• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
Kinondoni Municipal Council
Kinondoni Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Kinondoni

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Maadili ya Msingi
    • Wasifu wa Halmashauri
  • Utawala
    • Divisheni
      • Miundombinu, Vijijini na Mijini
      • Huduma za Afya, Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Elimu ya Awali na Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Usimamizi wa Rasilimali Watu
    • Vitengo
      • Usimamizi wa Taka na Usafi wa Mazingira
      • Uhifadhi wa Maliasili na Mazingira
      • Michezo, Utamaduni na Sanaa
      • Fedha na Mahesabu
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Usimamizi wa Manunuzi
      • TEHAMA
      • Mawasiliano Serikalini
    • Kata
      • Bunju
      • Hananasif
      • Kawe
      • Kigogo
      • Kijitonyama
      • Kinondoni
      • Kunduchi
      • Mabwepande
      • Magomeni
      • Makongo
      • Makumbusho
      • Mbezi Juu
      • Mbweni
      • Mikocheni
      • Msasani
      • Mwananyamala
      • Mzimuni
      • Ndugumbi
      • Tandale
      • Wazo
    • Muundo wa Taasisi
    • Ofisi ya Mtendaji wa Kata
    • Ofisi ya Mtendaji wa Mtaa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya utalii
      • Fukwe na Visiwa
      • Sehemu za kitamaduni, ngoma za asili na sanaa za mikono
    • Utalii
      • Matukio ya Utalii
      • Royal Tour Bus
  • Huduma zetu
    • Biashara
    • Huduma za Elimu
    • Ujasiriamali
    • Ushauri katika Kilimo
    • Vituo vya Ukusanyaji Mapato
    • Vibali vya Ujenzi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Uongozi
      • Mipangomiji na Mazingira
      • Maadili
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhibiti UKIMWI
    • Ratiba ya Vikao
    • Ratiba ya Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Sera
    • Makala
    • Mpango mkakati
    • Taarifa mbalimbali
    • Mkataba wa huduma kwa mteja
    • Fomu za maombi
    • Vibali vya Ujenzi Vilivyotolewa
    • Nyaraka za Elimu

TAMISEMI YAENDESHA MAFUNZO YA SIKU MOJA KWA KAMATI YA LISHE KINONDONI

Tarehe iliyowekwa: November 16th, 2018

 NI KUHUSIANA NA UANDAAJI WA MIPANGO YA HUDUMA ZA LISHE KWA MWAKA WA FEDHA 2019/2020.

 Ofisi ya Raisi -TAMISEMI kupitia kitengo cha lishe imeendesha mafunzo kwa Kamati ya lishe ya Manispaa ya Kinondoni, yahusuyo mipango ya utekelezaji wa  huduma za lishe kwa watoto umri chini ya miaka mitano, ikiwa ni pamoja na kuongeza uelewa katika swala zima la utekelezaji wake, hasa uwekaji wa vipaumbele katika bajeti ya 2019/2020.

 Akifungua mafunzo hayo ya siku moja yaliyofanyika katika ukumbi wa Mikutano wa Manispaa, kwa niaba ya Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni, Katibu Tawala wa Wilaya hiyo,  Bi Stella Msofe amesema mafunzo haya ni muhimu, na yakawe chachu ya utekelezaji wa jambo hili, hasa ikizingatiwa azma ya Serikali ni kuhakikisha inaepukana na madhara yanayoweza kutokea kwa watoto wetu pindi wanakosa lishe bora

 Naye mkufunzi kutoka ofisi ya Rais -TAMISEMI Bi.Mary Kibona, alipokuwa akiwasilisha mada  ihusianayo na mpango mkakati wa utekelezaji,amefafanua maana halisi ya  lishe kuwa ni  mchakato wa tangu chakula kinapoliwa mdomoni, kinasagwa na kuingia mwilini na kuanisha madhara ayapatayo mtoto anapokosa lishe bora kuwa ni  kupata upungufu wa madini na Vitamini mwilini.

 Akiainisha mafanikio ya Kamati ya lishe kwa Manispaa ya kinondoni tangu kuundwa kwake, Afisa lishe wa Manispaa hiyo Bi Emiliana Sumaye amesema , kamati hiyo imefanikiwa kupeleka shughuli za lishe kwa idara mtambuka, imefanikiwa kukaa vikao vitatu vya kujadiliana mwelekeo mzima wa lishe na kuainisha njia sahihi za kuhakikisha lengo linafikiwa, imefanikiwa pia kuhakikisha vituo 65 vya kutolea huduma za afya vilivyoko Manispaa vinatoa elimu ya lishe, na kufikia wazazi takribani 19,399 kwa elimu hiyo ya lishe kwa watoto na wajawazito.

 Pia ameainisha changamoto zinazowakabili kuwa ni Jamii kushindwa kutumia huduma ya uzazi kikamilifu, watoa huduma kutowajibika ipasavyo, kuwepo na  upungufu wa watoa huduma ngazi ya jamii, na watoa huduma kutopata elimu ya utoaji wa vidonge vya folic Acidi.

 Mafunzo haya yaliyohudhuriwa  pia na wawakilishi kutoka Ofisi ya Mkoa wa Dar es salaam Bi Janeth Mzava, Mwakilishi kutoka, UNICEF Bi.Joyce Ndeba, Mwenyekiti wa huduma za Uchumi Afya na Elimu Mh.Thadei Masawe, kamati ya lishe ya Manispaa,  pamoja na wakuu wa idara na vitengo, yamejadili mada zihusuzo uwasilishaji wa taarifa za utekelezaji wa shughuli za lishe.

 Nyingine ni Mpango na bajeti ya lishe kwa kutumia planrep, shughuli za lishe/afua za lishe zinazoweza kupangwa ngazi ya vituo vya afya na upatikanaji wa rasilimali watu na fedha.

 Imeandaliwa na,
 Kitengo cha Habari na Uhusiano.
 Manispaa ya Kinondoni.

Matangazo

  • UTOAJI WA MIKOPO KWA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU April 01, 2025
  • TANGAZO March 22, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI October 05, 2024
  • MATOKEO YA USAILI WA VITENDO KADA YA AFISA TEHAMA MSAIDIZI ULIOFANYIKA TAREHE 25/03/2024 March 25, 2024
  • Tazama zote

Habari mpya

  • ZAIDI YA MITI 1200 YAPANDWA KUADHIMISHA MIAKA 63 YA UHURU

    December 09, 2024
  • MAAMBUKIZI UKIMWI YAPUNGUA

    December 01, 2024
  • MAAMBUKIZI YA VIRUSI VYA UKIMWI YASHUKA KINONDONI

    November 29, 2024
  • WENYEVITI NA WAJUMBE WAPYA WAPEWA MAELEKEZO YA MAJUKUMU YAO

    November 28, 2024
  • Tazama zote

Picha Jongefu

IFAHAMU KATA YA MZIMUNI, MANISPAA YA KINONDONI
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • MWONGOZO WA NAMNA YA KUTUMIA MFUMO WA TAUSI
  • UJASIRIAMALI NA UTOAJI MIKOPO
  • MAKTABA YA PICHA
  • TAARIFA KWA UMMA
  • HOTUBA
  • ORODHA YA WAHESHIMIWA MADIWANI
  • MKATABA WA HUDUMA KWA MTEJA
  • MIRADI ILIYOKAMILIKA

Viunganishi Linganifu

  • TOVUTI KUU YA IKULU
  • TOVUTI YA UTUMISHI
  • TOVUTI YA OR-TAMISEMI
  • TOVUTI YA OFISI YA TAKWIMU YA TAIFA
  • TOVUTI YA IDARA YA HABARI MAELEZO
  • TOVUTI KUU YA SERIKALI

Idadi ya Wasomaji

world map hits counter

Waliotembelea tovuti

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    2 Barabara ya Morogoro, 14883 Dar es Salaam

    Anuani ya Posta: S.L.P 31902

    Simu ya mezani: +255222170173

    Simu ya mkononi: +255733241052

    Barua pepe: md@kinondonimc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya tovuti

Hatimiliki © 2017 Halmashauri ya Manispaa ya Kinondoni. Haki Zote Zimehifadhiwa.