• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
Kinondoni Municipal Council
Kinondoni Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Kinondoni

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Maadili ya Msingi
    • Wasifu wa Halmashauri
  • Utawala
    • Divisheni
      • Miundombinu, Vijijini na Mijini
      • Huduma za Afya, Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Elimu ya Awali na Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Usimamizi wa Rasilimali Watu
    • Vitengo
      • Usimamizi wa Taka na Usafi wa Mazingira
      • Uhifadhi wa Maliasili na Mazingira
      • Michezo, Utamaduni na Sanaa
      • Fedha na Mahesabu
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Usimamizi wa Manunuzi
      • TEHAMA
      • Mawasiliano Serikalini
    • Kata
      • Bunju
      • Hananasif
      • Kawe
      • Kigogo
      • Kijitonyama
      • Kinondoni
      • Kunduchi
      • Mabwepande
      • Magomeni
      • Makongo
      • Makumbusho
      • Mbezi Juu
      • Mbweni
      • Mikocheni
      • Msasani
      • Mwananyamala
      • Mzimuni
      • Ndugumbi
      • Tandale
      • Wazo
    • Muundo wa Taasisi
    • Ofisi ya Mtendaji wa Kata
    • Ofisi ya Mtendaji wa Mtaa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya utalii
      • Fukwe na Visiwa
      • Sehemu za kitamaduni, ngoma za asili na sanaa za mikono
    • Utalii
      • Matukio ya Utalii
      • Royal Tour Bus
  • Huduma zetu
    • Biashara
    • Huduma za Elimu
    • Ujasiriamali
    • Ushauri katika Kilimo
    • Vituo vya Ukusanyaji Mapato
    • Vibali vya Ujenzi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Uongozi
      • Mipangomiji na Mazingira
      • Maadili
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhibiti UKIMWI
    • Ratiba ya Vikao
    • Ratiba ya Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Sera
    • Makala
    • Mpango mkakati
    • Taarifa mbalimbali
    • Mkataba wa huduma kwa mteja
    • Fomu za maombi
    • Vibali vya Ujenzi Vilivyotolewa
    • Nyaraka za Elimu

KINONDONI YAPONGEZWA KWA UBORA NA UTEKELEZAJI WA MIRADI

Tarehe iliyowekwa: December 14th, 2020

NI ULE WA UJENZI WA  HOSPITALI YA MABWEPANDE KWA GHARAMA YA TSH BILIONI 2.5, MAPATO YAKE YA NDANI HADI KUKAMILIKA KWAKE.

Pongezi hizo zimetolewa na Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Mheshimiwa Abubakar Kunenge alipofanya ziara katika Manispaa hiyo ya kukagua utekelezaji wa miradi ya maendeleo hususani ujenzi wa Hospitali ya Mabwepande iliyopo katika eneo la Mabwepande Manispaa ya Kinondoni.

Amesema Manispaa hiyo ndiyo pekee kwa Mkoa wa Dar es Salaam iliyoweza kujenga Hospitali kubwa yenye kiwango kinachoridhisha itakayokuwa na uwezo wa kutoa huduma kwa wananchi kwa kutumia mapato yake ya ndani.


Amesema "Kinondoni mnafanya vizuri kwa habari ya miradi, mnatafsiri vizuri maagizo ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Joseph Magufuli kwa kusogeza huduma karibu na wananchi kwa ujenzi wa hospitali hii na inabidi Halmashauri nyingine zije kujifunza hapa kwenu kwani ndio Halmashauri ya mfano ninayotamani Halmashauri nyingine ziwe" Amesema Kunenge.

Naye Mstahiki Meya wa Manispaa hiyo Mheshimiwa Songoro Mnyonge alipotakiwa kufafanua jambo amesema kuwa Hospitali hiyo ya Mabwepande inayo uwezo wa kuhudumia wagonjwa wa nje 400 hadi 700 kwa siku na wagonjwa wa kulazwa 187 hadi 224 kwa siku.

Aidha Mstahiki Meya pia ameahidi kuyatekeleza maagizo yote aliyopewa na Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Mheshimiwa Kunenge kwa kushirikiana na watendaji pamoja na kutekeleza mikakati kwa kutenga fedha katika bajeti ya 2021/2122.

Alipotakiwa kuzitaja changamoto zinazoikabili Hospitali ya Mabwepande, Mganga Mfawidhi wa Hospital hiyo Dkt. Christowelu Mande amesema ni ukosefu wa gari ya kubebea wagonjwa hali inayopelekea mazingira magumu wakati wa uhitaji wake.

Katika hatua nyingine Mganga Mkuu wa Manispaa hiyo Dkt. Samweli Laiser amesema Hospitali ya Mabwepande inatarajiwa kutumia kiasi cha shilingi za Kitanzania takribani Bilioni 2.5 hadi kukamilika kwake.

Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam ametembelea mradi wa Hospitali ya Wilaya ya Mabwepande na kiwanda cha kuchakata taka kilichopo Mabwepande pamoja na Zahanati ya Bunju.


Imeandaliwa na

Kitengo Cha Uhusiano na Habari.

Manispaa ya Kinondoni.

Matangazo

  • UTOAJI WA MIKOPO KWA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU April 01, 2025
  • TANGAZO March 22, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI October 05, 2024
  • MATOKEO YA USAILI WA VITENDO KADA YA AFISA TEHAMA MSAIDIZI ULIOFANYIKA TAREHE 25/03/2024 March 25, 2024
  • Tazama zote

Habari mpya

  • ZAIDI YA MITI 1200 YAPANDWA KUADHIMISHA MIAKA 63 YA UHURU

    December 09, 2024
  • MAAMBUKIZI UKIMWI YAPUNGUA

    December 01, 2024
  • MAAMBUKIZI YA VIRUSI VYA UKIMWI YASHUKA KINONDONI

    November 29, 2024
  • WENYEVITI NA WAJUMBE WAPYA WAPEWA MAELEKEZO YA MAJUKUMU YAO

    November 28, 2024
  • Tazama zote

Picha Jongefu

IFAHAMU KATA YA MZIMUNI, MANISPAA YA KINONDONI
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • MWONGOZO WA NAMNA YA KUTUMIA MFUMO WA TAUSI
  • UJASIRIAMALI NA UTOAJI MIKOPO
  • MAKTABA YA PICHA
  • TAARIFA KWA UMMA
  • HOTUBA
  • ORODHA YA WAHESHIMIWA MADIWANI
  • MKATABA WA HUDUMA KWA MTEJA
  • MIRADI ILIYOKAMILIKA

Viunganishi Linganifu

  • TOVUTI KUU YA IKULU
  • TOVUTI YA UTUMISHI
  • TOVUTI YA OR-TAMISEMI
  • TOVUTI YA OFISI YA TAKWIMU YA TAIFA
  • TOVUTI YA IDARA YA HABARI MAELEZO
  • TOVUTI KUU YA SERIKALI

Idadi ya Wasomaji

world map hits counter

Waliotembelea tovuti

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    2 Barabara ya Morogoro, 14883 Dar es Salaam

    Anuani ya Posta: S.L.P 31902

    Simu ya mezani: +255222170173

    Simu ya mkononi: +255733241052

    Barua pepe: md@kinondonimc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya tovuti

Hatimiliki © 2017 Halmashauri ya Manispaa ya Kinondoni. Haki Zote Zimehifadhiwa.