• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
Kinondoni Municipal Council
Kinondoni Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Kinondoni

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Maadili ya Msingi
    • Wasifu wa Halmashauri
  • Utawala
    • Divisheni
      • Miundombinu, Vijijini na Mijini
      • Huduma za Afya, Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Elimu ya Awali na Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Usimamizi wa Rasilimali Watu
    • Vitengo
      • Usimamizi wa Taka na Usafi wa Mazingira
      • Uhifadhi wa Maliasili na Mazingira
      • Michezo, Utamaduni na Sanaa
      • Fedha na Mahesabu
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Usimamizi wa Manunuzi
      • TEHAMA
      • Mawasiliano Serikalini
    • Kata
      • Bunju
      • Hananasif
      • Kawe
      • Kigogo
      • Kijitonyama
      • Kinondoni
      • Kunduchi
      • Mabwepande
      • Magomeni
      • Makongo
      • Makumbusho
      • Mbezi Juu
      • Mbweni
      • Mikocheni
      • Msasani
      • Mwananyamala
      • Mzimuni
      • Ndugumbi
      • Tandale
      • Wazo
    • Muundo wa Taasisi
    • Ofisi ya Mtendaji wa Kata
    • Ofisi ya Mtendaji wa Mtaa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya utalii
      • Fukwe na Visiwa
      • Sehemu za kitamaduni, ngoma za asili na sanaa za mikono
    • Utalii
      • Matukio ya Utalii
      • Royal Tour Bus
  • Huduma zetu
    • Biashara
    • Huduma za Elimu
    • Ujasiriamali
    • Ushauri katika Kilimo
    • Vituo vya Ukusanyaji Mapato
    • Vibali vya Ujenzi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Uongozi
      • Mipangomiji na Mazingira
      • Maadili
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhibiti UKIMWI
    • Ratiba ya Vikao
    • Ratiba ya Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Sera
    • Makala
    • Mpango mkakati
    • Taarifa mbalimbali
    • Mkataba wa huduma kwa mteja
    • Fomu za maombi
    • Vibali vya Ujenzi Vilivyotolewa
    • Nyaraka za Elimu

KINONDONI YAWASHUKIA WAUZAJI WA MBWA NA PAKA KIHOLELA

Tarehe iliyowekwa: September 28th, 2020

 Kinondoni imetoa onyo kali kwa watu wanaouza wanyama jamii ya mbwa na Paka kiholela kwani kwa kufanya hivyo ni kinyume cha sheria ya ufugaji mjini.

Onyo hilo limetolewa leo na katibu Tawala wa Wilaya hiyo Bi Stella Msofe, alipokuwa mgeni rasmi katika  maadhimisho ya siku ya  kichaa Cha mbwa Duniani yenye  kaulimbiu isemayo "TOKOMEZA KICHAA CHA MBWA: TUSHIRIKIANE, KUCHANJA" na kuzindua rasmi chanjo ya ugonjwa wa kichwa cha mbwa hafla iliyofanyika katika viwanja vya Tanganyika Packer's.

Amesema sheria hairuhusu mbwa na paka kupangwa barabarani na kuuzwa, wanyama hawa Wana haki zao na kuna maeneo maalum ambayo biashara hii inatakiwa kufanyika, hivyo Wananchi wafuate sheria ili kwa pamoja tuweze kutokomeza magonjwa yanayozeza kutoka kwao wanyama na kuja kwa binaadamu ukiwemo huu wa Kichaa cha mbwa.

"Napenda kutumia maadhimisho ya siku hii kuwakumbusha wenzetu wanaoishi na mifugo majumbani mwao kufuata sheria za ufugaji mjini ili kudhibiti mbwa wanaozurura na Wananchi waache mara moja biashara ya kuuza mbwa barabarani"

 Ameongeza Bi Msofe.

Kwa upande wake Mkuu wa Idara ya mifugo na uvuvi Manispaa ya Kinondoni Bi Patricia Henjewele amesema ugonjwa wa kichwa cha mbwa unaowapata mbwa pia unawapata binaadamu, na ni vigumu kutibu binaadamu ambae anakuwa ameambukizwa ugonjwa huu hivyo ni bora zaidi kuchanja mifugo ili kuzuia kusambaa kwa ugonjwa.

 Amesema zoezi la chanjo kwa mbwa na paka ambalo limezinduliwa leo, litakuwa endelevu kwa kipindi cha mwezi mzima katika kata mbalimbali zilizopo wilaya ya Kinondoni hivyo Wananchi wawasiliane na Maafisa mifugo wa kata husika.

Aidha amewashukuru Taasisi ya Every living Things inayojihusisha na haki za wanyama hususani wanyama wanaozurura mitaani kwa kushirikiana na Manispaa ya Kinondoni kutokomeza ugonjwa wa Kichaa cha Mbwa.

Siku ya kichaa cha mbwa duniani huadhimishwa kila ifikapo Tar 28 mwezi Septemba ambapo kwa Kinondoni wameadhimisha kwa kutoa chanjo kwa mbwa na paka dhidi ya ugonjwa wa kichaa cha mbwa, Kutibu wanyama watakaogundulika na magonjwa ya aina mbalimbali, Kuogesha wanyama kwa lengo la kuua kupe na viroboto na kukata kucha zilizodidi.

Imeandaliwa na

 Kitengo cha Habari na Uhusiano

Manispaa ya Kinondoni.

Matangazo

  • UTOAJI WA MIKOPO KWA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU April 01, 2025
  • TANGAZO March 22, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI October 05, 2024
  • MATOKEO YA USAILI WA VITENDO KADA YA AFISA TEHAMA MSAIDIZI ULIOFANYIKA TAREHE 25/03/2024 March 25, 2024
  • Tazama zote

Habari mpya

  • ZAIDI YA MITI 1200 YAPANDWA KUADHIMISHA MIAKA 63 YA UHURU

    December 09, 2024
  • MAAMBUKIZI UKIMWI YAPUNGUA

    December 01, 2024
  • MAAMBUKIZI YA VIRUSI VYA UKIMWI YASHUKA KINONDONI

    November 29, 2024
  • WENYEVITI NA WAJUMBE WAPYA WAPEWA MAELEKEZO YA MAJUKUMU YAO

    November 28, 2024
  • Tazama zote

Picha Jongefu

IFAHAMU KATA YA MZIMUNI, MANISPAA YA KINONDONI
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • MWONGOZO WA NAMNA YA KUTUMIA MFUMO WA TAUSI
  • UJASIRIAMALI NA UTOAJI MIKOPO
  • MAKTABA YA PICHA
  • TAARIFA KWA UMMA
  • HOTUBA
  • ORODHA YA WAHESHIMIWA MADIWANI
  • MKATABA WA HUDUMA KWA MTEJA
  • MIRADI ILIYOKAMILIKA

Viunganishi Linganifu

  • TOVUTI KUU YA IKULU
  • TOVUTI YA UTUMISHI
  • TOVUTI YA OR-TAMISEMI
  • TOVUTI YA OFISI YA TAKWIMU YA TAIFA
  • TOVUTI YA IDARA YA HABARI MAELEZO
  • TOVUTI KUU YA SERIKALI

Idadi ya Wasomaji

world map hits counter

Waliotembelea tovuti

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    2 Barabara ya Morogoro, 14883 Dar es Salaam

    Anuani ya Posta: S.L.P 31902

    Simu ya mezani: +255222170173

    Simu ya mkononi: +255733241052

    Barua pepe: md@kinondonimc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya tovuti

Hatimiliki © 2017 Halmashauri ya Manispaa ya Kinondoni. Haki Zote Zimehifadhiwa.