• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
Kinondoni Municipal Council
Kinondoni Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Kinondoni

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Maadili ya Msingi
    • Wasifu wa Halmashauri
  • Utawala
    • Divisheni
      • Miundombinu, Vijijini na Mijini
      • Huduma za Afya, Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Elimu ya Awali na Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Usimamizi wa Rasilimali Watu
    • Vitengo
      • Usimamizi wa Taka na Usafi wa Mazingira
      • Uhifadhi wa Maliasili na Mazingira
      • Michezo, Utamaduni na Sanaa
      • Fedha na Mahesabu
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Usimamizi wa Manunuzi
      • TEHAMA
      • Mawasiliano Serikalini
    • Ofisi ya Mtendaji wa Kata
    • Ofisi ya Mtendaji wa Mtaa
    • Kata
      • Bunju
      • Hananasif
      • Kawe
      • Kigogo
      • Kijitonyama
      • Kinondoni
      • Kunduchi
      • Mabwepande
      • Magomeni
      • Makongo
      • Makumbusho
      • Mbezi Juu
      • Mbweni
      • Mikocheni
      • Msasani
      • Mwananyamala
      • Mzimuni
      • Ndugumbi
      • Tandale
      • Wazo
    • Muundo wa Taasisi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Fukwe na Visiwa
    • Sehemu za kitamaduni, ngoma za asili na sanaa za mikono
    • Matukio ya Utalii
  • Huduma zetu
    • Biashara
    • Huduma za Elimu
    • Ujasiriamali
    • Ushauri katika Kilimo
    • Vituo vya Ukusanyaji Mapato
    • Vibali vya Ujenzi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Uongozi
      • Mipangomiji na Mazingira
      • Maadili
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhibiti UKIMWI
    • Ratiba ya Vikao
    • Ratiba ya Meya
  • Miradi
    • Iliyopangwa
    • Inayoendelea
    • Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Sera
    • Makala
    • Mpango mkakati
    • Taarifa mbalimbali
    • Mkataba wa huduma
    • Fomu za maombi
    • Vibali vya Ujenzi
    • Nyaraka za Elimu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video
    • Habari
    • Matukio

VITUO 292 KUTOA CHANJO YA SARATANI YA SHINGO YA KIZAZI AWAMU YA KWANZA KWA WASICHANA 5562 KINONDONI

Tarehe iliyowekwa: April 30th, 2018

Jumla ya vituo 292 vyatarajiwa kutoa huduma ya chanjo ya saratani ya mlango wa kizazi (HPV vaccine) awamu ya kwanza kwa wasichana 5,562  wenye umri wa miaka 14, katika Manispaa ya Kinondoni.

Hayo yamethibitishwa leo na Mstahiki Meya wa Manispaa hiyo Mh Benjamin Sitta, alipokuwa mgeni rasmi katika uzinduzi wa chanjo ya mlango wa kizazi uliofanyika katika kituo cha Afya Magomeni na kuhudhuriwa na viongozi wa vyama na Serikali.

Amesema kwa idadi hii ya wasichana kupata chanjo ni mwanzo mzuri na pia kutasaidia kupunguza kiasi kikubwa cha ongezeko la maambukizi ya ugonjwa huu.


"Kwa namna ya pekee, nimpongeze Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania pamoja na uongozi wake mzima, kwa kukaa na kuumiza kichwa, na kuja na jambo jema kama hili, la kuwanusuru watoto wetu wa kike kwa chanjo hii ya saratani ya mlango wa kizazi, Mungu awabariki sana "Amesisitiza Meya.

Akitoa ufafanuzi wa chanjo hiyo kwa mgeni rasmi katika taarifa iliyosomwa kwake na Sr. Edith Mboga ambaye ni mratibu wa afya ya Mama na mtoto Kinondoni amesema, idadi hiyo inajumuisha wasichana 4,581 waliopo mashuleni na 892, waliopo katika jamii.

Ameongeza kuwa uzinduzi huu utawezesha huduma kuanza kutolewa kwa kushirikiana na wadau wote,  wakiwemo wazazi, walezi, viongozi wa Serikali za mitaa, Kata Wilaya pamoja na viongozi wa dini.

Akitoa mchango wake Mganga Mkuu wa Manispaa hiyo Dr. Festo Dugange amesema virusi hivi vya HPV huambukizwa kwa njia ya kujamiiana na ndio maana chanjo hii itahusisha wasichana wa umri wa miaka 14, kwani wanasadikiwa kutokuanza kwa mambo ya kujamiana.

Aidha amewaasa wanawake kuwa na utaratibu wa kupima afya zao kwani kwa kufanya hivyo kutaepusha madhara makubwa kutokea, hasa ikizingatia ugonjwa huu wa saratani ya shingo ya kizazi dalili zake huchelewa kujulikana.

Kinondoni imejipanga kushirikiana na wadau mbalimbali wa sekta ya Afya, wakiwemo waalimu wa shule za msingi na Sekondari, ikiwa ni mkakati wa pamoja kuhakikisha uelewa unatolewa kwa wazazi, na walezi ili kuhimiza wasichana wao kupata chanjo hii.


Imeandaliwa na

Kitengo cha Uhusiano na Habari.

Manispaa ya Kinondoni.

Matangazo

  • KUFUTA TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI March 14, 2023
  • TANGAZO LA AJIRA YA MKATABA March 13, 2023
  • TANGAZO KWA WASIOLIPIA VIWANJA BOKO DOVYA (KWA SOMJI) NA SALASALA February 15, 2023
  • MABADILIKO YA SIKU YA MAFUNZO YA WASIMAMIZI WA MAUDHUI, WASIMAMIZI WA TEHAMA NA MAKARANI WA SENSA YA WATU NA MAKAZI 2022 July 28, 2022
  • Tazama zote

Habari mpya

  • JAPAN YAIPATIA MSAADA MZIMUNI SEKONDARI

    March 15, 2023
  • VIKUNDI VYAASWA MATUMIZI SAHIHI YA MIKOPO

    February 18, 2023
  • "HAKUNA TIMU KUBWA ZAIDI YA KMC FC"

    February 18, 2023
  • ULINZI NI KIPAUMBELE KINODONI-DC SAAD

    February 12, 2023
  • Tazama zote

Picha Jongefu

VIKUNDI VILIVYOSEPA NA BILIONI 11 VYAKALIWA KOONI MANISPAA YA KINONDONI. REJESHENI...
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • TARATIBU ZA KUPATA KIBALI CHA UJENZI
  • MKATABA WA HUDUMA KWA MTEJA
  • UJASIRIAMALI NA UTOAJI MIKOPO
  • VITUO VYA KUKUSANYIA MAPATO
  • ORODHA YA WAHESHIMIWA MADIWANI
  • RATIBA YA MSTAHIKI MEYA
  • TAARIFA KWA UMMA
  • MIRADI ILIYOKAMILIKA

Viunganishi Linganifu

  • TOVUTI KUU YA IKULU
  • TOVUTI YA UTUMISHI
  • TOVUTI YA OR-TAMISEMI
  • TOVUTI YA OFISI YA TAKWIMU YA TAIFA
  • TOVUTI YA IDARA YA HABARI MAELEZO
  • TOVUTI KUU YA SERIKALI

Idadi ya Wasomaji

world map hits counter

Waliotembelea tovuti

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    2 Barabara ya Morogoro, 14883 Dar es Salaam

    Anuani ya Posta: S.L.P 31902

    Simu ya mezani: +255 22 2170173

    Simu ya mkononi:

    Barua pepe: md@kinondonimc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya tovuti

Hatimiliki © 2017 Halmashauri ya Manispaa ya Kinondoni. Haki Zote Zimehifadhiwa.