• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
Kinondoni Municipal Council
Kinondoni Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Kinondoni

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Maadili ya Msingi
    • Wasifu wa Halmashauri
  • Utawala
    • Divisheni
      • Miundombinu, Vijijini na Mijini
      • Huduma za Afya, Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Elimu ya Awali na Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Usimamizi wa Rasilimali Watu
    • Vitengo
      • Usimamizi wa Taka na Usafi wa Mazingira
      • Uhifadhi wa Maliasili na Mazingira
      • Michezo, Utamaduni na Sanaa
      • Fedha na Mahesabu
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Usimamizi wa Manunuzi
      • TEHAMA
      • Mawasiliano Serikalini
    • Kata
      • Bunju
      • Hananasif
      • Kawe
      • Kigogo
      • Kijitonyama
      • Kinondoni
      • Kunduchi
      • Mabwepande
      • Magomeni
      • Makongo
      • Makumbusho
      • Mbezi Juu
      • Mbweni
      • Mikocheni
      • Msasani
      • Mwananyamala
      • Mzimuni
      • Ndugumbi
      • Tandale
      • Wazo
    • Muundo wa Taasisi
    • Ofisi ya Mtendaji wa Kata
    • Ofisi ya Mtendaji wa Mtaa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya utalii
      • Fukwe na Visiwa
      • Sehemu za kitamaduni, ngoma za asili na sanaa za mikono
    • Utalii
      • Matukio ya Utalii
      • Royal Tour Bus
  • Huduma zetu
    • Biashara
    • Huduma za Elimu
    • Ujasiriamali
    • Ushauri katika Kilimo
    • Vituo vya Ukusanyaji Mapato
    • Vibali vya Ujenzi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Uongozi
      • Mipangomiji na Mazingira
      • Maadili
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhibiti UKIMWI
    • Ratiba ya Vikao
    • Ratiba ya Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Sera
    • Makala
    • Mpango mkakati
    • Taarifa mbalimbali
    • Mkataba wa huduma kwa mteja
    • Fomu za maombi
    • Vibali vya Ujenzi Vilivyotolewa
    • Nyaraka za Elimu

KINONDONI YASOGEZA HUDUMA KWA WANANCHI, KWA KUFUNGUA VITUO VYA KUKUSANYA MAPATO KATIKA KATA TANO

Tarehe iliyowekwa: September 19th, 2018

Hayo yamebainishwa na Mstahiki Meya wa Manispaa hiyo Mhe. Benjamini Sitta, alipokuwa akiongea na waandishi wa habari katika mahojiano yaliyofanyika mara baada ya kikao cha Baraza la Madiwani kilichofanyika leo katika ukumbi wa mikutano wa Manispaa.

Amesema lengo la ufunguzi wa vituo hivyo ni kutekeleza mpango mkakati wa kuongeza mapato, unaoenda sambamba na ukusanyaji wake, ikihusisha ulipaji wa tozo mbalimbali katika Halmashauri, lakini pia ni katika kuwajali wananchi kwa kuwasogezea huduma hiyo kwa ukaribu zaidi kutakakorahisisha ulipaji wa tozo na kodi mbalimbali ambapo hapo awali iliwalazimu kufuata huduma hiyo katika ofisi za Halmashauri.

"Leo tulikuwa na kikao cha kawaida cha Baraza la Madiwani, na katika kikao hicho,  yamejadiliwa mambo mengi yakiwemo mpango mkakati wa kukabiliana na changamoto ya ukusanyaji mapato na kama Halmashauri tumekuja na mkakati thabiti wa kukabiliana na swala hilo kwa kufungua vituo vya kimapato katika Kata tano za Halmashauri yetu." Amefafanua Meya Sitta.

Aidha, amezitaja Kata na  vituo  hivyo kuwa ni  Bunju, Tegeta-Kibo Complex, Mwenge, Msasani na Mikocheni na kuanisha huduma zitakazopatikana kuwa ni ukataji na ulipaji wa  leseni za vileo, Ada za kupima afya, ada za TFDA, na ada za SUMATRA kwa vyombo vya usafiri kama vile pikipiki na bajaji.

Aidha, katika kikao hicho cha Baraza kilichojumuisha Wakuu wa Idara na Vitengo, Waheshimiwa Madiwani, TARURA, TAKUKURU na Jeshi la Polisi, kimejadili ajenda kuu tatu ambazo ni taarifa za utekelezaji wa Kamati mbalimbali za Kudumu za robo ya nne, taarifa ya utekelezaji wa miradi ya maendeleo, pamoja na kuthibitisha taarifa za Kamati mbalimbali za Kudumu.

Katika hatua nyingine Meya Sitta amewataka wananchi wa Manispaa ya Kinondoni kuvitumia vituo vilivyofunguliwa katika Kata na maeneo wanakoishi kwa ajili ya kulipia tozo mbalimbali  kwani ndio njia rahisi ya kuepukana na mlolongo wa foleni wakati wa kupatiwa huduma hizo.

Aidha, kikao hicho kimeenda sambamba na kuapishwa kwa Mbunge wa jimbo la Kinondoni Mhe. Abdallah Mtulia, aliyeshinda uchaguzi mara baada ya kufanyika uchaguzi wa  marudio katika jimbo hilo.


Imeandaliwa na

Kitengo cha Uhusiano na Habari.

Manispaa ya Kinondoni.

Matangazo

  • UTOAJI WA MIKOPO KWA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU April 01, 2025
  • TANGAZO March 22, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI October 05, 2024
  • MATOKEO YA USAILI WA VITENDO KADA YA AFISA TEHAMA MSAIDIZI ULIOFANYIKA TAREHE 25/03/2024 March 25, 2024
  • Tazama zote

Habari mpya

  • ZAIDI YA MITI 1200 YAPANDWA KUADHIMISHA MIAKA 63 YA UHURU

    December 09, 2024
  • MAAMBUKIZI UKIMWI YAPUNGUA

    December 01, 2024
  • MAAMBUKIZI YA VIRUSI VYA UKIMWI YASHUKA KINONDONI

    November 29, 2024
  • WENYEVITI NA WAJUMBE WAPYA WAPEWA MAELEKEZO YA MAJUKUMU YAO

    November 28, 2024
  • Tazama zote

Picha Jongefu

IFAHAMU KATA YA MZIMUNI, MANISPAA YA KINONDONI
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • MWONGOZO WA NAMNA YA KUTUMIA MFUMO WA TAUSI
  • UJASIRIAMALI NA UTOAJI MIKOPO
  • MAKTABA YA PICHA
  • TAARIFA KWA UMMA
  • HOTUBA
  • ORODHA YA WAHESHIMIWA MADIWANI
  • MKATABA WA HUDUMA KWA MTEJA
  • MIRADI ILIYOKAMILIKA

Viunganishi Linganifu

  • TOVUTI KUU YA IKULU
  • TOVUTI YA UTUMISHI
  • TOVUTI YA OR-TAMISEMI
  • TOVUTI YA OFISI YA TAKWIMU YA TAIFA
  • TOVUTI YA IDARA YA HABARI MAELEZO
  • TOVUTI KUU YA SERIKALI

Idadi ya Wasomaji

world map hits counter

Waliotembelea tovuti

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    2 Barabara ya Morogoro, 14883 Dar es Salaam

    Anuani ya Posta: S.L.P 31902

    Simu ya mezani: +255222170173

    Simu ya mkononi: +255733241052

    Barua pepe: md@kinondonimc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya tovuti

Hatimiliki © 2017 Halmashauri ya Manispaa ya Kinondoni. Haki Zote Zimehifadhiwa.