• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
Kinondoni Municipal Council
Kinondoni Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Kinondoni

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Maadili ya Msingi
    • Wasifu wa Halmashauri
  • Utawala
    • Divisheni
      • Miundombinu, Vijijini na Mijini
      • Huduma za Afya, Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Elimu ya Awali na Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Usimamizi wa Rasilimali Watu
    • Vitengo
      • Usimamizi wa Taka na Usafi wa Mazingira
      • Uhifadhi wa Maliasili na Mazingira
      • Michezo, Utamaduni na Sanaa
      • Fedha na Mahesabu
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Usimamizi wa Manunuzi
      • TEHAMA
      • Mawasiliano Serikalini
    • Kata
      • Bunju
      • Hananasif
      • Kawe
      • Kigogo
      • Kijitonyama
      • Kinondoni
      • Kunduchi
      • Mabwepande
      • Magomeni
      • Makongo
      • Makumbusho
      • Mbezi Juu
      • Mbweni
      • Mikocheni
      • Msasani
      • Mwananyamala
      • Mzimuni
      • Ndugumbi
      • Tandale
      • Wazo
    • Muundo wa Taasisi
    • Ofisi ya Mtendaji wa Kata
    • Ofisi ya Mtendaji wa Mtaa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya utalii
      • Fukwe na Visiwa
      • Sehemu za kitamaduni, ngoma za asili na sanaa za mikono
    • Utalii
      • Matukio ya Utalii
      • Royal Tour Bus
  • Huduma zetu
    • Biashara
    • Huduma za Elimu
    • Ujasiriamali
    • Ushauri katika Kilimo
    • Vituo vya Ukusanyaji Mapato
    • Vibali vya Ujenzi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Uongozi
      • Mipangomiji na Mazingira
      • Maadili
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhibiti UKIMWI
    • Ratiba ya Vikao
    • Ratiba ya Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Sera
    • Makala
    • Mpango mkakati
    • Taarifa mbalimbali
    • Mkataba wa huduma kwa mteja
    • Fomu za maombi
    • Vibali vya Ujenzi Vilivyotolewa
    • Nyaraka za Elimu

KINONDONI YAAPISHA WENYEVITI WA SERIKALI ZA MITAA NA WAJUMBE WAKE

Tarehe iliyowekwa: December 2nd, 2019

Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni Mhe. Daniel Chongolo amewataka Wenyeviti wa Serikali za mitaa kuwa wadilifu katika kuwatumikia wananchi walio wachagua na kwamba waepuke kuwa miungu watu.

Mhe. Chongolo ametoa kauli hiyo leo wakati wa hafla ya kuapishwa kwa viongozi wa serikali za mitaa wa Halmashauri hiyo na kueleza kuwa kuapishwa kwao leo hakuwafanyi wakawe miungu watu kwa wananchi badala yake wakawatumikie kwa uadilifu.

Ameongeza kuwa suala la maslahi binafsi haliruhusiwi katika utendaji wao na kwamba hategemei kuona wenyeviti hao wanakwenda kinyume na maelekezo yanayotolewa.

“ Mmekula kiapo cha kwenda kutenda haki majukumu ya kuwatumikia wananchi, hamjala kiapo cha kwenda kuwa miungu watu, kuwa wabaguzi, hamjala kiapo ili mkawe watu wa kupendelea baadhi ya watu, na kuonea wengine"

Aidha Mhe. Chongolo amewaeleza kuwa kuna changamoto ya uonevu wa nyumba na mali za wanyonge hivyo kuwataka viongozi hao wa mitaa wakasimamie changamoto hizo.

 “ Kuna wananchi wanatapeliwa nyumba zao  na wajanja wajanja , ili wajimilikishe wao, kuanzia sasa nitasikitika sana hasa nikitambua nyinyi ambao leo hii ninawashuhudia mkila kiapo hapa mnakwenda kufanya mambo haya , nawaonya awamu hii sitawaacha, hatuwezi kukaa na watu wa hovyo, narudia hatuwezi kukaa na watu wa hovyo” amesisitiza Mhe. Chongolo.

Kwa upande wake Mkurugenzi wa Manispaa Ndugu. Aron Kagurumjuli amewataka wenyeviti wa serikali za mitaa kutumia vizuri madaraka waliyopewa na wananchi ili kuepusha mitafaruku ambayo ilikuwa ikijitokeza kwa baadhi ya wenyeweviti waliomaliza muda wao.

Amefafanua kuwa kazi ya wenyeviti wa serikali za mitaa hazina mishahara na kwamba inahitaji uzalendo mkubwa hivyo kuwataka watumie nafasi zao vizuri ili waweze kuendesha shuguli zao kwa ajili ya kuleta maendeleo kwa wananchi waliowachagua.

Aidha amewaonya wenyeviti hao kuacha mara moja tabia ya kuwatoza fedha wananchi pindi wanapotaka huduma  hivyo kuwaeleza kuwa huduma hizo zinapaswa kutolewa bure na kwamba atakayekwenda kinyume na maelekezo hayo hatamvumilia kwa namna yoyote ile.


Imetolewa na 

Kitengo Cha Habari na Uhusiano

 Manispaa ya Kinondoni.

Matangazo

  • UTOAJI WA MIKOPO KWA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU April 01, 2025
  • TANGAZO March 22, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI October 05, 2024
  • MATOKEO YA USAILI WA VITENDO KADA YA AFISA TEHAMA MSAIDIZI ULIOFANYIKA TAREHE 25/03/2024 March 25, 2024
  • Tazama zote

Habari mpya

  • ZAIDI YA MITI 1200 YAPANDWA KUADHIMISHA MIAKA 63 YA UHURU

    December 09, 2024
  • MAAMBUKIZI UKIMWI YAPUNGUA

    December 01, 2024
  • MAAMBUKIZI YA VIRUSI VYA UKIMWI YASHUKA KINONDONI

    November 29, 2024
  • WENYEVITI NA WAJUMBE WAPYA WAPEWA MAELEKEZO YA MAJUKUMU YAO

    November 28, 2024
  • Tazama zote

Picha Jongefu

IFAHAMU KATA YA MZIMUNI, MANISPAA YA KINONDONI
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • MWONGOZO WA NAMNA YA KUTUMIA MFUMO WA TAUSI
  • UJASIRIAMALI NA UTOAJI MIKOPO
  • MAKTABA YA PICHA
  • TAARIFA KWA UMMA
  • HOTUBA
  • ORODHA YA WAHESHIMIWA MADIWANI
  • MKATABA WA HUDUMA KWA MTEJA
  • MIRADI ILIYOKAMILIKA

Viunganishi Linganifu

  • TOVUTI KUU YA IKULU
  • TOVUTI YA UTUMISHI
  • TOVUTI YA OR-TAMISEMI
  • TOVUTI YA OFISI YA TAKWIMU YA TAIFA
  • TOVUTI YA IDARA YA HABARI MAELEZO
  • TOVUTI KUU YA SERIKALI

Idadi ya Wasomaji

world map hits counter

Waliotembelea tovuti

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    2 Barabara ya Morogoro, 14883 Dar es Salaam

    Anuani ya Posta: S.L.P 31902

    Simu ya mezani: +255222170173

    Simu ya mkononi: +255733241052

    Barua pepe: md@kinondonimc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya tovuti

Hatimiliki © 2017 Halmashauri ya Manispaa ya Kinondoni. Haki Zote Zimehifadhiwa.