• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
Kinondoni Municipal Council
Kinondoni Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Kinondoni

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Maadili ya Msingi
    • Wasifu wa Halmashauri
  • Utawala
    • Divisheni
      • Miundombinu, Vijijini na Mijini
      • Huduma za Afya, Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Elimu ya Awali na Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Usimamizi wa Rasilimali Watu
    • Vitengo
      • Usimamizi wa Taka na Usafi wa Mazingira
      • Uhifadhi wa Maliasili na Mazingira
      • Michezo, Utamaduni na Sanaa
      • Fedha na Mahesabu
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Usimamizi wa Manunuzi
      • TEHAMA
      • Mawasiliano Serikalini
    • Kata
      • Bunju
      • Hananasif
      • Kawe
      • Kigogo
      • Kijitonyama
      • Kinondoni
      • Kunduchi
      • Mabwepande
      • Magomeni
      • Makongo
      • Makumbusho
      • Mbezi Juu
      • Mbweni
      • Mikocheni
      • Msasani
      • Mwananyamala
      • Mzimuni
      • Ndugumbi
      • Tandale
      • Wazo
    • Muundo wa Taasisi
    • Ofisi ya Mtendaji wa Kata
    • Ofisi ya Mtendaji wa Mtaa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya utalii
      • Fukwe na Visiwa
      • Sehemu za kitamaduni, ngoma za asili na sanaa za mikono
    • Utalii
      • Matukio ya Utalii
      • Royal Tour Bus
  • Huduma zetu
    • Biashara
    • Huduma za Elimu
    • Ujasiriamali
    • Ushauri katika Kilimo
    • Vituo vya Ukusanyaji Mapato
    • Vibali vya Ujenzi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Uongozi
      • Mipangomiji na Mazingira
      • Maadili
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhibiti UKIMWI
    • Ratiba ya Vikao
    • Ratiba ya Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Sera
    • Makala
    • Mpango mkakati
    • Taarifa mbalimbali
    • Mkataba wa huduma kwa mteja
    • Fomu za maombi
    • Vibali vya Ujenzi Vilivyotolewa
    • Nyaraka za Elimu

VIJANA KOTE NCHINI WAMETAKIWA KUJENGA UTAMADUNI WA KUJISHUGHULISHA NA SHUGHULI ZA KUJIKWAMUA KIUCHUMI

Tarehe iliyowekwa: October 6th, 2017

 Vijana kote nchini wametakiwa kuhakikisha wanajenga Utamaduni wa kujishughulisha na shughuli za kujikwamua kiuchumi ikiwa ni pamoja na kujiunga kwenye vikundi endelevu vya vicoba ili waweze kupata elimu ya ujasiriamali kwa lengo la kukabiliana na changamoto za ajira. 

 Agizo hilo limetolewa leo na Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni Mh Ali Hapi alipokuwa mgeni rasmi katika uzinduzi wa taasisi ya BUTA Vicoba endelevu iliyofanyika katika Kata ya Bunju Manispaa ya Kinondoni.

 Amesema vijana wengi wamekosa Utamaduni wa kujishughulisha na shughuli za ujasiriamali kitu ambacho hakimjengi katika kujikwamua kiuchumi, kimaendeleo na kifikra kuelekea uchumi wa viwanda. 

 "Wasichana hawana Utamaduni wa kuweka akiba, wengi wadada zetu wanawekeza kwenye urembo, wakishafika umri wa kuwa wamama ndio wanaanza kuchangamkia fursa za uchumi Kama hizi, kwa hiyo kinamama popote mlipo wahamasisheni mabinti zenu na kinababa wahamasisheni mabinti zenu wakiwa bado wanaumri mdogo wawe na Utamaduni wa kuweka akiba, wawe na Utamaduni wa kushiriki kwenye shughuli za ujasiriamali" amesema Hapi 

 Amesema Serikali inahitaji sekta binafsi pamoja na wajasiriamali ili kwa pamoja tuweze kuwafikia watu wengi zaidi ili waweze kujikwamua na tatizo la ajira.

 "Ndugu zangu ninyi mnafahamu ya kwamba Serikali inayomajukumu makubwa ya kufanya katika kujenga uchumi wa wananchi wetu, lakini Serikali peke yake haiwezi kufanya jukumu hilo, tunawahitaji sekta binafsi tunahitaji wajasiriamali, tukishirikiana kwa pamoja unauwezo wa kuwasaidia na kuwafikia wananchi wengi zaidi, tunafahamu tunalo tatizo la ajira, tunao vijana, tunao kinamama ambao hawana ajira, lakini nataka kuwakikishia kwamba hakuna serikali duniani ambayo inauwezo wa kumaliza tatizo la ajira kwa asilimia miamoja haipo " amefahamisha Hapi 

 Aidha amefurahishwa na wanachama hawa wa vicoba endelevu kushirikiana na taasisi za kifedha kama mabenki na mashirika mbalimbali, kadhalika kuwa na utaratibu wa kujiunga kwenye mifuko ya hifadhi ya kijamii inayowawezesha wanachama kupata matibabu,mikopo na mafao ya uzeeni.

 Naye Rais wa vicoba endelevu Tanzania Bi Devota likokola ameishukuru Serikali ya Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kuruhusu siku ya kuondoa umaskini duniani kuwa siku ya Vicoba. 

 Amesema kwa mujibu wa taarifa ya baraza la vicoba Tanzania mpaka sasa vimefikia zaidi ya vicoba endelevu laki moja, vyenye wanachama zaidi ya milioni mbili na laki mbili na vyenye mzunguko wa fedha uliofikia kiasi cha trilioni moja na milioni miambili .

 Katika hatua nyingine Mh Hapi amewataka wanachama hao wa vicoba endelevu kupanua wigo mkubwa ili waweze kuwafikia wajasiriamali, waalimu, wafanyakazi wa Serikali, wafanyabiashara wa kwenye masoko, ili kwa pamoja tuweze kusaidiana kulikwamua gurudumu la maendeleo.

 Imetolewa na
 Kitengo cha Uhusiano
 Manispaa ya Kinondoni.

Matangazo

  • UTOAJI WA MIKOPO KWA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU April 01, 2025
  • TANGAZO March 22, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI October 05, 2024
  • MATOKEO YA USAILI WA VITENDO KADA YA AFISA TEHAMA MSAIDIZI ULIOFANYIKA TAREHE 25/03/2024 March 25, 2024
  • Tazama zote

Habari mpya

  • ZAIDI YA MITI 1200 YAPANDWA KUADHIMISHA MIAKA 63 YA UHURU

    December 09, 2024
  • MAAMBUKIZI UKIMWI YAPUNGUA

    December 01, 2024
  • MAAMBUKIZI YA VIRUSI VYA UKIMWI YASHUKA KINONDONI

    November 29, 2024
  • WENYEVITI NA WAJUMBE WAPYA WAPEWA MAELEKEZO YA MAJUKUMU YAO

    November 28, 2024
  • Tazama zote

Picha Jongefu

IFAHAMU KATA YA MZIMUNI, MANISPAA YA KINONDONI
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • MWONGOZO WA NAMNA YA KUTUMIA MFUMO WA TAUSI
  • UJASIRIAMALI NA UTOAJI MIKOPO
  • MAKTABA YA PICHA
  • TAARIFA KWA UMMA
  • HOTUBA
  • ORODHA YA WAHESHIMIWA MADIWANI
  • MKATABA WA HUDUMA KWA MTEJA
  • MIRADI ILIYOKAMILIKA

Viunganishi Linganifu

  • TOVUTI KUU YA IKULU
  • TOVUTI YA UTUMISHI
  • TOVUTI YA OR-TAMISEMI
  • TOVUTI YA OFISI YA TAKWIMU YA TAIFA
  • TOVUTI YA IDARA YA HABARI MAELEZO
  • TOVUTI KUU YA SERIKALI

Idadi ya Wasomaji

world map hits counter

Waliotembelea tovuti

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    2 Barabara ya Morogoro, 14883 Dar es Salaam

    Anuani ya Posta: S.L.P 31902

    Simu ya mezani: +255222170173

    Simu ya mkononi: +255733241052

    Barua pepe: md@kinondonimc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya tovuti

Hatimiliki © 2017 Halmashauri ya Manispaa ya Kinondoni. Haki Zote Zimehifadhiwa.