• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
Kinondoni Municipal Council
Kinondoni Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Kinondoni

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Maadili ya Msingi
    • Wasifu wa Halmashauri
  • Utawala
    • Divisheni
      • Miundombinu, Vijijini na Mijini
      • Huduma za Afya, Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Elimu ya Awali na Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Usimamizi wa Rasilimali Watu
    • Vitengo
      • Usimamizi wa Taka na Usafi wa Mazingira
      • Uhifadhi wa Maliasili na Mazingira
      • Michezo, Utamaduni na Sanaa
      • Fedha na Mahesabu
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Usimamizi wa Manunuzi
      • TEHAMA
      • Mawasiliano Serikalini
    • Ofisi ya Mtendaji wa Kata
    • Ofisi ya Mtendaji wa Mtaa
    • Kata
      • Bunju
      • Hananasif
      • Kawe
      • Kigogo
      • Kijitonyama
      • Kinondoni
      • Kunduchi
      • Mabwepande
      • Magomeni
      • Makongo
      • Makumbusho
      • Mbezi Juu
      • Mbweni
      • Mikocheni
      • Msasani
      • Mwananyamala
      • Mzimuni
      • Ndugumbi
      • Tandale
      • Wazo
    • Muundo wa Taasisi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Fukwe na Visiwa
    • Sehemu za kitamaduni, ngoma za asili na sanaa za mikono
    • Matukio ya Utalii
  • Huduma zetu
    • Biashara
    • Huduma za Elimu
    • Ujasiriamali
    • Ushauri katika Kilimo
    • Vituo vya Ukusanyaji Mapato
    • Vibali vya Ujenzi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Uongozi
      • Mipangomiji na Mazingira
      • Maadili
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhibiti UKIMWI
    • Ratiba ya Vikao
    • Ratiba ya Meya
  • Miradi
    • Iliyopangwa
    • Inayoendelea
    • Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Sera
    • Makala
    • Mpango mkakati
    • Taarifa mbalimbali
    • Mkataba wa huduma
    • Fomu za maombi
    • Vibali vya Ujenzi
    • Nyaraka za Elimu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video
    • Habari
    • Matukio

VIKUNDI VYAASWA MATUMIZI SAHIHI YA MIKOPO

Tarehe iliyowekwa: February 18th, 2023

VIKUNDI 115 vya wanawake, vijana na watu wenye ulemavu vimeaswa kutumia vizuri mikopo ya asilimia kumi inayotolewa na Manispaa ya Kinondoni kwa ajili ya kukuza uchumi, kuongeza kipato na kutengeneza ajira.

Kauli hiyo imetolewa Februari 18, 2023 na Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni, Mhe. Saad Mtambule, wakati wa hafla ya utoaji wa mikopo yenye jumla ya shilingi za Kitanzania 2,555,333,332.

Vikundi vilivyonufaika na mikopo hiyo ni vikundi 11 vya watu wenye ulemavu waliopata shilingi za Kitanzania 297,754,580; Wananwake vikundi 73 vilivyopata shilingi za Kitanzania 1,239,150,000 na Vijana vikundi 31 ambao wamepata shilingi za Kitanzania 1,018,428,742.

Mheshimiwa Mtambule alisema, "Manispaa imetekeleza jukumu lake la kisheria la kutoa mikopo isiyo na riba kwenu, hivyo ni jukumu lenu kuwajibika kutumia mikopo hii vizuri ili mpate faida, mkuze uchumi na kutengeneza ajira. Simamieni vizuri biashara zenu ili mrejeshe mikopo yenu na msimkatishe tamaa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan, Chama cha Mapinduzi na Manispaa yenu".

Aidha, aliwataka wanufaika hao kutoielekeza mikopo hiyo kwenye shughuli zisizo kusudiwa. Pia aliwataka wanufaika kufanya biashara katika mazingira salama na safi.

Katika hatua nyingine Mheshimiwa Mtambule ameipongeza Manispaa ya Kinondoni kwa kutoa mikopo inayotokana na asilimia kumi kwa utimilifu. "Kuna Halmashauri nyingi nchini hazifikii malengo ya utoaji mikopo hii kwa utimilifu, lakini Manispaa yetu imekuwa inaongoza kwa kutoa mikopo. Nawapongeza sana".

Akitoa taarifa ya utoaji mikopo hiyo tangu mwaka 2017/2018, Mkurugenzi wa Manispaa ya Kinondoni, Bi. Hanifa Suleiman Hamza, alimweleza Mkuu wa Wilaya kuwa mikopo hiyo ni ya kipindi cha robo ya kwanza na ya pili ya mwaka wa fedha 2022/2023 kwamba, "Halmashauri itaendelea kuiwezesha jamii kushiriki kikamilifu katika shughuli kujiletea maendeleo ili kufikia azma ya jamii kujikwamua kiuchumi na kupiga vita umasikini."

Alieleza kuwa Halmashauri inaendelea na jitihada za kuhamasisha jamii kuunda vikundi na kuvisajili ili kuweza kupata mikopo isiyo na riba kupitia fedha zinazotengwa kwa ajili ya mikopo ya asilimia kumi ya mapato ya ndani pamoja na pesa inayotokana na marejesho.


Imeandaliwa na Kitengo cha Mawasiliano Serikalini:

Manispaa ya Kinondoni.

Matangazo

  • KUFUTA TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI March 14, 2023
  • TANGAZO LA AJIRA YA MKATABA March 13, 2023
  • TANGAZO KWA WASIOLIPIA VIWANJA BOKO DOVYA (KWA SOMJI) NA SALASALA February 15, 2023
  • MABADILIKO YA SIKU YA MAFUNZO YA WASIMAMIZI WA MAUDHUI, WASIMAMIZI WA TEHAMA NA MAKARANI WA SENSA YA WATU NA MAKAZI 2022 July 28, 2022
  • Tazama zote

Habari mpya

  • JAPAN YAIPATIA MSAADA MZIMUNI SEKONDARI

    March 15, 2023
  • VIKUNDI VYAASWA MATUMIZI SAHIHI YA MIKOPO

    February 18, 2023
  • "HAKUNA TIMU KUBWA ZAIDI YA KMC FC"

    February 18, 2023
  • ULINZI NI KIPAUMBELE KINODONI-DC SAAD

    February 12, 2023
  • Tazama zote

Picha Jongefu

VIKUNDI VILIVYOSEPA NA BILIONI 11 VYAKALIWA KOONI MANISPAA YA KINONDONI. REJESHENI...
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • TARATIBU ZA KUPATA KIBALI CHA UJENZI
  • MKATABA WA HUDUMA KWA MTEJA
  • UJASIRIAMALI NA UTOAJI MIKOPO
  • VITUO VYA KUKUSANYIA MAPATO
  • ORODHA YA WAHESHIMIWA MADIWANI
  • RATIBA YA MSTAHIKI MEYA
  • TAARIFA KWA UMMA
  • MIRADI ILIYOKAMILIKA

Viunganishi Linganifu

  • TOVUTI KUU YA IKULU
  • TOVUTI YA UTUMISHI
  • TOVUTI YA OR-TAMISEMI
  • TOVUTI YA OFISI YA TAKWIMU YA TAIFA
  • TOVUTI YA IDARA YA HABARI MAELEZO
  • TOVUTI KUU YA SERIKALI

Idadi ya Wasomaji

world map hits counter

Waliotembelea tovuti

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    2 Barabara ya Morogoro, 14883 Dar es Salaam

    Anuani ya Posta: S.L.P 31902

    Simu ya mezani: +255 22 2170173

    Simu ya mkononi:

    Barua pepe: md@kinondonimc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya tovuti

Hatimiliki © 2017 Halmashauri ya Manispaa ya Kinondoni. Haki Zote Zimehifadhiwa.