• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
Kinondoni Municipal Council
Kinondoni Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Kinondoni

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Maadili ya Msingi
    • Wasifu wa Halmashauri
  • Utawala
    • Divisheni
      • Miundombinu, Vijijini na Mijini
      • Huduma za Afya, Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Elimu ya Awali na Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Usimamizi wa Rasilimali Watu
    • Vitengo
      • Usimamizi wa Taka na Usafi wa Mazingira
      • Uhifadhi wa Maliasili na Mazingira
      • Michezo, Utamaduni na Sanaa
      • Fedha na Mahesabu
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Usimamizi wa Manunuzi
      • TEHAMA
      • Mawasiliano Serikalini
    • Kata
      • Bunju
      • Hananasif
      • Kawe
      • Kigogo
      • Kijitonyama
      • Kinondoni
      • Kunduchi
      • Mabwepande
      • Magomeni
      • Makongo
      • Makumbusho
      • Mbezi Juu
      • Mbweni
      • Mikocheni
      • Msasani
      • Mwananyamala
      • Mzimuni
      • Ndugumbi
      • Tandale
      • Wazo
    • Muundo wa Taasisi
    • Ofisi ya Mtendaji wa Kata
    • Ofisi ya Mtendaji wa Mtaa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya utalii
      • Fukwe na Visiwa
      • Sehemu za kitamaduni, ngoma za asili na sanaa za mikono
    • Utalii
      • Matukio ya Utalii
      • Royal Tour Bus
  • Huduma zetu
    • Biashara
    • Huduma za Elimu
    • Ujasiriamali
    • Ushauri katika Kilimo
    • Vituo vya Ukusanyaji Mapato
    • Vibali vya Ujenzi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Uongozi
      • Mipangomiji na Mazingira
      • Maadili
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhibiti UKIMWI
    • Ratiba ya Vikao
    • Ratiba ya Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Sera
    • Makala
    • Mpango mkakati
    • Taarifa mbalimbali
    • Mkataba wa huduma kwa mteja
    • Fomu za maombi
    • Vibali vya Ujenzi Vilivyotolewa
    • Nyaraka za Elimu

MAADHIMISHO YA WIKI YA UPANDAJI MITI YENYE KAULI MBIU ISEMAYO "TANZANIA YA KIJANI INAWEZEKANA, PANDA MITI KWA MAENDELEO YA VIWANDA " KIMKOA YAFANYIKA MANISPAA YA KINONDONI

Tarehe iliyowekwa: April 5th, 2018

 DC HAPI KWA NIABA YA MKUU WA MKOA WA DAR ES SALAAM AWA MGENI RASMI.-ASISITIZA UMUHIMU WA UPANDAJI NA UTUNZAJI WA MITI. 

 Maadhimisho ya wiki ya upandaji miti ngazi ya Mkoa, yameadhimishwa katika Manispaa ya Kinondoni kwa kupanda takriban miti 800 kwenye maeneo mbalimbali ya Mkoa huo ,kutoka katika vitalu vya wakala wa misitu (TFS) kwa kushirikiana na Halmashauri za Mkoa wa Dar es salaam.

 Akiongea katika maadhimisho hayo, yaliyofanyika katika Kata ya Kunduchi, Manispaa ya Kinondoni, Mkuu wa Wilaya hiyo, Mh. Alli Hapi kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam amesema siku hii ni muhimu Sana kwa wananchi kushiriki ili kwa pamoja tuweze kufikisha ujumbe mahususi kwa jamii kuhusiana na umuhimu wa upandaji miti, utunzaji na usimamizi wake. 

 "lengo ni kutumia siku hii maalum kufikisha ujumbe kwa jamii yetu, juu ya kuihamasisha Jamii katika swala zima la upandaji miti, utunzaji na usimamizi wake, na matumizi endelevu juu ya rasilimali zetu za misitu. "Amesema Hapi 

 Akifafanua kuhusiana na kauli mbiu ya mwaka huu isemayo "Tanzania ya Kijani inawezekana panda miti kwa Maendeleo ya viwanda" amesema ni muhimu Sana Tanzania yetu ya viwanda ikaendana na zoezi la upandaji miti kwani kwa kufanya hivyo itapunguza uharibifu wa tabaka la juu la anga(ozone) itokanayo na uzalishwaji wa hewa ya ukaa, ambapo uharibifu unapotokea husababisha miale ya moja kwa moja kushuka na kuumiza viumbe hai. 

 Ameongeza kuwa upandaji wa miti na utunzaji wa Mazingira ni ajira nzuri kwa vijana, kwani Mazingira yawapo mazuri na safi huwa vivutio kwa watu kupumnzika na kufanya shughuli zao .

 Aidha amezitaka Halmashauri zote za Mkoa wa Dar es salaam kuweka mifumo ya maji katika barabara zilizopandwa miti ili kuweza kurahisisha umwagiliaji. 

  Awali akitoa taarifa mbele ya Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni, mwakilishi wa wakala wa huduma za  misitu nchini (TFS)  Bi Dyaga Follen Mkomwa, amesema siku hii ya upandaji miti kitaifa inatokana na waraka wa Serikali namba moja wa mwaka 2000 ,ambapo kila Wilaya nchini inatakiwa kupanda miche ya miti milioni moja na laki tano kila mwaka. 

 Ameongeza kuwa misitu iliyopo katika Mkoa wa Dar es salaam pamoja na upandaji huu wa miti ni jitihada za viongozi mbalimbali wa Serikali katika kusimamia utunzaji Mazingira, ambayo inasaidia kuboresha Mazingira na kufyonza hewa ukaa inayozalishwa viwandani kwa sasa, na pia kukabiliana na ongezeko kubwa la hewa ukaa itakayozalishwa kutokana na mkakati uliopo wa kuongeza viwanda katika Mkoa wa Dar es salaam. 

 Maadhimisho haya kimkoa yamehudhuriwa na viongozi mbalimbali wa vyama na serikali kutoka katika Halmashauri zote za Mkoa wa Dar es salaam,  ambapo Kitaifa yanadhimishwa mkoani Shinyanga katika wilaya ya Kishapu.

 Imeandaliwa na
 Kitengo Cha habari na uhusiano
 Manispaa ya Kinondoni.

Matangazo

  • UTOAJI WA MIKOPO KWA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU April 01, 2025
  • TANGAZO March 22, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI October 05, 2024
  • MATOKEO YA USAILI WA VITENDO KADA YA AFISA TEHAMA MSAIDIZI ULIOFANYIKA TAREHE 25/03/2024 March 25, 2024
  • Tazama zote

Habari mpya

  • ZAIDI YA MITI 1200 YAPANDWA KUADHIMISHA MIAKA 63 YA UHURU

    December 09, 2024
  • MAAMBUKIZI UKIMWI YAPUNGUA

    December 01, 2024
  • MAAMBUKIZI YA VIRUSI VYA UKIMWI YASHUKA KINONDONI

    November 29, 2024
  • WENYEVITI NA WAJUMBE WAPYA WAPEWA MAELEKEZO YA MAJUKUMU YAO

    November 28, 2024
  • Tazama zote

Picha Jongefu

IFAHAMU KATA YA MZIMUNI, MANISPAA YA KINONDONI
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • MWONGOZO WA NAMNA YA KUTUMIA MFUMO WA TAUSI
  • UJASIRIAMALI NA UTOAJI MIKOPO
  • MAKTABA YA PICHA
  • TAARIFA KWA UMMA
  • HOTUBA
  • ORODHA YA WAHESHIMIWA MADIWANI
  • MKATABA WA HUDUMA KWA MTEJA
  • MIRADI ILIYOKAMILIKA

Viunganishi Linganifu

  • TOVUTI KUU YA IKULU
  • TOVUTI YA UTUMISHI
  • TOVUTI YA OR-TAMISEMI
  • TOVUTI YA OFISI YA TAKWIMU YA TAIFA
  • TOVUTI YA IDARA YA HABARI MAELEZO
  • TOVUTI KUU YA SERIKALI

Idadi ya Wasomaji

world map hits counter

Waliotembelea tovuti

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    2 Barabara ya Morogoro, 14883 Dar es Salaam

    Anuani ya Posta: S.L.P 31902

    Simu ya mezani: +255222170173

    Simu ya mkononi: +255733241052

    Barua pepe: md@kinondonimc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya tovuti

Hatimiliki © 2017 Halmashauri ya Manispaa ya Kinondoni. Haki Zote Zimehifadhiwa.