• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa mara |
    • Barua pepe |
Kinondoni Municipal Council
Kinondoni Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Kinondoni

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Wasifu wa Halmashauri
  • Utawala
    • Idara
      • Idara ya Utumishi
      • Afya na Usafishaji
      • Mipangomiji na Maendeleo ya Makazi
      • Kilimo na Mifugo
      • Elimu Sekondari
      • Elimu ya Awali na Msingi
      • Fedha na Biashara
      • Mipango na takwimu
      • Maendeleo ya Jamii
    • Vitengo
      • sheria
      • Manunuzi
      • Ukaguzi wa ndani
      • Tehama
    • Kata
      • Kinondoni
      • Magomeni
      • Makumbusho
      • Mwananyamala
      • Kijitonyama
      • Wazo
      • Bunju
      • Mbezi juu
      • Ndugumbi
      • Msasani
      • Kawe
      • Mzimuni
      • Mabwepande
      • Tandale
      • Kigogo
      • Mikocheni
      • Hananasif
      • Kunduchi
      • Makongo
      • Mbweni
    • Muundo wa utawala
  • Fursa za uwekezaji
  • Huduma zetu
    • Biashara
    • Elimu
    • Afya
    • Maji na Usafishaji
    • Ujasiriamali na utoaji wa mikopo
    • Ushauri katika Kilimo
    • Elimu ya ufugaji mifugo na nyuki
    • Vituo vya Ukusanyaji Mapato
  • Madiwani
    • Baraza la madiwani
    • Kamati za kudumu
    • Ratiba za vikao
    • Ratiba ya Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyopangwa kutekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Sera
    • Makala
    • Mpango mkakati
    • Taarifa mbalimbali
    • Vipeperushi
    • Mkataba wa huduma kwa mteja
    • Fomu za maombi
  • Kituo cha Habari
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Umma
    • Maktaba ya Video
    • Maktaba ya Picha

"TENGENEZENI MPANGO WA UWASILISHAJI MADA ZA AFYA ZINAZOISHI, KWENYE KILA MKUTANO WA WANANCHI UNAOFANYIKA

Posted on: August 29th, 2018

Ni agizo lake Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni Mh. Daniel Chongolo, alipokuwa akitoa maelekezo, katika kikao kazi cha Kamati ya Afya ya Msingi ya Wilaya, kilichofanyika leo kwa lengo la kupokea taarifa za utekelezaji wa shughuli za Afya, ikiwemo utekelezaji wa kampeni ya ugawaji dawa kinga na tiba kwa magonjwa ya kichocho na Minyoo ya tumbo kwa wanafunzi wa shule za awali na msingi.

Amesema mada zinazoishi kuhusiana na masuala ya magonjwa ya jumla yanayoweza kuzuilika, ni kitu ambacho mwananchi anatakiwa kukumbushwa mara kwa mara kupitia watendaji ngazi ya Kata na Mitaa kwani asilimia kubwa yanatokana na uchafu na mazalia ya mbu.

"Nitoe Rai idara ya Afya, tusisubiri dharura kwenye kushughulikia magonjwa ya mlipuko, katika vikao vyenu, ngazi za Kata,Mikutano ya wananchi, tengenezeni mpango wa uwasilishaji mada zinazoishi, mada inayoishi katika magonjwa ya jumla kama kipindupindu, kichocho, kwani haya msingi wake ni uchafu" Amebainisha Mh.Chongolo.

Awali akimkaribisha Mkuu wa Wilaya, Mganga Mkuu wa Manispaa hiyo Dr. Festo Dugange amesema, Manispaa ya Kinondoni inavyo vituo 187, vya kutolea huduma za Afya vikihusisha hospitali, zahanati, kliniki, na martenity home ambavyo, kati yake 27 ni vya Serikali, na 160, ni vya binafsi, taasisi za Serikali, na Mashirika ya kidini tunavyoshirikiana navyo katika kuboresha utoaji huduma za Afya, ikiwa ni pamoja na kushughulikia changamoto zinazojitokeza, na kuweka mikakati ya maboresho katika sekta hiyo.

Akitoa taarifa ya kampeni ya ugawaji wa dawa kinga na tiba kwa magonjwa ya kichocho na minyoo ya tumbo kwa wanafunzi wa shule za awali na Msingi, mratibu wa magonjwa yaliyokuwa hayapewi kipaumbele Dr. Neema Mlole amesema, Kinondoni imelenga kufikia wanafunzi 121,086 , wenye umri kuanzia miaka 5 hadi 14, walioandikishwa katika shule za awali na Msingi, 157, zilizopo ndani ya Kata 20 za Manispaa ya Kinondoni.

Ameongeza kuwa, katika kampeni hii, kwa kushirikiana na Wizara ya Afya maendeleo ya jamii, jinsia ,wazee na watoto kupitia kitengo cha Mpango wa magonjwa yaliyokuwa hayapewi kipaumbele imeshachukua hatua stahiki kuelekea kwenye utekelezaji ikiwemo kutoa elimu kwa wazazi na walezi, kutoa elimu kwa wagawa kinga tiba hizo watakaoshiriki zoezi, kusambaza dawa na vifaa maalumu, pamoj na mpango wa kuandaa chakula kwa wanafunzi kabla ya kuwapa kinga tiba hizo.


Katika hatua nyingine Mkuu huyo wa Wilaya, kwenye kikao hicho kilichohusisha Kamati ya Ulinzi na usalama ya Wilaya, wawakilishi wa mashirika ya dini, pamoja na wajumbe wa kamati, ameitaka idara ya Afya kuhakikisha inashughulikia maduka ya dawa muhimu, pamoja na hospitali bubu zinazoendeshwa bila vibali wala utaratibu, ili kujiepusha na madhara ya kiafya yanayoweza kutokea kwa watumiaji.


Imeandaliwa na

Kitengo cha Uhusiano na Habari.
Manispaa ya Kinondoni.





































1



Matangazo

  • TANGAZO KUHUSU VIBANDA VYA MWENGE February 22, 2021
  • TAARIFA KUHUSIANA NA WASTAAFU WANAOLIPWA NA HAZINA February 18, 2021
  • TANGAZO KUHUSU WAMILIKI WA KUMBI ZA BURUDANI, SHEREHE NA BAA January 22, 2021
  • HAWA HAPA WADAIWA SUGU WA LESENI ZA BIASHARA MANISPAA YA KINONDONI December 04, 2020
  • Tazama zote

Habari mpya

  • WATENDAJI WA KATA NA MITAA KINONDONI TIMIZENI WAJIBU WENU

    April 08, 2021
  • ZIARA YA KATA KWA KATA WILAYA YA KINONDONI YAANZA LEO

    April 01, 2021
  • MSTAHIKI MEYA MANISPAA YA KINONDONI MHE. SONGORO MNYONGE AKIFAFANUA JAMBO WAKATI WA BARAZA LA MADIWANI

    March 17, 2021
  • UWASILISHWAJI WA TAARIFA ZA KAMATI ZA KUDUMU-BARAZA LA MADIWANI.

    March 17, 2021
  • Tazama zote

Picha Jongefu

DCChongolo akemea vikali wakandarasi wazembe
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Ilala Municipal website
  • Ubungo Municipal Council
  • Kigamboni Municipal
  • Temeke Municipal

Viunganishi Linganifu

  • TAMISEMI
  • eGoverment Agency
  • Manispaa ya Kinondoni yaongoza katika Makusanyo kufikia Dec.12,2017, 2017.
  • TUME YA UTUMISHI.Tangazo la nafasi za Kazi.

Idadi ya Wasomaji

world map hits counter

Waliotembelea tovuti

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Dar es salaam, Tanzania

    Postal Address: P.O.BOX 31902 ,2Morogoro Road

    Namba za simu: +255 22 2170173

    Namba ya simu :

    Barua pepe: md@kinondonimc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Privacy Policy
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa mara
    • Ramani ya tovuti
    • Service

Hatimiliki