• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
Kinondoni Municipal Council
Kinondoni Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Kinondoni

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Maadili ya Msingi
    • Wasifu wa Halmashauri
  • Utawala
    • Divisheni
      • Miundombinu, Vijijini na Mijini
      • Huduma za Afya, Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Elimu ya Awali na Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Usimamizi wa Rasilimali Watu
    • Vitengo
      • Usimamizi wa Taka na Usafi wa Mazingira
      • Uhifadhi wa Maliasili na Mazingira
      • Michezo, Utamaduni na Sanaa
      • Fedha na Mahesabu
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Usimamizi wa Manunuzi
      • TEHAMA
      • Mawasiliano Serikalini
    • Kata
      • Bunju
      • Hananasif
      • Kawe
      • Kigogo
      • Kijitonyama
      • Kinondoni
      • Kunduchi
      • Mabwepande
      • Magomeni
      • Makongo
      • Makumbusho
      • Mbezi Juu
      • Mbweni
      • Mikocheni
      • Msasani
      • Mwananyamala
      • Mzimuni
      • Ndugumbi
      • Tandale
      • Wazo
    • Muundo wa Taasisi
    • Ofisi ya Mtendaji wa Kata
    • Ofisi ya Mtendaji wa Mtaa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya utalii
      • Fukwe na Visiwa
      • Sehemu za kitamaduni, ngoma za asili na sanaa za mikono
    • Utalii
      • Matukio ya Utalii
      • Royal Tour Bus
  • Huduma zetu
    • Biashara
    • Huduma za Elimu
    • Ujasiriamali
    • Ushauri katika Kilimo
    • Vituo vya Ukusanyaji Mapato
    • Vibali vya Ujenzi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Uongozi
      • Mipangomiji na Mazingira
      • Maadili
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhibiti UKIMWI
    • Ratiba ya Vikao
    • Ratiba ya Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Sera
    • Makala
    • Mpango mkakati
    • Taarifa mbalimbali
    • Mkataba wa huduma kwa mteja
    • Fomu za maombi
    • Vibali vya Ujenzi Vilivyotolewa
    • Nyaraka za Elimu

WAKAZI WA WAZO MJI MPYA WAPATIWA SULUHISHO LA BARABARA

Tarehe iliyowekwa: November 27th, 2020

Suluhisho hilo limekuja leo baada ya Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni Mhe. Daniel Chongolo kuzuru eneo lenye bwawa na kushauri kufunguliwa kwa barabara ya muda katika mazungumzo yaliyohusisha  wananchi wa mji mpya, wamiliki wa viwanja vilivyopakana na bwawa pamoja na wadau wa maendeleo .

 Akizungumza na wakazi hao, Mhe. Chongolo amesema kufunguliwa kwa barabara ya muda kutawawezesha wakazi wa wazo mji mpya kufika majumbani kwao, lakini pia kutatoa nafasi ya eneo linalojaa maji kuboreshwa kwa kusambaza kifusi na kuchimba mitaro  itakayoelekeza  maji katika mkondo wake ili kuzuia athari za uharibifu wa barabara.

Amesema " Kwanza tuondoe hatari iliyo mbele yetu,  miti ing'olewe ili kuandaa eneo la barabara ya watu kupita ili waweze kufika katika makazi yao, kupatikane kifusi cha kujaza eneo kuyaelekeza maji kufuata mkondo wake, mana suala lililoko hapa ni makubaliano tu, baina ya mwenye kiwanja kilichopakana na bwawa kutoa eneo kwa muda ili waweze kusambaza kifusi kwa ajili ya kupata barabara ya muda, wakati tukiendelea kupata suluhisho la kudumu. jukumu langu ni kuhakikisha wananchi wanapata Amani katika makazi yao" Amesema Chongolo.

Aidha amemtaka Bw.Gerald Lusula Mwenye kiwanja Na.392 na Bwana Andrew Peter Mwenye kiwanja namba 393 vyote vikiwa vimepakana na eneo lenye bwawa kutoa ushirikiano katika kuhakikisha suluhu ya pamoja inapatikana kwa kuruhusu kusambazwa kifusi kwenye ukingo wa viwanja ili kupatikana kwa barabara ya muda kwa wakazi wa mji mpya kufika majumbani kwao huku wakiangalia suluhu ya kudumu ya eneo hilo.

Katika hatua nyingine ameiagiza  kampuni ya Mecco inayojenga barabara ya wazo kutumia scaveta pamoja na greda kusambaza kifusi kitakachotolewa na kiwanda cha wazo ikiwa ni pamoja na mifuko 20 ya cement pamoja na kalvati kwa ajili ya kuboreshwa eneo hilo la bwawa.

Awali akiainisha changamoto ya eneo hilo Mhandisi wa Tanroad Bi.Mariam Hassan amesema ni kutokana na kuzuiwa kwa mkondo huo wa maji hali iliyopelekea kutuama na kusababisha bwawa linaloendelea kukua na kuharibu barabara.


Imeandaliwa na

Kitengo Cha Uhusiano na Habari

Manispaa ya Kinondoni.

Matangazo

  • UTOAJI WA MIKOPO KWA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU April 01, 2025
  • TANGAZO March 22, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI October 05, 2024
  • MATOKEO YA USAILI WA VITENDO KADA YA AFISA TEHAMA MSAIDIZI ULIOFANYIKA TAREHE 25/03/2024 March 25, 2024
  • Tazama zote

Habari mpya

  • ZAIDI YA MITI 1200 YAPANDWA KUADHIMISHA MIAKA 63 YA UHURU

    December 09, 2024
  • MAAMBUKIZI UKIMWI YAPUNGUA

    December 01, 2024
  • MAAMBUKIZI YA VIRUSI VYA UKIMWI YASHUKA KINONDONI

    November 29, 2024
  • WENYEVITI NA WAJUMBE WAPYA WAPEWA MAELEKEZO YA MAJUKUMU YAO

    November 28, 2024
  • Tazama zote

Picha Jongefu

IFAHAMU KATA YA MZIMUNI, MANISPAA YA KINONDONI
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • MWONGOZO WA NAMNA YA KUTUMIA MFUMO WA TAUSI
  • UJASIRIAMALI NA UTOAJI MIKOPO
  • MAKTABA YA PICHA
  • TAARIFA KWA UMMA
  • HOTUBA
  • ORODHA YA WAHESHIMIWA MADIWANI
  • MKATABA WA HUDUMA KWA MTEJA
  • MIRADI ILIYOKAMILIKA

Viunganishi Linganifu

  • TOVUTI KUU YA IKULU
  • TOVUTI YA UTUMISHI
  • TOVUTI YA OR-TAMISEMI
  • TOVUTI YA OFISI YA TAKWIMU YA TAIFA
  • TOVUTI YA IDARA YA HABARI MAELEZO
  • TOVUTI KUU YA SERIKALI

Idadi ya Wasomaji

world map hits counter

Waliotembelea tovuti

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    2 Barabara ya Morogoro, 14883 Dar es Salaam

    Anuani ya Posta: S.L.P 31902

    Simu ya mezani: +255222170173

    Simu ya mkononi: +255733241052

    Barua pepe: md@kinondonimc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya tovuti

Hatimiliki © 2017 Halmashauri ya Manispaa ya Kinondoni. Haki Zote Zimehifadhiwa.