• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
Kinondoni Municipal Council
Kinondoni Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Kinondoni

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Maadili ya Msingi
    • Wasifu wa Halmashauri
  • Utawala
    • Divisheni
      • Miundombinu, Vijijini na Mijini
      • Huduma za Afya, Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Elimu ya Awali na Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Usimamizi wa Rasilimali Watu
    • Vitengo
      • Usimamizi wa Taka na Usafi wa Mazingira
      • Uhifadhi wa Maliasili na Mazingira
      • Michezo, Utamaduni na Sanaa
      • Fedha na Mahesabu
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Usimamizi wa Manunuzi
      • TEHAMA
      • Mawasiliano Serikalini
    • Ofisi ya Mtendaji wa Kata
    • Ofisi ya Mtendaji wa Mtaa
    • Kata
      • Bunju
      • Hananasif
      • Kawe
      • Kigogo
      • Kijitonyama
      • Kinondoni
      • Kunduchi
      • Mabwepande
      • Magomeni
      • Makongo
      • Makumbusho
      • Mbezi Juu
      • Mbweni
      • Mikocheni
      • Msasani
      • Mwananyamala
      • Mzimuni
      • Ndugumbi
      • Tandale
      • Wazo
    • Muundo wa Taasisi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Fukwe na Visiwa
    • Sehemu za kitamaduni, ngoma za asili na sanaa za mikono
    • Matukio ya Utalii
  • Huduma zetu
    • Biashara
    • Huduma za Elimu
    • Ujasiriamali
    • Ushauri katika Kilimo
    • Vituo vya Ukusanyaji Mapato
    • Vibali vya Ujenzi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Uongozi
      • Mipangomiji na Mazingira
      • Maadili
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhibiti UKIMWI
    • Ratiba ya Vikao
    • Ratiba ya Meya
  • Miradi
    • Iliyopangwa
    • Inayoendelea
    • Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Sera
    • Makala
    • Mpango mkakati
    • Taarifa mbalimbali
    • Mkataba wa huduma
    • Fomu za maombi
    • Vibali vya Ujenzi
    • Nyaraka za Elimu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video
    • Habari
    • Matukio

NI KINONDONI TENA UFAULU WA MATOKEO YA DARASA LA SABA 2020 MKOA WA DAR ES SALAAM

Tarehe iliyowekwa: December 24th, 2020

Manispaa ya Kinondoni imeshika nafasi ya kwanza kimkoa na ya pili Kitaifa kwa ufaulu wa asilimia 98.1 matokeo ya darasa la Saba kwa mwaka 2020.

Hayo yamebainishwa na Mstahiki Meya Manispaa ya Kinondoni Mhe Songoro Mnyonge alipokuwa akiongea na waandishi wa Habari kwa lengo la kuelezea mikakati ya Halmashauri katika kuhakikisha wanafunzi wote waliofaulu wanaingia kidato cha kwanza kwa mwaka 2021.

Mhe.Songoro mesema "Kinondoni imeendelea kuongoza katika matokeo yaliyotangazwa, ambapo 13,401 walifanya mtihani wa darasa la Saba mwaka huu na 13,159 wamefaulu na kupelekea ufaulu huo kufikia asilimia 98.1 na kwa ufaulu huo, umeufanya Manispaa ya Kinondoni kuwa ni nafasi ya kwanza Kimkoa na kuwa ya pili Kitaifa, haya ni mafanikio makubwa" Amesema Mstahiki Meya.

Ameongeza kuwa kwa wanafunzi 775 wanaosubiri chaguo la pili, Manispaa ya Kinondoni tayari Imekwishajipanga kuhakikisha inakabiliana  na changamoto hizo za uhaba  wa madarasa zinazopelekea wanafunzi hao kusubiri kwa kujenga vyumba 64 vitakavyoweza kupunguza adha hiyo kwa kiasi kikubwa mara vitakapokamilika.

Ameainisha mchanganuo wa ujenzi pamoja na ukarabati  wa vyumba hivyo vya madarasa kuwa ni ujenzi wa vyumba vya madarasa 10 sekondari ya kijitonyama, ukaratabati wa vyumba 7 shule ya Sekondari Magomeni, ujenzi wa madarasa 6 shule ya sekondari ya Benaco na ujenzi was  madarasa 6  sekondari ya mzimuni.

Mchanganuo mwingine ni ujenzi madarasa 6 shule ya Sekondari Mbezi juu, ujenzi wa madarasa 8 shule  ya Bunju tarimo, ujenzi wa madarasa 8 Boko mtambani, ujenzi wa madarasa 5 shule ya sekondari kondo, ujenzi wa madarasa 6 shule ya sekondari Oysterbay pamoja na  ujenzi wa shule mpya ya miti mirefu.

Aidha amefafanua kuwa ujenzi wa vyumba vya madarasa unaenda sambamba na ujenzi wa hostel itakayoweza kuchukua wanafunzi 320, pamoja na madawati 6000 ambapo kiasi cha tsh milioni180 na laki 5 zimetengwa kwa ajili ya utengenezaji wa madawati hayo ambapo madawati 3210 yamekamilika.

Mhe songoro ameeleza kuwa matarajio ya Manispaa ni kuhakikisha ifikapo mwezi wa pili 2021,  ujenzi pamoja na ukarabati wa vyumba vya madarasa 64, yawe yameshakamilika tayari kupokea wanafunzi.

Jumla ya wanafunzi 13401 walifanya mtihani wa darasa la Saba mwaka huu ambapo wanafunzi 13,159 wamefaulu na 12,384 wameshapata nafasi za kujiunga na kidato cha kwanza na kupelekea  wanafunzi 775 kusubiri chaguo la pili.


Imeandaliwana

Kitengo cha Habari na Uhusiano

Manispaa ya Kinondoni

Matangazo

  • KUFUTA TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI March 14, 2023
  • TANGAZO LA AJIRA YA MKATABA March 13, 2023
  • TANGAZO KWA WASIOLIPIA VIWANJA BOKO DOVYA (KWA SOMJI) NA SALASALA February 15, 2023
  • MABADILIKO YA SIKU YA MAFUNZO YA WASIMAMIZI WA MAUDHUI, WASIMAMIZI WA TEHAMA NA MAKARANI WA SENSA YA WATU NA MAKAZI 2022 July 28, 2022
  • Tazama zote

Habari mpya

  • JAPAN YAIPATIA MSAADA MZIMUNI SEKONDARI

    March 15, 2023
  • VIKUNDI VYAASWA MATUMIZI SAHIHI YA MIKOPO

    February 18, 2023
  • "HAKUNA TIMU KUBWA ZAIDI YA KMC FC"

    February 18, 2023
  • ULINZI NI KIPAUMBELE KINODONI-DC SAAD

    February 12, 2023
  • Tazama zote

Picha Jongefu

VIKUNDI VILIVYOSEPA NA BILIONI 11 VYAKALIWA KOONI MANISPAA YA KINONDONI. REJESHENI...
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • TARATIBU ZA KUPATA KIBALI CHA UJENZI
  • MKATABA WA HUDUMA KWA MTEJA
  • UJASIRIAMALI NA UTOAJI MIKOPO
  • VITUO VYA KUKUSANYIA MAPATO
  • ORODHA YA WAHESHIMIWA MADIWANI
  • RATIBA YA MSTAHIKI MEYA
  • TAARIFA KWA UMMA
  • MIRADI ILIYOKAMILIKA

Viunganishi Linganifu

  • TOVUTI KUU YA IKULU
  • TOVUTI YA UTUMISHI
  • TOVUTI YA OR-TAMISEMI
  • TOVUTI YA OFISI YA TAKWIMU YA TAIFA
  • TOVUTI YA IDARA YA HABARI MAELEZO
  • TOVUTI KUU YA SERIKALI

Idadi ya Wasomaji

world map hits counter

Waliotembelea tovuti

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    2 Barabara ya Morogoro, 14883 Dar es Salaam

    Anuani ya Posta: S.L.P 31902

    Simu ya mezani: +255 22 2170173

    Simu ya mkononi:

    Barua pepe: md@kinondonimc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya tovuti

Hatimiliki © 2017 Halmashauri ya Manispaa ya Kinondoni. Haki Zote Zimehifadhiwa.