• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
Kinondoni Municipal Council
Kinondoni Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Kinondoni

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Maadili ya Msingi
    • Wasifu wa Halmashauri
  • Utawala
    • Divisheni
      • Miundombinu, Vijijini na Mijini
      • Huduma za Afya, Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Elimu ya Awali na Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Usimamizi wa Rasilimali Watu
    • Vitengo
      • Usimamizi wa Taka na Usafi wa Mazingira
      • Uhifadhi wa Maliasili na Mazingira
      • Michezo, Utamaduni na Sanaa
      • Fedha na Mahesabu
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Usimamizi wa Manunuzi
      • TEHAMA
      • Mawasiliano Serikalini
    • Kata
      • Bunju
      • Hananasif
      • Kawe
      • Kigogo
      • Kijitonyama
      • Kinondoni
      • Kunduchi
      • Mabwepande
      • Magomeni
      • Makongo
      • Makumbusho
      • Mbezi Juu
      • Mbweni
      • Mikocheni
      • Msasani
      • Mwananyamala
      • Mzimuni
      • Ndugumbi
      • Tandale
      • Wazo
    • Muundo wa Taasisi
    • Ofisi ya Mtendaji wa Kata
    • Ofisi ya Mtendaji wa Mtaa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya utalii
      • Fukwe na Visiwa
      • Sehemu za kitamaduni, ngoma za asili na sanaa za mikono
    • Utalii
      • Matukio ya Utalii
      • Royal Tour Bus
  • Huduma zetu
    • Biashara
    • Huduma za Elimu
    • Ujasiriamali
    • Ushauri katika Kilimo
    • Vituo vya Ukusanyaji Mapato
    • Vibali vya Ujenzi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Uongozi
      • Mipangomiji na Mazingira
      • Maadili
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhibiti UKIMWI
    • Ratiba ya Vikao
    • Ratiba ya Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Sera
    • Makala
    • Mpango mkakati
    • Taarifa mbalimbali
    • Mkataba wa huduma kwa mteja
    • Fomu za maombi
    • Vibali vya Ujenzi Vilivyotolewa
    • Nyaraka za Elimu

KINONDONI KUBORESHA MBINU ZA UFUNDISHAJI

Tarehe iliyowekwa: August 24th, 2022

Katika kuongeza mikakati ya kuinua elimu, Manispaa ya Kinondoni jijini Dar es Salaam, inatarajia kuanza kufundisha wanafunzi kwa njia ya mtandao ili kuwawezesha kujifunza kwa wepesi zaidi.

Hayo yamesemwa na Mkurugenzi wa Manispaa ya Kinondoni, Bi. Hanifa Suleiman Hamza, alipotoa ufafanuzi wa swali la Mheshimiwa Manfred Lyoto, Diwani wa Kata ya Mzimuni. 

Diwani huyo alitaka kufahamu mikakati ya uboreshaji elimu ndani ya Manispaa wakati wa kikao cha Baraza la Madiwani lililoketi Agosti 24,2022 katika ukumbi wa Manispaa hiyo.

Mkurugenzi huyo alilielezea Baraza hilo kuwa, ni kweli kuwa siku zote walimu hawatoshi kutokana na kuwa shule na madarasa yamekuwa yakiongezeka kulingana na mahitaji ambapo hata hivyo Serikali imekuwa ikifanya jitihada za kuleta walimu. 

Alieleza kuwa mkakati wa Manispaa kwa sasa ni kujielekeza kutumia mapato ya ndani kuajiri walimu wa mkataba ili kupunguza nakisi ya walimu.

Aidha alieleza kuwa mwaka jana mwezi Aprili Manispaa ilifanya majaribio ya mfumo wa elimu mtandao ‘visual learning’ kwa kutumia ubao janja ‘smart screen’ katika kufundisha wanafunzi. Kwamba mwalimu atakaa shule moja ambayo itaunganishwa na shule nyingine. 

Alilieza Baraza hilo kuwa majaribio hayo yalifanikiwa na kwamba, kwa sasa Manispaa inaendelea kutafuta vifaa vikiwemo ubao janja 'smart screen' zitakazowawezesha wanafunzi kuona kinachofundishwa katika shule nyingine za sekondari haswa katika masomo ya sayansi.

Mkurugenzi aliongeza kuwa ameshatoa maelekezo kwa Afisa Elimu kuandaa bajeti ya kununua smartboards na kuzungumza na watoa huduma za mitandao. “Nishukuru kwamba Afisa Elimu sekondari ametenga kiasi cha shilingi milioni 16 kwa ajili ya ununuzi wa smartboards ambayo smartboard moja inagharimu shilingi milioni Tano.” Aliongeza kuwa, “kwa sasa mchakato unaendelea wa kumtafuta mzabuni wa kuleta smartboards hizo.”

Naye Mstahiki Meya wa Manispaa ya Kinondoni, Mheshimiwa Songoro Mnyonge, aliongeza kuwa, “tunaanza na kiasi hicho cha shilingi Milioni 16, lakini lengo ni kwamba katika bajeti ya mwaka wa fedha ujao ama katika marejeo ya bajeti ya mwaka huu mwezi Desemba, uhitaji ukiwepo tutaongeza fedha ili tuweze kuzitawanya katika shule zetu nyingi za Sekondari”

Aidha, Mkurugenzi huyo pamoja na kueleza kuwa wataendelea kuomba walimu OR-TAMISEMI, pia aliwaomba Waheshimiwa Madiwani hao kuwa kwa vile wao ni wadau wa maendeleo wahakikishe panakuwepo na kumbi za kufundishia wanafunzi hao. 

Kikao hicho cha Baraza kimekutana kwa ajili ya kujadili taarifa za robo ya nne (Aprili hadi Juni) ya mwaka wa fedha 2021/2022.

Matangazo

  • UTOAJI WA MIKOPO KWA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU April 01, 2025
  • TANGAZO March 22, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI October 05, 2024
  • MATOKEO YA USAILI WA VITENDO KADA YA AFISA TEHAMA MSAIDIZI ULIOFANYIKA TAREHE 25/03/2024 March 25, 2024
  • Tazama zote

Habari mpya

  • ZAIDI YA MITI 1200 YAPANDWA KUADHIMISHA MIAKA 63 YA UHURU

    December 09, 2024
  • MAAMBUKIZI UKIMWI YAPUNGUA

    December 01, 2024
  • MAAMBUKIZI YA VIRUSI VYA UKIMWI YASHUKA KINONDONI

    November 29, 2024
  • WENYEVITI NA WAJUMBE WAPYA WAPEWA MAELEKEZO YA MAJUKUMU YAO

    November 28, 2024
  • Tazama zote

Picha Jongefu

IFAHAMU KATA YA MZIMUNI, MANISPAA YA KINONDONI
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • MWONGOZO WA NAMNA YA KUTUMIA MFUMO WA TAUSI
  • UJASIRIAMALI NA UTOAJI MIKOPO
  • MAKTABA YA PICHA
  • TAARIFA KWA UMMA
  • HOTUBA
  • ORODHA YA WAHESHIMIWA MADIWANI
  • MKATABA WA HUDUMA KWA MTEJA
  • MIRADI ILIYOKAMILIKA

Viunganishi Linganifu

  • TOVUTI KUU YA IKULU
  • TOVUTI YA UTUMISHI
  • TOVUTI YA OR-TAMISEMI
  • TOVUTI YA OFISI YA TAKWIMU YA TAIFA
  • TOVUTI YA IDARA YA HABARI MAELEZO
  • TOVUTI KUU YA SERIKALI

Idadi ya Wasomaji

world map hits counter

Waliotembelea tovuti

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    2 Barabara ya Morogoro, 14883 Dar es Salaam

    Anuani ya Posta: S.L.P 31902

    Simu ya mezani: +255222170173

    Simu ya mkononi: +255733241052

    Barua pepe: md@kinondonimc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya tovuti

Hatimiliki © 2017 Halmashauri ya Manispaa ya Kinondoni. Haki Zote Zimehifadhiwa.