• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
Kinondoni Municipal Council
Kinondoni Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Kinondoni

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Maadili ya Msingi
    • Wasifu wa Halmashauri
  • Utawala
    • Divisheni
      • Miundombinu, Vijijini na Mijini
      • Huduma za Afya, Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Elimu ya Awali na Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Usimamizi wa Rasilimali Watu
    • Vitengo
      • Usimamizi wa Taka na Usafi wa Mazingira
      • Uhifadhi wa Maliasili na Mazingira
      • Michezo, Utamaduni na Sanaa
      • Fedha na Mahesabu
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Usimamizi wa Manunuzi
      • TEHAMA
      • Mawasiliano Serikalini
    • Kata
      • Bunju
      • Hananasif
      • Kawe
      • Kigogo
      • Kijitonyama
      • Kinondoni
      • Kunduchi
      • Mabwepande
      • Magomeni
      • Makongo
      • Makumbusho
      • Mbezi Juu
      • Mbweni
      • Mikocheni
      • Msasani
      • Mwananyamala
      • Mzimuni
      • Ndugumbi
      • Tandale
      • Wazo
    • Muundo wa Taasisi
    • Ofisi ya Mtendaji wa Kata
    • Ofisi ya Mtendaji wa Mtaa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya utalii
      • Fukwe na Visiwa
      • Sehemu za kitamaduni, ngoma za asili na sanaa za mikono
    • Utalii
      • Matukio ya Utalii
      • Royal Tour Bus
  • Huduma zetu
    • Biashara
    • Huduma za Elimu
    • Ujasiriamali
    • Ushauri katika Kilimo
    • Vituo vya Ukusanyaji Mapato
    • Vibali vya Ujenzi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Uongozi
      • Mipangomiji na Mazingira
      • Maadili
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhibiti UKIMWI
    • Ratiba ya Vikao
    • Ratiba ya Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Sera
    • Makala
    • Mpango mkakati
    • Taarifa mbalimbali
    • Mkataba wa huduma kwa mteja
    • Fomu za maombi
    • Vibali vya Ujenzi Vilivyotolewa
    • Nyaraka za Elimu

MADIWANI WA HALMASHAURI YA MANISPAA YA MOROGORO WAFANYA ZIARA YA KUJIFUNZA NAMNA YA UKUSANYAJI MAPATO KATIKA HALMASHAURI YA KINONDONI

Tarehe iliyowekwa: November 27th, 2019

Madiwani wa Halmashauri ya Manispaa ya Morogoro  wamefanya ziara ya kujifunza namna ya ukusanyaji mapato katika Halmashauri ya Manispaa ya Kinondoni.

Madiwani hao waliokuwa wameambata na Mkuu wa Wilaya hiyo Mh. Regina Chonjo, Mstahiki Meya Amir Nondo wamepokelewa na Mkurugenzi wa Halmashauri ya Manispaa ya Kinondoni, Aron Kagurumjuli na Mstahiki Meya Benjamini Sita.

Aidha madiwani hao pia wamepokelewa na Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni Mhe. Daniel Chongolo , Katibu Tawala Stela Msofe pamoja na watumishi wengine wa Idara na vitengo ambapo pamoja na mambo mengine walipata nafasi ya kutembelea miradi mikubwa ya kimkakati ikiwemo Soko la Kisasa la Magomeni linalojengwa kwa shilingi bilioni 8.9.

Awali kabla ya kutembelea miradi hiyo , madiwani hao walipata nafasi ya kujifunza mbinu mbalimbali za ukusanyaji wa mapato zilizotolewa na Msimamizi wa Mapato wa Halmashauri ya Kinondoni Zahoro Rashidi.

Akizungumzia ziara hiyo, Mstahiki Meya wa Halmashauri ya Morogoro Mhe. Nondo alisema kuwa wamekuja kujifunza namna ya ukusanyaji wa mapato kwakuwa Halmahauri ya Kinondoni imekuwa ikifanya vizuri kwenye ukusanyaji.

“ Tumekuja kujifunza namna ya ukusanyaji mapato, ukiangalia kwenye takwimu zetu sisi tupo nyuma, sasa leo tumekuja kuona wenzetu mnafanyaje hadi mnafikia malengo, wote ni wamoja tunategemeana ,tunaomba mtupatie ujuzi mliokuwa nao” alisema Mhe. Nondo.

Kwaupande wake Mkuu wa Wilaya ya Morogoro, Mhe. Chonjo alisema aliishukuru Manispaa ya Kinondoni kwakuwapokea vizuri na kueleza kuwa wamefurahishwa na ukarimu waliopata kutoka kwa viongozi na watendaji wa Halmashauri hiyo.

“ Lengo letu na kuja hapa ni kujifunza, tunawashukuru mmetukaribisha , undugu tuliouanzisha hapa isiwe mwisho, karibuni na nyinyi Morogoro, hili tunalolifanya ndio lile linalotakiwa na Rais Dk. John Magufuli, asanteni kwa ushirikiano wenu” alisema Mhe. Chonjo.

Akiwakaribisha Madiwani hao, Mstahiki Meya . Mhe. Sita alisema kuwa Halmashauri ya Kinondoni ipo vizuri kwenye ukusanyaji wa mapato na kwamba anawakaribisha ili waweze kujinza kwa lengo la kutimiza adhma hiyo.

Naye Mhe. Chongolo ambaye ni Mkuu wa Wilaya hiyo alisema kuwa ili kufikia malengo ,viongozi hawana budi kuweka juhudi na nia ya dhati katika kutekeleza majukumu yao na kwamba kila mmoja anapaswa kushiriki kikamilifu katika kutekeleza wajibu wake.

“ Bila kuweka malengo ya dhati kabisa, tunaweza kufanya ziara za kujifunza tukamaliza maeneo yote, natusipae kitu, kikubwa ni kuweka nia, kama ilivyo kwa wenzetu wa kabila la hehe wakisema wanajinyonga basi wanajinyonga kweli, inamana waliweka nia , kwahiyo nasisi viongozi tuwaige wahehe katika kuweka nia ya kuleta maendeleo.


Imetolewa na

Kitengo cha Habari na Uhusiano

Manispaa ya Kinondoni.

Matangazo

  • UTOAJI WA MIKOPO KWA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU April 01, 2025
  • TANGAZO March 22, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI October 05, 2024
  • MATOKEO YA USAILI WA VITENDO KADA YA AFISA TEHAMA MSAIDIZI ULIOFANYIKA TAREHE 25/03/2024 March 25, 2024
  • Tazama zote

Habari mpya

  • ZAIDI YA MITI 1200 YAPANDWA KUADHIMISHA MIAKA 63 YA UHURU

    December 09, 2024
  • MAAMBUKIZI UKIMWI YAPUNGUA

    December 01, 2024
  • MAAMBUKIZI YA VIRUSI VYA UKIMWI YASHUKA KINONDONI

    November 29, 2024
  • WENYEVITI NA WAJUMBE WAPYA WAPEWA MAELEKEZO YA MAJUKUMU YAO

    November 28, 2024
  • Tazama zote

Picha Jongefu

IFAHAMU KATA YA MZIMUNI, MANISPAA YA KINONDONI
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • MWONGOZO WA NAMNA YA KUTUMIA MFUMO WA TAUSI
  • UJASIRIAMALI NA UTOAJI MIKOPO
  • MAKTABA YA PICHA
  • TAARIFA KWA UMMA
  • HOTUBA
  • ORODHA YA WAHESHIMIWA MADIWANI
  • MKATABA WA HUDUMA KWA MTEJA
  • MIRADI ILIYOKAMILIKA

Viunganishi Linganifu

  • TOVUTI KUU YA IKULU
  • TOVUTI YA UTUMISHI
  • TOVUTI YA OR-TAMISEMI
  • TOVUTI YA OFISI YA TAKWIMU YA TAIFA
  • TOVUTI YA IDARA YA HABARI MAELEZO
  • TOVUTI KUU YA SERIKALI

Idadi ya Wasomaji

world map hits counter

Waliotembelea tovuti

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    2 Barabara ya Morogoro, 14883 Dar es Salaam

    Anuani ya Posta: S.L.P 31902

    Simu ya mezani: +255222170173

    Simu ya mkononi: +255733241052

    Barua pepe: md@kinondonimc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya tovuti

Hatimiliki © 2017 Halmashauri ya Manispaa ya Kinondoni. Haki Zote Zimehifadhiwa.