• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
Kinondoni Municipal Council
Kinondoni Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Kinondoni

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Maadili ya Msingi
    • Wasifu wa Halmashauri
  • Utawala
    • Divisheni
      • Miundombinu, Vijijini na Mijini
      • Huduma za Afya, Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Elimu ya Awali na Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Usimamizi wa Rasilimali Watu
    • Vitengo
      • Usimamizi wa Taka na Usafi wa Mazingira
      • Uhifadhi wa Maliasili na Mazingira
      • Michezo, Utamaduni na Sanaa
      • Fedha na Mahesabu
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Usimamizi wa Manunuzi
      • TEHAMA
      • Mawasiliano Serikalini
    • Kata
      • Bunju
      • Hananasif
      • Kawe
      • Kigogo
      • Kijitonyama
      • Kinondoni
      • Kunduchi
      • Mabwepande
      • Magomeni
      • Makongo
      • Makumbusho
      • Mbezi Juu
      • Mbweni
      • Mikocheni
      • Msasani
      • Mwananyamala
      • Mzimuni
      • Ndugumbi
      • Tandale
      • Wazo
    • Muundo wa Taasisi
    • Ofisi ya Mtendaji wa Kata
    • Ofisi ya Mtendaji wa Mtaa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya utalii
      • Fukwe na Visiwa
      • Sehemu za kitamaduni, ngoma za asili na sanaa za mikono
    • Utalii
      • Matukio ya Utalii
      • Royal Tour Bus
  • Huduma zetu
    • Biashara
    • Huduma za Elimu
    • Ujasiriamali
    • Ushauri katika Kilimo
    • Vituo vya Ukusanyaji Mapato
    • Vibali vya Ujenzi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Uongozi
      • Mipangomiji na Mazingira
      • Maadili
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhibiti UKIMWI
    • Ratiba ya Vikao
    • Ratiba ya Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Sera
    • Makala
    • Mpango mkakati
    • Taarifa mbalimbali
    • Mkataba wa huduma kwa mteja
    • Fomu za maombi
    • Vibali vya Ujenzi Vilivyotolewa
    • Nyaraka za Elimu

KINONDONI YAENDESHA MAFUNZO KWA WATENDAJI WA KATA NA MITAA

Tarehe iliyowekwa: February 23rd, 2022

Manispaa ya Kinondoni imeandaa mafunzo ya siku moja kwa Watendaji wa Kata na Mitaa yenye lengo la kuwawezesha kutekeleza jukumu la msingi la utambuzi wa maeneo pamoja na barabara ili zoezi la anwani za makazi liweze kukamilika kwa wakati na ufanisi.

Akifungua semina hiyo ya siku moja kwa Watendaji hao Kaimu Mkurugenzi wa Manispaa hiyo Bw. Salum Yusuph amesema Watendaji wa Kata na Mitaa ndio watu muhimu katika kufanikisha azma nzima hasa ikizingatiwa utekelezaji wa majukumu yao unagusa wananchi moja kwa moja.

"Ninyi Watendaji mnaotekeleza majukumu yenu kwenye Kata na Mitaa, huko ndio mnaojua eneo hili ni lipi na barabara hii ni ya wapi, ndio mnaotekeleza majukumu yanayogusa wananchi moja kwa moja, hivyo kwa zoezi hili bila nguvu yenu, uwajibikaji wenu, ufanisi wake utakuwa mgumu. Niwaombe mshiriki uwezeshaji huu wa siku moja kwa ufanisi ili tuweze kwenda sawa kufikia lengo kusudiwa".  Amesema Salum Yusuph.

Aidha Kaimu Mkurugenzi huyo pia amezitaja faida zitakazopatikana baada ya kukamilika kwa zoezi zima la anwani za makazi kuwa ni kurahisisha zoezi la sensa linalotarajiwa kuanza mwezi wa nane, litarahisisha upatikanaji wa huduma, litasaidia katika ukuaji wa uchumi, ulinzi na usalama wa mtu binafsi na Taifa, litatoa mwelekeo wa upatikanaji wa fursa mbalimbali na kusaidia utambuzi wa nyumba na idadi ya wakazi wa eneo husika.

Alpokuwa akitambulisha mada zilizoandaliwa kwa Watendaji hao wa Kata na Mitaa, Mwenyekti wa Kamati hiyo ambaye pia ni Afisa Ardhi Mteule Ndg. Geofrey Mwamsojo amesema mafunzo haya yatarahisisha utekelezaji wa zoezi hili na kuwataka watendaji hao kuzingatia ili waweze kukabiliana na kikwazo chochote katika ukamilishaji wake.

Mada zilizofundishwa ni pamoja na mwongozo wa mfumo wa anwani za makazi,  ukusanyaji wa taarifa, manufaa ya mfumo wa anwani, majukumu ya kila mmoja, pamoja na utoaji na upatikanaji wa taarifa.

Mafunzo haya ya siku moja yamehusisha Watendaji wa Kata zote 20 na Mitaa 106.


Imeandaliwa na

Kitengo Cha Habari na Uhusiano.

Manispaa ya Kinondoni.


Matangazo

  • UTOAJI WA MIKOPO KWA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU April 01, 2025
  • TANGAZO March 22, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI October 05, 2024
  • MATOKEO YA USAILI WA VITENDO KADA YA AFISA TEHAMA MSAIDIZI ULIOFANYIKA TAREHE 25/03/2024 March 25, 2024
  • Tazama zote

Habari mpya

  • ZAIDI YA MITI 1200 YAPANDWA KUADHIMISHA MIAKA 63 YA UHURU

    December 09, 2024
  • MAAMBUKIZI UKIMWI YAPUNGUA

    December 01, 2024
  • MAAMBUKIZI YA VIRUSI VYA UKIMWI YASHUKA KINONDONI

    November 29, 2024
  • WENYEVITI NA WAJUMBE WAPYA WAPEWA MAELEKEZO YA MAJUKUMU YAO

    November 28, 2024
  • Tazama zote

Picha Jongefu

IFAHAMU KATA YA MZIMUNI, MANISPAA YA KINONDONI
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • MWONGOZO WA NAMNA YA KUTUMIA MFUMO WA TAUSI
  • UJASIRIAMALI NA UTOAJI MIKOPO
  • MAKTABA YA PICHA
  • TAARIFA KWA UMMA
  • HOTUBA
  • ORODHA YA WAHESHIMIWA MADIWANI
  • MKATABA WA HUDUMA KWA MTEJA
  • MIRADI ILIYOKAMILIKA

Viunganishi Linganifu

  • TOVUTI KUU YA IKULU
  • TOVUTI YA UTUMISHI
  • TOVUTI YA OR-TAMISEMI
  • TOVUTI YA OFISI YA TAKWIMU YA TAIFA
  • TOVUTI YA IDARA YA HABARI MAELEZO
  • TOVUTI KUU YA SERIKALI

Idadi ya Wasomaji

world map hits counter

Waliotembelea tovuti

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    2 Barabara ya Morogoro, 14883 Dar es Salaam

    Anuani ya Posta: S.L.P 31902

    Simu ya mezani: +255222170173

    Simu ya mkononi: +255733241052

    Barua pepe: md@kinondonimc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya tovuti

Hatimiliki © 2017 Halmashauri ya Manispaa ya Kinondoni. Haki Zote Zimehifadhiwa.