• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
Kinondoni Municipal Council
Kinondoni Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Kinondoni

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Maadili ya Msingi
    • Wasifu wa Halmashauri
  • Utawala
    • Divisheni
      • Miundombinu, Vijijini na Mijini
      • Huduma za Afya, Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Elimu ya Awali na Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Usimamizi wa Rasilimali Watu
    • Vitengo
      • Usimamizi wa Taka na Usafi wa Mazingira
      • Uhifadhi wa Maliasili na Mazingira
      • Michezo, Utamaduni na Sanaa
      • Fedha na Mahesabu
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Usimamizi wa Manunuzi
      • TEHAMA
      • Mawasiliano Serikalini
    • Kata
      • Bunju
      • Hananasif
      • Kawe
      • Kigogo
      • Kijitonyama
      • Kinondoni
      • Kunduchi
      • Mabwepande
      • Magomeni
      • Makongo
      • Makumbusho
      • Mbezi Juu
      • Mbweni
      • Mikocheni
      • Msasani
      • Mwananyamala
      • Mzimuni
      • Ndugumbi
      • Tandale
      • Wazo
    • Muundo wa Taasisi
    • Ofisi ya Mtendaji wa Kata
    • Ofisi ya Mtendaji wa Mtaa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya utalii
      • Fukwe na Visiwa
      • Sehemu za kitamaduni, ngoma za asili na sanaa za mikono
    • Utalii
      • Matukio ya Utalii
      • Royal Tour Bus
  • Huduma zetu
    • Biashara
    • Huduma za Elimu
    • Ujasiriamali
    • Ushauri katika Kilimo
    • Vituo vya Ukusanyaji Mapato
    • Vibali vya Ujenzi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Uongozi
      • Mipangomiji na Mazingira
      • Maadili
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhibiti UKIMWI
    • Ratiba ya Vikao
    • Ratiba ya Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Sera
    • Makala
    • Mpango mkakati
    • Taarifa mbalimbali
    • Mkataba wa huduma kwa mteja
    • Fomu za maombi
    • Vibali vya Ujenzi Vilivyotolewa
    • Nyaraka za Elimu

WAZEE WAISHIO KINONDONI WAFUATWE KWENYE KATA KUANDIKISHWA ILI WAPATIWE KADI ZA MSAMAHA WA MATIBABU

Tarehe iliyowekwa: October 6th, 2017

  Wazee waishio  Wilaya ya Kinondoni wametakiwa kufuatwa kwenye Kata, Mitaa na maeneo wanayoishi ili waweze kutambuliwa kwa lengo la  kupatiwa kadi za msamaha wa matibabu. 

 Agizo hilo limetolewa na Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni Mh Ali Hapi alipozuru katika kata ya Wazo na kukutana na wananchi wa mtaa wa kilimahewa kwenye mkutano wa hadhara uliofanyika viwanjani hapo. 

 Amesema lengo la ziara yake ni ya kiserikali na kikazi pia, yenye nia ya kukutana na wananchi wa eneo husika kwa lengo la kusikiliza kero na changamoto zinazowakabili  ili ziweze kupatiwa ufumbuzi wa kudumu. 

 "Nimepewa kazi na Mh Rais, kwa hiyo nafanya kazi, hivyo niko hapa kama mtumishi wenu, ninyi ndio mabosi, Watendaji wanapaswa kujua kwamba ninyi wananchi ndio mmewaajiri na wanapaswa kutatua matatizo yenu, viongozi hatupaswi kuwa sehemu ya kutengeneza matatizo, viongozi tunapaswa kuwa sehemu ya suluhu ya matatizo,huo ndio uongozi bora ,na nilishasema tokeni ofisini, Mtendaji wa Kata, maafisa ugani wa kata watendaji wa Mitaa, tokeni ofisini nendeni kwa wananchi makasikilize shida zao ili muweze kuwapa maelezo na mipango ya Serikali kuhusiana na maeneo yao"amesisitiza Hapi 

 Amefafanua kuwa yapo mambo mengi ambayo Serikali imeyatilia mkazo hasa swala la matibabu ya bure kwa wazee na utekelezaji wake unaendelea vizuri. 

 "Nimewaagiza watendaji wangu, wafuateni wazee kwenye Kata na Mitaa yao, ili muweze kuwatambua, na kuwapatia kadi za msamaha wa matibabu, Serikali yetu imekwishasema wazee pamoja na watoto chini ya umri wa miaka mitano matibabu kwao ni bure, na hilo sina wasiwasi nalo kwa kuwa najua linatekelezeka "amesema Hapi 

 Amefafanua kuwa wazee ni hazina pekee tuliyonayo na hasa ikizingatiwa wameitumikia nchi yetu kwa kipindi chote hicho, hivyo yawapasa kutibiwa bure na hata wakati mwingine wasipange foleni. 

 Katika hatua nyingine amewataka wanachi kushirikisha Serikali pale inapotokea kuwepo na michango isiyoeleweka, isiyofuata utaratibu, wala kanuni za fedha ili matapeli hawa waweze kukomeshwa. 

 "Kuchangia maendeleo ni jambo zuri sana, na sisi tunahamasisha wananchi kuchangia maendeleo, lakini michango inautaratibu wake, nawaomba Sana pale mnapotaka kuchangia Jambo lenye nia ya maendeleo, washirikisheni viongozi wenu wa Serikali ili tujue na turizike, na wakati mwingine tujiridhishe kwamba lile mnalotaka kulichangia haliko kwenye mpango wa Serikali wa karibuni katika kulitekeleza "Amebainisha Hapi 

 Imetolewa na
 Kitengo cha Uhusiano
 Manispaa ya Kinondoni

Matangazo

  • UTOAJI WA MIKOPO KWA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU April 01, 2025
  • TANGAZO March 22, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI October 05, 2024
  • MATOKEO YA USAILI WA VITENDO KADA YA AFISA TEHAMA MSAIDIZI ULIOFANYIKA TAREHE 25/03/2024 March 25, 2024
  • Tazama zote

Habari mpya

  • ZAIDI YA MITI 1200 YAPANDWA KUADHIMISHA MIAKA 63 YA UHURU

    December 09, 2024
  • MAAMBUKIZI UKIMWI YAPUNGUA

    December 01, 2024
  • MAAMBUKIZI YA VIRUSI VYA UKIMWI YASHUKA KINONDONI

    November 29, 2024
  • WENYEVITI NA WAJUMBE WAPYA WAPEWA MAELEKEZO YA MAJUKUMU YAO

    November 28, 2024
  • Tazama zote

Picha Jongefu

IFAHAMU KATA YA MZIMUNI, MANISPAA YA KINONDONI
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • MWONGOZO WA NAMNA YA KUTUMIA MFUMO WA TAUSI
  • UJASIRIAMALI NA UTOAJI MIKOPO
  • MAKTABA YA PICHA
  • TAARIFA KWA UMMA
  • HOTUBA
  • ORODHA YA WAHESHIMIWA MADIWANI
  • MKATABA WA HUDUMA KWA MTEJA
  • MIRADI ILIYOKAMILIKA

Viunganishi Linganifu

  • TOVUTI KUU YA IKULU
  • TOVUTI YA UTUMISHI
  • TOVUTI YA OR-TAMISEMI
  • TOVUTI YA OFISI YA TAKWIMU YA TAIFA
  • TOVUTI YA IDARA YA HABARI MAELEZO
  • TOVUTI KUU YA SERIKALI

Idadi ya Wasomaji

world map hits counter

Waliotembelea tovuti

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    2 Barabara ya Morogoro, 14883 Dar es Salaam

    Anuani ya Posta: S.L.P 31902

    Simu ya mezani: +255222170173

    Simu ya mkononi: +255733241052

    Barua pepe: md@kinondonimc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya tovuti

Hatimiliki © 2017 Halmashauri ya Manispaa ya Kinondoni. Haki Zote Zimehifadhiwa.