Idara ina watumishi katika ngazi mbili katika utoaji wa huduma kama ifutavyo:-
Katika utoaji wa huduma kwa wadau wa Mifugo na Uvuvi ambao ni wafugaji, Maafisa Ugani wana madaftari ya wafugaji katika maeneo yao ya kazi. Aidha wataalamu wana ratiba zao za kazi ambao ni utaratibu wa kazi zao za kila siku. Ratiba hizo huwezesha kuwatembelea wafugaji wao hususani majumbani na mashambani kwa ajili ya kutoa huduma za ugani. Muda huo hutoa maelekezo, ushauri, pia kusimamia kanuni za ufugaji bora kulingana na mifugo waliyonayo.
Huduma inayotolewa na wataalamu walioko makao makuu ni masuala ya utawala. Sambamba na hilo kupokea na kutatua masuala ya utaalamu kuhusiana na mifugo na uvuvi, yanapokuwa yamekosa ufumbuzi yanapelekwa kwenye vituo vya utafiti ili kuhakikisha kwa shughuli za mifugo na uvuvi zinaendelea bila kukwama. Pindi tu utatuzi au majibu yanapopatikana yanapelekwa kwa wataalamu ngazi ya Kata ili yafikishwe kwa wafugaji ili wafanikishe shughuli zao.
Shughuli zote hizi zinafanyika chini ya Mkuu wa Idara ambaye ndiye mwenye kuratibu mambo yote na mambo mengine yanayohusu mifugo na uvuvi.
2 Barabara ya Morogoro, 14883 Dar es Salaam
Anuani ya Posta: S.L.P 31902
Simu ya mezani: +255222170173
Simu ya mkononi: +255733241052
Barua pepe: md@kinondonimc.go.tz
Hatimiliki © 2017 Halmashauri ya Manispaa ya Kinondoni. Haki Zote Zimehifadhiwa.