• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
Kinondoni Municipal Council
Kinondoni Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Kinondoni

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Maadili ya Msingi
    • Wasifu wa Halmashauri
  • Utawala
    • Divisheni
      • Miundombinu, Vijijini na Mijini
      • Huduma za Afya, Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Elimu ya Awali na Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Usimamizi wa Rasilimali Watu
    • Vitengo
      • Usimamizi wa Taka na Usafi wa Mazingira
      • Uhifadhi wa Maliasili na Mazingira
      • Michezo, Utamaduni na Sanaa
      • Fedha na Mahesabu
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Usimamizi wa Manunuzi
      • TEHAMA
      • Mawasiliano Serikalini
    • Kata
      • Bunju
      • Hananasif
      • Kawe
      • Kigogo
      • Kijitonyama
      • Kinondoni
      • Kunduchi
      • Mabwepande
      • Magomeni
      • Makongo
      • Makumbusho
      • Mbezi Juu
      • Mbweni
      • Mikocheni
      • Msasani
      • Mwananyamala
      • Mzimuni
      • Ndugumbi
      • Tandale
      • Wazo
    • Muundo wa Taasisi
    • Ofisi ya Mtendaji wa Kata
    • Ofisi ya Mtendaji wa Mtaa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya utalii
      • Fukwe na Visiwa
      • Sehemu za kitamaduni, ngoma za asili na sanaa za mikono
    • Utalii
      • Matukio ya Utalii
      • Royal Tour Bus
  • Huduma zetu
    • Biashara
    • Huduma za Elimu
    • Ujasiriamali
    • Ushauri katika Kilimo
    • Vituo vya Ukusanyaji Mapato
    • Vibali vya Ujenzi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Uongozi
      • Mipangomiji na Mazingira
      • Maadili
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhibiti UKIMWI
    • Ratiba ya Vikao
    • Ratiba ya Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Sera
    • Makala
    • Mpango mkakati
    • Taarifa mbalimbali
    • Mkataba wa huduma kwa mteja
    • Fomu za maombi
    • Vibali vya Ujenzi Vilivyotolewa
    • Nyaraka za Elimu

KINONDONI! WEKENI MPANGO MKAKATI WA KUKUSANYA MADENI YATOKANAYO NA KODI YA ARDHI.

Tarehe iliyowekwa: October 19th, 2017

 NI AGIZO LA NAIBU WAZIRI WIZARA YA ARDHI ,NYUMBA NA MAENDELEO YA MAKAZI MH ANGELINA MABULA KATIKA KIKAO KAZI CHAKE NA WATENDAJI WA IDARA YA MIPANGOMIJI, ARDHI NA UTHAMINI MANISPAA YA KINONDONI.

 Manispaa ya Kinondoni imetakiwa kuweka mpango mkakati wa kuhakikisha inakusanya madeni yote yatokanayo na kodi ya Ardhi kwa wadaiwa sugu ili fedha hizo ziweze kutumika katika kuendeleza miradi ya Maendeleo. 

 Agizo hilo limetolewa leo na Naibu Waziri Wizara ya Ardhi Nyumba na maendeleo ya makazi Mh Angelina Mabula alipokuwa katika kikao kazi chake pamoja na watendaji kutoka Idara ya Mipangomiji, Ardhi na Uthamini kilichofanyika katika ukumbi wa Mikutano wa Manispaa. 

 Amesema ni vema ukawepo utaratibu mzuri wa kuhakikisha madeni na kodi hizi za Ardhi zinakusanywa ili fedha hizo ziweze kutumika katika kutekeleza miradi ya Maendeleo .

 "Wekeni Mapango mkakati wa kukusanya madeni, na madiwani hakikisheni mnapokaa kwenye vikao vyenu vya kila robo mmeletewa orodha ya wadaiwa waliopatiwa notisi kwa ajili ya malipo "Amesisitiza waziri .

Aidha amesema kikao kazi chake pamoja na mambo mengine ni kwa lengo la kukagua mfumo wa ukusanyaji mapato katika sekta ya Ardhi, kuangalia utendaji kazi wa mabaraza ya Ardhi pamoja na kuangalia namna ya kuendeleza maeneo yetu kupitia shirika la nyumba (NHC). 

 Naye katibu Tawala Wilaya Kinondoni Bi Gifti Msuya kwa Niaba ya Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni katika taarifa yake kwa Naibu Waziri Wizara ya Ardhi amesema idara ya Mipangomiji inazo changamoto  ambazo zikifanyiwa kazi watakuwa katika hatua nzuri ya utekelezaji 

Amezitaja changamoto hizo kuwa ni ufinyu wa nafasi katika masijala ya ardhi, matumizi ya mfumo usiokuwa wa kielektroniki katika kutoa huduma, uwepo wa madalali na mwingiliano wa utekelezaji wa majukumu baina ya Wizara na Halmashauri. 

 Nyingine ni uvamizi wa maeneo, ujenzi holela, ufinyu wa bajeti katika kutoa fidia, wananchi kuwasilisha nyaraka za kughushi pamoja na ukusanyaji kodi maeneo yasiyopimwa. 

Katika hatua nyingine Mweyekiti wa baraza la Ardhi la Kinondoni Ndg Yose Mlyambina kwenye taarifa yake kwa Naibu waziri pia ameainisha changamoto za Baraza hilo la Ardhi kuwa ni kuchelewa kwa uteuzi wa wajumbe wa baraza, mfumo wa ulipaji wa ada za Halmashauri kutokuwa rafiki, ukosefu wa miongozo, uelewa mdogo wa sheria na taratibu za mahakama kwa wananchi pamoja na kuwa na mkanganyiko wa amri za utekelezaji kutoka kwa viongozi. 

 Hii ni mara ya kwanza kwa Naibu Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi kutembelea Manispaa ya Kinondoni tangu kuteuliwa kwake kushika nyadhifa hiyo. 

 Imetolewa
 Kitengo cha Uhusiano
 Manispaa ya Kinondoni.

Matangazo

  • UTOAJI WA MIKOPO KWA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU April 01, 2025
  • TANGAZO March 22, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI October 05, 2024
  • MATOKEO YA USAILI WA VITENDO KADA YA AFISA TEHAMA MSAIDIZI ULIOFANYIKA TAREHE 25/03/2024 March 25, 2024
  • Tazama zote

Habari mpya

  • ZAIDI YA MITI 1200 YAPANDWA KUADHIMISHA MIAKA 63 YA UHURU

    December 09, 2024
  • MAAMBUKIZI UKIMWI YAPUNGUA

    December 01, 2024
  • MAAMBUKIZI YA VIRUSI VYA UKIMWI YASHUKA KINONDONI

    November 29, 2024
  • WENYEVITI NA WAJUMBE WAPYA WAPEWA MAELEKEZO YA MAJUKUMU YAO

    November 28, 2024
  • Tazama zote

Picha Jongefu

IFAHAMU KATA YA MZIMUNI, MANISPAA YA KINONDONI
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • MWONGOZO WA NAMNA YA KUTUMIA MFUMO WA TAUSI
  • UJASIRIAMALI NA UTOAJI MIKOPO
  • MAKTABA YA PICHA
  • TAARIFA KWA UMMA
  • HOTUBA
  • ORODHA YA WAHESHIMIWA MADIWANI
  • MKATABA WA HUDUMA KWA MTEJA
  • MIRADI ILIYOKAMILIKA

Viunganishi Linganifu

  • TOVUTI KUU YA IKULU
  • TOVUTI YA UTUMISHI
  • TOVUTI YA OR-TAMISEMI
  • TOVUTI YA OFISI YA TAKWIMU YA TAIFA
  • TOVUTI YA IDARA YA HABARI MAELEZO
  • TOVUTI KUU YA SERIKALI

Idadi ya Wasomaji

world map hits counter

Waliotembelea tovuti

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    2 Barabara ya Morogoro, 14883 Dar es Salaam

    Anuani ya Posta: S.L.P 31902

    Simu ya mezani: +255222170173

    Simu ya mkononi: +255733241052

    Barua pepe: md@kinondonimc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya tovuti

Hatimiliki © 2017 Halmashauri ya Manispaa ya Kinondoni. Haki Zote Zimehifadhiwa.