• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
Kinondoni Municipal Council
Kinondoni Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Kinondoni

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Maadili ya Msingi
    • Wasifu wa Halmashauri
  • Utawala
    • Divisheni
      • Miundombinu, Vijijini na Mijini
      • Huduma za Afya, Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Elimu ya Awali na Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Usimamizi wa Rasilimali Watu
    • Vitengo
      • Usimamizi wa Taka na Usafi wa Mazingira
      • Uhifadhi wa Maliasili na Mazingira
      • Michezo, Utamaduni na Sanaa
      • Fedha na Mahesabu
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Usimamizi wa Manunuzi
      • TEHAMA
      • Mawasiliano Serikalini
    • Kata
      • Bunju
      • Hananasif
      • Kawe
      • Kigogo
      • Kijitonyama
      • Kinondoni
      • Kunduchi
      • Mabwepande
      • Magomeni
      • Makongo
      • Makumbusho
      • Mbezi Juu
      • Mbweni
      • Mikocheni
      • Msasani
      • Mwananyamala
      • Mzimuni
      • Ndugumbi
      • Tandale
      • Wazo
    • Muundo wa Taasisi
    • Ofisi ya Mtendaji wa Kata
    • Ofisi ya Mtendaji wa Mtaa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya utalii
      • Fukwe na Visiwa
      • Sehemu za kitamaduni, ngoma za asili na sanaa za mikono
    • Utalii
      • Matukio ya Utalii
      • Royal Tour Bus
  • Huduma zetu
    • Biashara
    • Huduma za Elimu
    • Ujasiriamali
    • Ushauri katika Kilimo
    • Vituo vya Ukusanyaji Mapato
    • Vibali vya Ujenzi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Uongozi
      • Mipangomiji na Mazingira
      • Maadili
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhibiti UKIMWI
    • Ratiba ya Vikao
    • Ratiba ya Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Sera
    • Makala
    • Mpango mkakati
    • Taarifa mbalimbali
    • Mkataba wa huduma kwa mteja
    • Fomu za maombi
    • Vibali vya Ujenzi Vilivyotolewa
    • Nyaraka za Elimu

"DC HAPI ATOA MIFUKO 100 YA CEMENT, NA BATI 50 KWA AJILI YA UJENZI WA CHOO ENEO LA SOKO KIGOGO.

Tarehe iliyowekwa: January 6th, 2018


 NI ENEO LENYE EKARI 4.9 LILILOKUWA DAMPO YA ZAMANI LITAKALOJENGWA SOKO LA KISASA KWA AJILI YA WAFANYABIASHARA WA SOKO LA MABIBO KUHAMIA NA KUFANYA BIASHARA ZAO. 

 Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni Mh. Alli Hapi ametoa mifuko 100 ya cement na Bati 50 kwa ajili ya ujenzi wa choo eneo la kigogo kitakachotumiwa na wafanyabiashara watakaohamia kutoka mabibo na kufanya biashara zao katika eneo hilo. 

 Ahadi hiyo ameitoa Leo alipokuwa katika mkutano wa hadhara kati yake na wafanyabisahara wa mabibo  pamoja na kigogo uliofanyika katika eneo la iliyokuwa kigogo Dampo Manispaa ya Kinondoni. 

 Amesema eneo hilo kuwa soko ni kufuatia maombi ya wafanyabiashara wa soko la mabibo kuomba kupatiwa eneo la kufanya biashara baada ya kupata changamoto ya eneo walilokuwepo awali. 

 Ameongeza kuwa lengo la Serikali ni kuleta Maendeleo na kwa kugeuza eneo hilo kuwa soko ni fursa itakayoleta neema si tu kwa wananchi wa kata ya kigogo, bali kwa wananchi wa Wilaya ya Kinondoni. 

 "Tumepokea maombi ya wafanyabiashara wa soko la mabibo, kutaka kufanya biashara eneo la kigogo , maombi yenu tumeyapokea, na kwasababu sisi tunafanya kazi kwa niaba ya Rais wetu wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Dr. John Pombe Magufuli, tunaendeleza falsafa yake ya kuwaletea wanachi maendeleo, tumeyakubali maombi yenu ya kufanya biashara eneo la kigogo. "Amebainisha Hapi. 

 Naye Diwani wa kata hiyo, ambaye pia ni Naibu Meya wa Manispaa ya Kinondoni Mh. Manyama Mangalu amesema fursa hiyo ni ya neema katika kata yake na Manispaa kwa ujumla, kwani pamoja na kufanya biashara itasaidia kwa kiasi kikubwa kukuza uchumi kwa wakazi wake wa kigogo pamoja na kuiingizia Halmashauri Mapato. 

 Katika hatua nyingine DC Hapi ameitaka Manispaa hiyo kuanza kuweka mpango mkakati wa kuboresha eneo hilo  kwa misingi ya kuwa soko la kisasa, ikiwa ni pamoja na kuweka mipaka.

 Aidha ameitaka Manispaa kuhakikisha kazi ya mpango wa kujenga choo inaanza mara moja ikienda sambamba na ujenzi wa kibanda cha mlinzi. 

 Imetolewa na
 Kitengo cha Uhusiano na Habari.
 Manispaa ya Kinondoni.

Matangazo

  • UTOAJI WA MIKOPO KWA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU April 01, 2025
  • TANGAZO March 22, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI October 05, 2024
  • MATOKEO YA USAILI WA VITENDO KADA YA AFISA TEHAMA MSAIDIZI ULIOFANYIKA TAREHE 25/03/2024 March 25, 2024
  • Tazama zote

Habari mpya

  • ZAIDI YA MITI 1200 YAPANDWA KUADHIMISHA MIAKA 63 YA UHURU

    December 09, 2024
  • MAAMBUKIZI UKIMWI YAPUNGUA

    December 01, 2024
  • MAAMBUKIZI YA VIRUSI VYA UKIMWI YASHUKA KINONDONI

    November 29, 2024
  • WENYEVITI NA WAJUMBE WAPYA WAPEWA MAELEKEZO YA MAJUKUMU YAO

    November 28, 2024
  • Tazama zote

Picha Jongefu

IFAHAMU KATA YA MZIMUNI, MANISPAA YA KINONDONI
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • MWONGOZO WA NAMNA YA KUTUMIA MFUMO WA TAUSI
  • UJASIRIAMALI NA UTOAJI MIKOPO
  • MAKTABA YA PICHA
  • TAARIFA KWA UMMA
  • HOTUBA
  • ORODHA YA WAHESHIMIWA MADIWANI
  • MKATABA WA HUDUMA KWA MTEJA
  • MIRADI ILIYOKAMILIKA

Viunganishi Linganifu

  • TOVUTI KUU YA IKULU
  • TOVUTI YA UTUMISHI
  • TOVUTI YA OR-TAMISEMI
  • TOVUTI YA OFISI YA TAKWIMU YA TAIFA
  • TOVUTI YA IDARA YA HABARI MAELEZO
  • TOVUTI KUU YA SERIKALI

Idadi ya Wasomaji

world map hits counter

Waliotembelea tovuti

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    2 Barabara ya Morogoro, 14883 Dar es Salaam

    Anuani ya Posta: S.L.P 31902

    Simu ya mezani: +255222170173

    Simu ya mkononi: +255733241052

    Barua pepe: md@kinondonimc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya tovuti

Hatimiliki © 2017 Halmashauri ya Manispaa ya Kinondoni. Haki Zote Zimehifadhiwa.