• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
Kinondoni Municipal Council
Kinondoni Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Kinondoni

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Maadili ya Msingi
    • Wasifu wa Halmashauri
  • Utawala
    • Divisheni
      • Miundombinu, Vijijini na Mijini
      • Huduma za Afya, Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Elimu ya Awali na Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Usimamizi wa Rasilimali Watu
    • Vitengo
      • Usimamizi wa Taka na Usafi wa Mazingira
      • Uhifadhi wa Maliasili na Mazingira
      • Michezo, Utamaduni na Sanaa
      • Fedha na Mahesabu
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Usimamizi wa Manunuzi
      • TEHAMA
      • Mawasiliano Serikalini
    • Kata
      • Bunju
      • Hananasif
      • Kawe
      • Kigogo
      • Kijitonyama
      • Kinondoni
      • Kunduchi
      • Mabwepande
      • Magomeni
      • Makongo
      • Makumbusho
      • Mbezi Juu
      • Mbweni
      • Mikocheni
      • Msasani
      • Mwananyamala
      • Mzimuni
      • Ndugumbi
      • Tandale
      • Wazo
    • Muundo wa Taasisi
    • Ofisi ya Mtendaji wa Kata
    • Ofisi ya Mtendaji wa Mtaa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya utalii
      • Fukwe na Visiwa
      • Sehemu za kitamaduni, ngoma za asili na sanaa za mikono
    • Utalii
      • Matukio ya Utalii
      • Royal Tour Bus
  • Huduma zetu
    • Biashara
    • Huduma za Elimu
    • Ujasiriamali
    • Ushauri katika Kilimo
    • Vituo vya Ukusanyaji Mapato
    • Vibali vya Ujenzi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Uongozi
      • Mipangomiji na Mazingira
      • Maadili
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhibiti UKIMWI
    • Ratiba ya Vikao
    • Ratiba ya Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Sera
    • Makala
    • Mpango mkakati
    • Taarifa mbalimbali
    • Mkataba wa huduma kwa mteja
    • Fomu za maombi
    • Vibali vya Ujenzi Vilivyotolewa
    • Nyaraka za Elimu

KINONDONI YAADHIMISHA SIKU YA MVUVI DUNIANI KWA KUTOA ZAWADI KWA WAVUVI WALIOSHINDA UVUVI WA SAMAKI -SOKO LA SAMAKI MSASANI

Tarehe iliyowekwa: November 23rd, 2017


  Manispaa ya Kinondoni leo imeadhimisha siku ya mvuvi duniani kwa kutoa zawadi kwa wavuvi washindi wa mashindano ya uvuvi wa samaki zoezi lililodumu kwa takribani masaa kumi na moja (11:00).kuanzia saa 12:00 alfajiri hadi saa 11:00Jioni kwa kuvua samaki kwa washiriki wa soko la Samaki lililopo Msasani jijini Dar Es Salaam. 

 Zawadi hizo zimetolewa na Mstahiki Meya wa Manispaa hiyo, Mh Benjamin Sitta alipokuwa mgeni rasmi kwenye mashindano ya kushindanisha  wavuvi hao na kupata washindi watatu kwa vigezo vya wingi wa kilo, kwenye hafla iliyofanyika katika viwanja vilivyopo sokoni hapo 

 Amesema wakati umefika sasa kwa wavuvi kujitambua kuwa, wanalojukumu kubwa la kuhakikisha wanaendana na kasi iliyopo ya uchumi wa viwanda , kwani wao ndio kundi kubwa linalotakiwa ili viwanda vya samaki viweze kujengwa na vijana wengi kupata ajira. 

 Ameongeza kuwa zawadi hizi za fedha taslimu zinazotolewa leo ni kuthibitisha uwezo mkubwa walionao vijana hawa walioko kwenye kundi hili la wavuvi katika kushiriki uchumi wa viwanda kwa kuhakikisha malighafi za kuendesha viwanda vya samaki zinaptikana. 

 Naye Afisa uvuvi wa Manispaa hiyo Bi. Grace Kakama amesema ni vema wavuvi wakaungana kwa pamoja kuchangamkia fursa za uwezeshaji zinapojitokeza ,pamoja na kuwa wamoja katika vikundi vya ulinzi wa rasilimali za bahari na pwani vilivyoanzishwa chini ya sheria ya uvuvi na. 22 ya mwaka 2003 kwa lengo la kuwaunganisha wavuvi na kuwa wamoja katika kuendeleza sekta ya uvuvi Nchini. 

 Aidha amewataja washiriki walioshiriki shindano la uvuvi kwa aina za vifaa vilivyotumika na idadi yao kuwa ni ishirini na sita (26),na kilo za samaki zilizopatikana ni 107.7

 Amebainisha washindi hao kuwa ni Selemani Marijani aliyepata Kg 24 na kuzawadiwa fedha taslimu tsh 400,000/=, mshindi wa pili ni Zuberi Ayubu aliyepata kg 18 na kuzawadiwa tsh 300,000/= na mshindi wa tatu ni Hamisi Juma aliyepata kg 14.5 na kuzawadiwa tsh 200,000/=.

 Maadhimisho haya huadhimishwa kila mwaka tarehe 21 Novemba, na kwa Manispaa ya Kinondoni yamefanyika soko la Samaki kwa kauli mbiu ya wavuvi wa sokoni hapo isemayo "Uvuvi endelevu wa Jodari kwa Maendeleo ya viwanda. "

 Imetolewa na
 Kitengo cha Uhusiano na habari
 Manispaa ya Kinondoni

Matangazo

  • UTOAJI WA MIKOPO KWA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU April 01, 2025
  • TANGAZO March 22, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI October 05, 2024
  • MATOKEO YA USAILI WA VITENDO KADA YA AFISA TEHAMA MSAIDIZI ULIOFANYIKA TAREHE 25/03/2024 March 25, 2024
  • Tazama zote

Habari mpya

  • ZAIDI YA MITI 1200 YAPANDWA KUADHIMISHA MIAKA 63 YA UHURU

    December 09, 2024
  • MAAMBUKIZI UKIMWI YAPUNGUA

    December 01, 2024
  • MAAMBUKIZI YA VIRUSI VYA UKIMWI YASHUKA KINONDONI

    November 29, 2024
  • WENYEVITI NA WAJUMBE WAPYA WAPEWA MAELEKEZO YA MAJUKUMU YAO

    November 28, 2024
  • Tazama zote

Picha Jongefu

IFAHAMU KATA YA MZIMUNI, MANISPAA YA KINONDONI
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • MWONGOZO WA NAMNA YA KUTUMIA MFUMO WA TAUSI
  • UJASIRIAMALI NA UTOAJI MIKOPO
  • MAKTABA YA PICHA
  • TAARIFA KWA UMMA
  • HOTUBA
  • ORODHA YA WAHESHIMIWA MADIWANI
  • MKATABA WA HUDUMA KWA MTEJA
  • MIRADI ILIYOKAMILIKA

Viunganishi Linganifu

  • TOVUTI KUU YA IKULU
  • TOVUTI YA UTUMISHI
  • TOVUTI YA OR-TAMISEMI
  • TOVUTI YA OFISI YA TAKWIMU YA TAIFA
  • TOVUTI YA IDARA YA HABARI MAELEZO
  • TOVUTI KUU YA SERIKALI

Idadi ya Wasomaji

world map hits counter

Waliotembelea tovuti

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    2 Barabara ya Morogoro, 14883 Dar es Salaam

    Anuani ya Posta: S.L.P 31902

    Simu ya mezani: +255222170173

    Simu ya mkononi: +255733241052

    Barua pepe: md@kinondonimc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya tovuti

Hatimiliki © 2017 Halmashauri ya Manispaa ya Kinondoni. Haki Zote Zimehifadhiwa.