• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
Kinondoni Municipal Council
Kinondoni Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Kinondoni

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Maadili ya Msingi
    • Wasifu wa Halmashauri
  • Utawala
    • Divisheni
      • Miundombinu, Vijijini na Mijini
      • Huduma za Afya, Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Elimu ya Awali na Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Usimamizi wa Rasilimali Watu
    • Vitengo
      • Usimamizi wa Taka na Usafi wa Mazingira
      • Uhifadhi wa Maliasili na Mazingira
      • Michezo, Utamaduni na Sanaa
      • Fedha na Mahesabu
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Usimamizi wa Manunuzi
      • TEHAMA
      • Mawasiliano Serikalini
    • Kata
      • Bunju
      • Hananasif
      • Kawe
      • Kigogo
      • Kijitonyama
      • Kinondoni
      • Kunduchi
      • Mabwepande
      • Magomeni
      • Makongo
      • Makumbusho
      • Mbezi Juu
      • Mbweni
      • Mikocheni
      • Msasani
      • Mwananyamala
      • Mzimuni
      • Ndugumbi
      • Tandale
      • Wazo
    • Muundo wa Taasisi
    • Ofisi ya Mtendaji wa Kata
    • Ofisi ya Mtendaji wa Mtaa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya utalii
      • Fukwe na Visiwa
      • Sehemu za kitamaduni, ngoma za asili na sanaa za mikono
    • Utalii
      • Matukio ya Utalii
      • Royal Tour Bus
  • Huduma zetu
    • Biashara
    • Huduma za Elimu
    • Ujasiriamali
    • Ushauri katika Kilimo
    • Vituo vya Ukusanyaji Mapato
    • Vibali vya Ujenzi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Uongozi
      • Mipangomiji na Mazingira
      • Maadili
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhibiti UKIMWI
    • Ratiba ya Vikao
    • Ratiba ya Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Sera
    • Makala
    • Mpango mkakati
    • Taarifa mbalimbali
    • Mkataba wa huduma kwa mteja
    • Fomu za maombi
    • Vibali vya Ujenzi Vilivyotolewa
    • Nyaraka za Elimu

KINONDONI YAADHIMISHA SIKU YA MTOTO WA AFRIKA KWA VITENDO

Tarehe iliyowekwa: June 16th, 2021

Akiongea katika maadhimisho hayo yaliyofanyika katika viwanja vya Kijitonyama, Katibu Tawala wa Wilaya ya Kinondoni Bi. Stella Msofe amesema siku hii ni muhimu kwa watoto wote na hivyo wanastahili kupata haki sawa bila kuwabagua kama kaulimbiu ya mwaka huu inavyosema" Tutekeleze agenda 2040: Kwa Afrika inayolinda haki za watoto"

Amesema Serikali ya awamu ya sita inatambua umuhimu wa siku ya mtoto wa Afrika na ndio maana inaadhimishwa kwa kaulimbiu yenye lengo la kuwakumbusha wasimamizi wa sera na sheria, wazazi, walezi na jamii yote kwa ujumla kujua wajibu wao katika kulinda na kusimamia haki za watoto.

Amesema "Sisi kama watanzania tunayo sera ya mtoto ya mwaka 2008 ambayo ilipelekea kutungwa kwa sheria yetu ya namba 21 ya mwaka 2009 na sera hii ina vipengele vikuu vitano muhimu ambavyo watoto wanastahili kuvitambua na kuvielewa. Vipengele hivyo  ni haki ya mtoto kuishi kabla na baada ya kuzaliwa, haki ya kuendelezwa, haki ya kulindwa, haki ya kushirikishwa na kushiriki  pamoja na haki ya kupinga ubaguzi.

Naye Mstahiki Meya wa Manispaa hiyo Mhe. Songoro Mnyonge alipokuwa akimkaribisha Katibu Tawala Wilaya amesisitiza umuhimu wa kutambua siku hii ya mtoto wa Afrika na kuwataka wazazi, waalimu na jamii nzima kuhakikisha inazingatia kwa kuwapatia watoto haki zao wanazostahili ikiwa ni pamoja na kuipongeza Manispaa hiyo kwa maandalizi mazuri.

Kadhalika Bi. Khalima Kahema Mkuu wa Idara ya Maendeleo ya Jamii kwa niaba ya Mkurugenzi wa Manispaa ya Kinondoni amesema kwa kutambua umuhimu wa siku ya mtoto wa Afrika na kaulimbiu yake, wametenga bajeti kwa ajili hiyo na kuhakikisha inatumika kwa malengo yaliyokusudiwa.

Maadhimisho haya ya siku ya Mtoto wa Afrika hufanyika Juni 16 ya kila mwaka ambapo Tanzania huungana na mataifa mengine ya Umoja wa Afrika kufanya kumbukizi ya mauaji ya watoto yaliyofanywa na utawala wa makaburu kitongoji cha Soweto nchini Afrika Kusini.

Imeandaliwa na

Kitengo cha Habari na Uhusiano Manispaa ya Kinondoni.

Matangazo

  • UTOAJI WA MIKOPO KWA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU April 01, 2025
  • TANGAZO March 22, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI October 05, 2024
  • MATOKEO YA USAILI WA VITENDO KADA YA AFISA TEHAMA MSAIDIZI ULIOFANYIKA TAREHE 25/03/2024 March 25, 2024
  • Tazama zote

Habari mpya

  • ZAIDI YA MITI 1200 YAPANDWA KUADHIMISHA MIAKA 63 YA UHURU

    December 09, 2024
  • MAAMBUKIZI UKIMWI YAPUNGUA

    December 01, 2024
  • MAAMBUKIZI YA VIRUSI VYA UKIMWI YASHUKA KINONDONI

    November 29, 2024
  • WENYEVITI NA WAJUMBE WAPYA WAPEWA MAELEKEZO YA MAJUKUMU YAO

    November 28, 2024
  • Tazama zote

Picha Jongefu

IFAHAMU KATA YA MZIMUNI, MANISPAA YA KINONDONI
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • MWONGOZO WA NAMNA YA KUTUMIA MFUMO WA TAUSI
  • UJASIRIAMALI NA UTOAJI MIKOPO
  • MAKTABA YA PICHA
  • TAARIFA KWA UMMA
  • HOTUBA
  • ORODHA YA WAHESHIMIWA MADIWANI
  • MKATABA WA HUDUMA KWA MTEJA
  • MIRADI ILIYOKAMILIKA

Viunganishi Linganifu

  • TOVUTI KUU YA IKULU
  • TOVUTI YA UTUMISHI
  • TOVUTI YA OR-TAMISEMI
  • TOVUTI YA OFISI YA TAKWIMU YA TAIFA
  • TOVUTI YA IDARA YA HABARI MAELEZO
  • TOVUTI KUU YA SERIKALI

Idadi ya Wasomaji

world map hits counter

Waliotembelea tovuti

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    2 Barabara ya Morogoro, 14883 Dar es Salaam

    Anuani ya Posta: S.L.P 31902

    Simu ya mezani: +255222170173

    Simu ya mkononi: +255733241052

    Barua pepe: md@kinondonimc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya tovuti

Hatimiliki © 2017 Halmashauri ya Manispaa ya Kinondoni. Haki Zote Zimehifadhiwa.