• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
Kinondoni Municipal Council
Kinondoni Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Kinondoni

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Maadili ya Msingi
    • Wasifu wa Halmashauri
  • Utawala
    • Divisheni
      • Miundombinu, Vijijini na Mijini
      • Huduma za Afya, Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Elimu ya Awali na Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Usimamizi wa Rasilimali Watu
    • Vitengo
      • Usimamizi wa Taka na Usafi wa Mazingira
      • Uhifadhi wa Maliasili na Mazingira
      • Michezo, Utamaduni na Sanaa
      • Fedha na Mahesabu
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Usimamizi wa Manunuzi
      • TEHAMA
      • Mawasiliano Serikalini
    • Ofisi ya Mtendaji wa Kata
    • Ofisi ya Mtendaji wa Mtaa
    • Kata
      • Bunju
      • Hananasif
      • Kawe
      • Kigogo
      • Kijitonyama
      • Kinondoni
      • Kunduchi
      • Mabwepande
      • Magomeni
      • Makongo
      • Makumbusho
      • Mbezi Juu
      • Mbweni
      • Mikocheni
      • Msasani
      • Mwananyamala
      • Mzimuni
      • Ndugumbi
      • Tandale
      • Wazo
    • Muundo wa Taasisi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Fukwe na Visiwa
    • Sehemu za kitamaduni, ngoma za asili na sanaa za mikono
    • Matukio ya Utalii
  • Huduma zetu
    • Biashara
    • Huduma za Elimu
    • Ujasiriamali
    • Ushauri katika Kilimo
    • Vituo vya Ukusanyaji Mapato
    • Vibali vya Ujenzi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Uongozi
      • Mipangomiji na Mazingira
      • Maadili
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhibiti UKIMWI
    • Ratiba ya Vikao
    • Ratiba ya Meya
  • Miradi
    • Iliyopangwa
    • Inayoendelea
    • Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Sera
    • Makala
    • Mpango mkakati
    • Taarifa mbalimbali
    • Mkataba wa huduma
    • Fomu za maombi
    • Vibali vya Ujenzi
    • Nyaraka za Elimu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video
    • Habari
    • Matukio

KINONDONI YATANGAZA RASMI MAENEO MAALUMU (SMART AREA).

Tarehe iliyowekwa: August 3rd, 2021

Maeneo hayo yametangazwa na Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni Mhe.Godwin Gondwe alipokuwa katika ziara yake ya kikazi ya ukaguzi wa miradi ya upanuzi wa barabara inayosimamiwa na Tanroads kwa lengo la kujiridhisha na hatua za utekelezaji zilizofikiwa, ikiwa ni pamoja na thamani ya fedha na kiwango cha mradi katika ubora.

Amesema kutangaza kwa maeneo haya ya Magomeni mataa hadi Morroco na Morroco hadi Mwenge kuwa maeneo maalumu "smart area" ni katika kutekeleza agizo la Waziri Mkuu wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Kassim Majaliwa Kassim la kuhakikisha kila Halmashauri inakuwa na eneo kwa ajili ya vivutio vya utalii.

Aidha ameongeza kuwa  maeneo haya yanatakiwa kutunzwa kwa kufanyiwa Usafi, kupendezeshwa kwa kuotesha maua na nyasi, kutokubadilishwa mandhari yake ikiwa ni pamoja na kutokuwepo uharibifu wowote pembezoni mwa barabara.

" Tanroads hakikisheni mnasimamia suala la wamachinga kwenda eneo walilopangiwa ili kupisha ujenzi na ukamilishaji wa barabara unaoendelea kwa sasa, lakini pia simamieni Mradi huu wa barabara unaopita eneo la Morroco hadi Mwenge ukamilike kwa wakati, barabara hii itunzwe na iheshimike ili wananchi wanufaike, tusingependa eneo hili liharibiwe, lichafuliwe, bali liboreshwe na kutunzwa, nalitangaza Rasmi kuwa "smart area" Ameongeza Gondwe.

Naye Mhandisi kutoka Tanroads Bi. Mwanaisha Rajab alipotakiwa kuzungumza amesema anayapokea maelekezo yote kutoka kwa uongozi na kuhakikisha miradi yote ya barabara inayosimamiwa na Tanroads kwa Manispaa ya Kinondoni inamalizika kwa wakati kutokana na makubaliano ya mkataba na kwa viwango vilivyokusudiwa ili viweze kuleta tija kwa maslahi mapana ya wananchi wa Kinondoni na Taifa kwa ujumla.

 Katika hatua nyingine Mkuu huyo wa Wilaya Mhe. Godwin Gondwe amezitaka Taasisi na mamlaka husika zikiwemo Tanesco na Dawasco kushirikiana kwa pamoja katika kuhakikisha miradi ya Serikali inatekelezwa ili iweze kuondokana na changamoto zinazoweza kukwamisha utekelezaji wake kwa viwango vilivyokusudiwa na yenye kuleta tija kwa Taifa.

Katika ziara hiyo iliyohusisha Kamati ya ulinzi na usalama ya Wilaya imetembelea mradi wa upanuzi wa barabara ya Morroco-Mwenge yenye urefu wa Km 4.3, barabara ya Ardhi-Makongo yenye urefu wa Km 4.5, na barabara ya Madale.

Imeandaliwa na

Kitengo Cha Habari na Uhusiano

Manispaa ya Kinondoni.

Matangazo

  • KUFUTA TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI March 14, 2023
  • TANGAZO LA AJIRA YA MKATABA March 13, 2023
  • TANGAZO KWA WASIOLIPIA VIWANJA BOKO DOVYA (KWA SOMJI) NA SALASALA February 15, 2023
  • MABADILIKO YA SIKU YA MAFUNZO YA WASIMAMIZI WA MAUDHUI, WASIMAMIZI WA TEHAMA NA MAKARANI WA SENSA YA WATU NA MAKAZI 2022 July 28, 2022
  • Tazama zote

Habari mpya

  • JAPAN YAIPATIA MSAADA MZIMUNI SEKONDARI

    March 15, 2023
  • VIKUNDI VYAASWA MATUMIZI SAHIHI YA MIKOPO

    February 18, 2023
  • "HAKUNA TIMU KUBWA ZAIDI YA KMC FC"

    February 18, 2023
  • ULINZI NI KIPAUMBELE KINODONI-DC SAAD

    February 12, 2023
  • Tazama zote

Picha Jongefu

VIKUNDI VILIVYOSEPA NA BILIONI 11 VYAKALIWA KOONI MANISPAA YA KINONDONI. REJESHENI...
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • TARATIBU ZA KUPATA KIBALI CHA UJENZI
  • MKATABA WA HUDUMA KWA MTEJA
  • UJASIRIAMALI NA UTOAJI MIKOPO
  • VITUO VYA KUKUSANYIA MAPATO
  • ORODHA YA WAHESHIMIWA MADIWANI
  • RATIBA YA MSTAHIKI MEYA
  • TAARIFA KWA UMMA
  • MIRADI ILIYOKAMILIKA

Viunganishi Linganifu

  • TOVUTI KUU YA IKULU
  • TOVUTI YA UTUMISHI
  • TOVUTI YA OR-TAMISEMI
  • TOVUTI YA OFISI YA TAKWIMU YA TAIFA
  • TOVUTI YA IDARA YA HABARI MAELEZO
  • TOVUTI KUU YA SERIKALI

Idadi ya Wasomaji

world map hits counter

Waliotembelea tovuti

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    2 Barabara ya Morogoro, 14883 Dar es Salaam

    Anuani ya Posta: S.L.P 31902

    Simu ya mezani: +255 22 2170173

    Simu ya mkononi:

    Barua pepe: md@kinondonimc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya tovuti

Hatimiliki © 2017 Halmashauri ya Manispaa ya Kinondoni. Haki Zote Zimehifadhiwa.