• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
Kinondoni Municipal Council
Kinondoni Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Kinondoni

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Maadili ya Msingi
    • Wasifu wa Halmashauri
  • Utawala
    • Divisheni
      • Miundombinu, Vijijini na Mijini
      • Huduma za Afya, Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Elimu ya Awali na Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Usimamizi wa Rasilimali Watu
    • Vitengo
      • Usimamizi wa Taka na Usafi wa Mazingira
      • Uhifadhi wa Maliasili na Mazingira
      • Michezo, Utamaduni na Sanaa
      • Fedha na Mahesabu
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Usimamizi wa Manunuzi
      • TEHAMA
      • Mawasiliano Serikalini
    • Kata
      • Bunju
      • Hananasif
      • Kawe
      • Kigogo
      • Kijitonyama
      • Kinondoni
      • Kunduchi
      • Mabwepande
      • Magomeni
      • Makongo
      • Makumbusho
      • Mbezi Juu
      • Mbweni
      • Mikocheni
      • Msasani
      • Mwananyamala
      • Mzimuni
      • Ndugumbi
      • Tandale
      • Wazo
    • Muundo wa Taasisi
    • Ofisi ya Mtendaji wa Kata
    • Ofisi ya Mtendaji wa Mtaa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya utalii
      • Fukwe na Visiwa
      • Sehemu za kitamaduni, ngoma za asili na sanaa za mikono
    • Utalii
      • Matukio ya Utalii
      • Royal Tour Bus
  • Huduma zetu
    • Biashara
    • Huduma za Elimu
    • Ujasiriamali
    • Ushauri katika Kilimo
    • Vituo vya Ukusanyaji Mapato
    • Vibali vya Ujenzi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Uongozi
      • Mipangomiji na Mazingira
      • Maadili
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhibiti UKIMWI
    • Ratiba ya Vikao
    • Ratiba ya Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Sera
    • Makala
    • Mpango mkakati
    • Taarifa mbalimbali
    • Mkataba wa huduma kwa mteja
    • Fomu za maombi
    • Vibali vya Ujenzi Vilivyotolewa
    • Nyaraka za Elimu

KINONDONI YAZINDUA KAMATI YA MAAFA YA WILAYA.

Tarehe iliyowekwa: November 22nd, 2018

Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni Mh Daniel Chongolo leo,  amezindua kamati ya maafa ya Wilaya yenye wajumbe 29 ambapo wajumbe 18 ni kutoka timu ya Manispaa na wajumbe  11 ni wadau kutoka nje ya Halmashauri, hafla iliyofanyika katika ukumbi wa Mikutano wa Manispaa.

 Akizindua kamati hiyo, Mkuu huyo wa Wilaya katika hotuba yake amesema,  maafa ni tukio kubwa linalotokea na kuathiri utaratibu wa maisha ya jamii na kusababisha madhara makubwa kwa watu, mali, uchumi na mazingira  ambapo huzidi uwezo wa jamii kukabiliana nalo.

 Ameongeza kuwa kwa Serikali kutambua uwepo wa maafa na majanga Nchini na umuhimu wa kukabiliana nayo,  imetunga sheria ya usimamizi wa maafa namba 7 ya mwaka 2015, inayotaka uundwaji wa kamati ufanyike, kwa lengo la kuchukua hatua za kujiepusha nayo na kukabiliana pindi yanapojitokeza.

 Amesema "Kamati ninayoizindua leo ni utekelezaji wa matakwa ya Sheria, hivyo hatupo hapa kwa bahati mbaya na kamati hii inatambulika kwa mujibu wa sheria tajwa, kifungu cha 15 na 16 hivyo nendeni mkafanye kazi" Amesisitiza Chongolo.


 Awali akisoma taarifa ya uundaji wa kamati ya usimamizi wa Maafa wa Wilaya kwa niaba ya Mkurugenzi wa Manispaa,  Mratibu wa Maafa wa Manispaa hiyo Bi.Pendo Fred amewataja wajumbe wanaounda kamati kuwa ni wakuu wa idara na vitengo 16 vya Manispaa, Jeshi la zimamoto na uokozi Mkoa wa Kinondoni, TARURA, TANESCO, DART,  DAWASCO na vyombo vya habari.

 Aidha ameainisha mipango na mikakati ya kamati kwa mwaka 2018/2019 kuwa ni kufanya mkutano na wadau, kutoa mafunzo kwa kamati za maafa ndani ya Mtaa na Kata, kuanzisha program ya kutoa mafunzo katika jamii na Halmashauri kutekeleza miradi ya DMDP kwa kujenga barabara zenye mifereji.

 Naye mratibu wa timu ya wataalam ya uokoaji ya Mkoa wa Dar es Salaam (DARMAERT),  Ndg Christopher Mzava, alipokuwa akitoa taarifa yake ameyaainisha majukumu ya kamati iliyozinduliwa kuwa ni kuhuisha masuala ya dharura na maafa katika mipango ya maendeleo, kufuatilia tishio la majanga na maafa na kufanya uchunguzi wa kutokea kwa maafa na uchoraji wa ramani.

 Nyingine ni kuainisha mahitaji ya mafunzo kwa umma na kutoa elimu, kutafuta rasilimali na kusimamia operesheni za maafa na kuunda timu ya ukabilianaji wa maafa na muundo wa kulinda jamii.

 Uzinduzi wa kamati hiyo pia umehudhuriwa na wawakilishi kutoka Bank ya Dunia, msalaba mwekundu, wawakilishi kutoka ofisi ya Mkuu wa mkoa na waheshimiwa madiwani.

 Imeandaliwa na
 Kitengo cha Habari na Uhusiano.
 Manispaa ya Kinondoni.

Matangazo

  • UTOAJI WA MIKOPO KWA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU April 01, 2025
  • TANGAZO March 22, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI October 05, 2024
  • MATOKEO YA USAILI WA VITENDO KADA YA AFISA TEHAMA MSAIDIZI ULIOFANYIKA TAREHE 25/03/2024 March 25, 2024
  • Tazama zote

Habari mpya

  • ZAIDI YA MITI 1200 YAPANDWA KUADHIMISHA MIAKA 63 YA UHURU

    December 09, 2024
  • MAAMBUKIZI UKIMWI YAPUNGUA

    December 01, 2024
  • MAAMBUKIZI YA VIRUSI VYA UKIMWI YASHUKA KINONDONI

    November 29, 2024
  • WENYEVITI NA WAJUMBE WAPYA WAPEWA MAELEKEZO YA MAJUKUMU YAO

    November 28, 2024
  • Tazama zote

Picha Jongefu

IFAHAMU KATA YA MZIMUNI, MANISPAA YA KINONDONI
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • MWONGOZO WA NAMNA YA KUTUMIA MFUMO WA TAUSI
  • UJASIRIAMALI NA UTOAJI MIKOPO
  • MAKTABA YA PICHA
  • TAARIFA KWA UMMA
  • HOTUBA
  • ORODHA YA WAHESHIMIWA MADIWANI
  • MKATABA WA HUDUMA KWA MTEJA
  • MIRADI ILIYOKAMILIKA

Viunganishi Linganifu

  • TOVUTI KUU YA IKULU
  • TOVUTI YA UTUMISHI
  • TOVUTI YA OR-TAMISEMI
  • TOVUTI YA OFISI YA TAKWIMU YA TAIFA
  • TOVUTI YA IDARA YA HABARI MAELEZO
  • TOVUTI KUU YA SERIKALI

Idadi ya Wasomaji

world map hits counter

Waliotembelea tovuti

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    2 Barabara ya Morogoro, 14883 Dar es Salaam

    Anuani ya Posta: S.L.P 31902

    Simu ya mezani: +255222170173

    Simu ya mkononi: +255733241052

    Barua pepe: md@kinondonimc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya tovuti

Hatimiliki © 2017 Halmashauri ya Manispaa ya Kinondoni. Haki Zote Zimehifadhiwa.