
      • Royal Tour Bus
  • Huduma zetu
    • Biashara
    • Huduma za Elimu
    • Ujasiriamali
    • Ushauri katika Kilimo
    • Vituo vya Ukusanyaji Mapato
    • Vibali vya Ujenzi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Uongozi
      • Mipangomiji na Mazingira
      • Maadili
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhibiti UKIMWI
    • Ratiba ya Vikao
    • Ratiba ya Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Sera
    • Makala
    • Mpango mkakati
    • Taarifa mbalimbali
    • Mkataba wa huduma kwa mteja
    • Fomu za maombi
    • Vibali vya Ujenzi Vilivyotolewa
    • Nyaraka za Elimu

WITO WATOLEWA KWA ASASI ZA KIRAIA KUSHIRIKI KAMPENI YA UBORESHAJI MIUNDOMBINU YA ELIMU KINONDONI

Tarehe iliyowekwa: January 30th, 2019

Wito huo umetolewa leo na Afisa maendeleo ya jamii Manispaa hiyo Bi Halima Kahema, alipokuwa akifungua mkutano wa siku moja uliowakutanisha wadau wa maendeleo, maafisa maendeleo ya jamii wa Kata pamoja na Taasisi zisizo za kiserikali zinazofanya shughuli zake katika Manispaa hiyo, kwa lengo la kujadili mstakabali mzima wa maboresho ya miundombinu ya Elimu na utatuzi wa changamoto zilizopo katika sekta hiyo.

Amesema katika kumuunga mkono Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania kwenye swala zima la elimu, Asasi za Kiraia na Taasisi zisizo za kiserikali ni vema kuwa na mchango wake wa hiari katika hili.

"Elimu ni yetu sote, hivyo ninyi Asasi za kiraia mliopo Kinondoni, tukishirikiana kwa pamoja kuongeza nguvu katika hili, hakika tutakuwa tumetatua Changamoto kubwa sana katika sekta hii nyeti, ambayo Rais wetu wa awamu ya tano ameipa kipaumbele cha kutosha" Amesisitiza Bi.Kahema.

Awali  akifafanua changamoto ya upungufu wa vyumba vya madarasa katika Halmasahuri hiyo,  Afisa Elimu taaluma  Bw Japhet Moshi amesema, upungufu wa vyumba vya madarasa kwa shule za sekondari pekee ni 103, kwani  idadi ya wanafunzi waliomaliza kidato cha nne mwaka jana ni 4,054,  na waliochaguliwa kujiunga  kidato cha kwanza mwaka huu ni 11,562.

 Amezitaja changamoto nyingine kuwa ni uhaba wa mabweni, matundu ya vyoo vya wanafunzi, nyumba za walimu, huduma ya maji na chakula mashuleni, mazingira, watoto yatima, watoto wanaoishi kwenye mazingira magumu na huduma za afya.

Naye Balozi wa Uturuki nchini Tanzania Bw Mohammed Yusuph, alipotakiwa kuzungumza aliahidi kushirikiana na Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania katika kuhakikisha maswala ya miundombinu ya elimu, pamoja na watoto waishio katika mazingira hatarishi yanapatiwa suluhisho kwa kiasi cha kuridhisha, ili miundombinu ya elimu iweze kuboreshwa.

Mkutano huo uliofanyika katika ukumbi wa shule ya Msingi Oysterbay umekutanisha Asasi za Kiraia zaidi ya 400, kwa lengo la kuelezea na kuainisha mpango wa Halmashauri wa kujenga vyumba 100 vya madarasa ili kupambana na changamoto hiyo ambayo ndio kikwazo kikubwa katika sekta hii.

Imeandaliwa na

Kitengo Cha Habari na uhusiano

Manispaa ya Kinondoni.

Matangazo

  • UTOAJI WA MIKOPO KWA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU April 01, 2025
  • TANGAZO March 22, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI October 05, 2024
  • MATOKEO YA USAILI WA VITENDO KADA YA AFISA TEHAMA MSAIDIZI ULIOFANYIKA TAREHE 25/03/2024 March 25, 2024
  • Tazama zote

Habari mpya

  • ZAIDI YA MITI 1200 YAPANDWA KUADHIMISHA MIAKA 63 YA UHURU

    December 09, 2024
  • MAAMBUKIZI UKIMWI YAPUNGUA

    December 01, 2024
  • MAAMBUKIZI YA VIRUSI VYA UKIMWI YASHUKA KINONDONI

    November 29, 2024
  • WENYEVITI NA WAJUMBE WAPYA WAPEWA MAELEKEZO YA MAJUKUMU YAO

    November 28, 2024
  • Tazama zote

Picha Jongefu

IFAHAMU KATA YA MZIMUNI, MANISPAA YA KINONDONI
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • MWONGOZO WA NAMNA YA KUTUMIA MFUMO WA TAUSI
  • UJASIRIAMALI NA UTOAJI MIKOPO
  • MAKTABA YA PICHA
  • TAARIFA KWA UMMA
  • HOTUBA
  • ORODHA YA WAHESHIMIWA MADIWANI
  • MKATABA WA HUDUMA KWA MTEJA
  • MIRADI ILIYOKAMILIKA

Viunganishi Linganifu

  • TOVUTI KUU YA IKULU
  • TOVUTI YA UTUMISHI
  • TOVUTI YA OR-TAMISEMI
  • TOVUTI YA OFISI YA TAKWIMU YA TAIFA
  • TOVUTI YA IDARA YA HABARI MAELEZO
  • TOVUTI KUU YA SERIKALI

Idadi ya Wasomaji

world map hits counter

Waliotembelea tovuti

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    2 Barabara ya Morogoro, 14883 Dar es Salaam

    Anuani ya Posta: S.L.P 31902

    Simu ya mezani: +255222170173

    Simu ya mkononi: +255733241052

    Barua pepe: md@kinondonimc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya tovuti

Hatimiliki © 2017 Halmashauri ya Manispaa ya Kinondoni. Haki Zote Zimehifadhiwa.