• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
Kinondoni Municipal Council
Kinondoni Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Kinondoni

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Maadili ya Msingi
    • Wasifu wa Halmashauri
  • Utawala
    • Divisheni
      • Miundombinu, Vijijini na Mijini
      • Huduma za Afya, Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Elimu ya Awali na Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Usimamizi wa Rasilimali Watu
    • Vitengo
      • Usimamizi wa Taka na Usafi wa Mazingira
      • Uhifadhi wa Maliasili na Mazingira
      • Michezo, Utamaduni na Sanaa
      • Fedha na Mahesabu
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Usimamizi wa Manunuzi
      • TEHAMA
      • Mawasiliano Serikalini
    • Kata
      • Bunju
      • Hananasif
      • Kawe
      • Kigogo
      • Kijitonyama
      • Kinondoni
      • Kunduchi
      • Mabwepande
      • Magomeni
      • Makongo
      • Makumbusho
      • Mbezi Juu
      • Mbweni
      • Mikocheni
      • Msasani
      • Mwananyamala
      • Mzimuni
      • Ndugumbi
      • Tandale
      • Wazo
    • Muundo wa Taasisi
    • Ofisi ya Mtendaji wa Kata
    • Ofisi ya Mtendaji wa Mtaa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya utalii
      • Fukwe na Visiwa
      • Sehemu za kitamaduni, ngoma za asili na sanaa za mikono
    • Utalii
      • Matukio ya Utalii
      • Royal Tour Bus
  • Huduma zetu
    • Biashara
    • Huduma za Elimu
    • Ujasiriamali
    • Ushauri katika Kilimo
    • Vituo vya Ukusanyaji Mapato
    • Vibali vya Ujenzi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Uongozi
      • Mipangomiji na Mazingira
      • Maadili
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhibiti UKIMWI
    • Ratiba ya Vikao
    • Ratiba ya Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Sera
    • Makala
    • Mpango mkakati
    • Taarifa mbalimbali
    • Mkataba wa huduma kwa mteja
    • Fomu za maombi
    • Vibali vya Ujenzi Vilivyotolewa
    • Nyaraka za Elimu

TAMISEMI YARIDHISHWA NA MATUMIZI MAZURI YA FEDHA ZA MAPATO YA NDANI KATIKA MIRADI YA MAENDELEO KINONDONI

Tarehe iliyowekwa: June 25th, 2020

Hayo yamebainishwa na Naibu waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) Mhe. Josephat Kandege alipozuru Kinondoni kwa lengo la ukaguzi wa miradi ya maendeleo, kujiridhisha na hatua za utekelezaji wake unaoenda sambamba na thamani ya fedha na ukamilishaji wa viwango kwa wakati.

Amesema kuwa Manispaa hiyo ni mfano wakuigwa kwa kuwa imeonesha nidhamu nzuri katika matumizi ya fedha zinazotokana na vyanzo vya mapato ya ndani na kwamba miradi ambayo imetekelezwa kupitia fedha hizo inaendana na thamani halisia.

 “Kimsingi leo nimemaliza ziara yangu katika Halmashauri hii, na kikubwa nilikuwa nimelenga zaidi kuona fedha zinazokusanywa  na Halmashauri  na namna ambavyo zinatumika katika miradi ambayo inaonekana na kimsingi naomba niwapongeze sana Kinondoni,  mnazitendea haki fedha zenu mnazokusanya” amesema Mhe. Kandege.

Kadhalika Mhe. Kandege ameridhishwa na kiwango cha barabara zinazojengwa katika Halmashauri hiyo kupitia mradi wa DMDP na kusema kuwa kukamilika kwake kutaleta mafanikio makubwa kwa wananchi hususani watumiaji wa barabara ya Shekilango na kwamba itaondoa msongamano wa daladala na kuwawezesha wananchi kuondokana na adha ya foleni.

Amefafanua kuwa Mafanikio haya yanayoonekana leo Kinondoni ni kutokana na uongozi imara wa Serikali ya awamu ya tano ya Rais Dk. John Pombe Joseph Magufuli pamoja na usimamizi mzuri wa Mkurugenzi ndg. Aron Kagurumjuli ulioleta tija kwa Wananchi.

Katika hatua nyingine Mhe.Kandege ameipongeza Manispaa ya Kinondoni kwa kujenga kituo cha Afya katika Kata ya Kigogo na kusema kuwa walifanya mamuzi ya busara na yakujali wananchi kwakuwa eneo hilo halikuwa na Hospitali na kwamba litawasaidia wakazi hao kupata huduma bora ya afya.

 “Kinondoni mliona mbali kuweka kituo cha Afya pale Kigogo, mlitumia busara ya hali ya juu mkaona ni bora mnunue eneo kwa ajili ya kuwajengea wananchi kituo cha Afya, hivyo hata kwenye Kata ya Kawe kwa ujumla ukiondoa Kawe kama Kawe eneo lililobaki halikuwa na kituo cha Afya, pamoja na ujenzi wa Hopsitali ya Wilaya nilazima uwe navituo hivi ili hata mgonjwa wa eneo jirani apate huduma.

Katika ziara hiyo Mhe. Kandege ametembelea Barabara ya shekilango inayojengwa kwa kiwango cha lami kwa shilingi Bilioni 14. 8, mfereji wa Kilongawima uliyopo Jimbo la Kawe kwa shilingi Bilioni 3.1 pamoja na upanuzi wa Zahanati ya Bunju mradi unajongekwa cha shilingi Milioni 600.


Imeandaliwa na

Kitengo cha Habari na Mahusiano

Halmashauri ya Manispaa ya Kinondoni.



Matangazo

  • UTOAJI WA MIKOPO KWA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU April 01, 2025
  • TANGAZO March 22, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI October 05, 2024
  • MATOKEO YA USAILI WA VITENDO KADA YA AFISA TEHAMA MSAIDIZI ULIOFANYIKA TAREHE 25/03/2024 March 25, 2024
  • Tazama zote

Habari mpya

  • ZAIDI YA MITI 1200 YAPANDWA KUADHIMISHA MIAKA 63 YA UHURU

    December 09, 2024
  • MAAMBUKIZI UKIMWI YAPUNGUA

    December 01, 2024
  • MAAMBUKIZI YA VIRUSI VYA UKIMWI YASHUKA KINONDONI

    November 29, 2024
  • WENYEVITI NA WAJUMBE WAPYA WAPEWA MAELEKEZO YA MAJUKUMU YAO

    November 28, 2024
  • Tazama zote

Picha Jongefu

IFAHAMU KATA YA MZIMUNI, MANISPAA YA KINONDONI
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • MWONGOZO WA NAMNA YA KUTUMIA MFUMO WA TAUSI
  • UJASIRIAMALI NA UTOAJI MIKOPO
  • MAKTABA YA PICHA
  • TAARIFA KWA UMMA
  • HOTUBA
  • ORODHA YA WAHESHIMIWA MADIWANI
  • MKATABA WA HUDUMA KWA MTEJA
  • MIRADI ILIYOKAMILIKA

Viunganishi Linganifu

  • TOVUTI KUU YA IKULU
  • TOVUTI YA UTUMISHI
  • TOVUTI YA OR-TAMISEMI
  • TOVUTI YA OFISI YA TAKWIMU YA TAIFA
  • TOVUTI YA IDARA YA HABARI MAELEZO
  • TOVUTI KUU YA SERIKALI

Idadi ya Wasomaji

world map hits counter

Waliotembelea tovuti

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    2 Barabara ya Morogoro, 14883 Dar es Salaam

    Anuani ya Posta: S.L.P 31902

    Simu ya mezani: +255222170173

    Simu ya mkononi: +255733241052

    Barua pepe: md@kinondonimc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya tovuti

Hatimiliki © 2017 Halmashauri ya Manispaa ya Kinondoni. Haki Zote Zimehifadhiwa.