• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
Kinondoni Municipal Council
Kinondoni Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Kinondoni

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Maadili ya Msingi
    • Wasifu wa Halmashauri
  • Utawala
    • Divisheni
      • Miundombinu, Vijijini na Mijini
      • Huduma za Afya, Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Elimu ya Awali na Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Usimamizi wa Rasilimali Watu
    • Vitengo
      • Usimamizi wa Taka na Usafi wa Mazingira
      • Uhifadhi wa Maliasili na Mazingira
      • Michezo, Utamaduni na Sanaa
      • Fedha na Mahesabu
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Usimamizi wa Manunuzi
      • TEHAMA
      • Mawasiliano Serikalini
    • Ofisi ya Mtendaji wa Kata
    • Ofisi ya Mtendaji wa Mtaa
    • Kata
      • Bunju
      • Hananasif
      • Kawe
      • Kigogo
      • Kijitonyama
      • Kinondoni
      • Kunduchi
      • Mabwepande
      • Magomeni
      • Makongo
      • Makumbusho
      • Mbezi Juu
      • Mbweni
      • Mikocheni
      • Msasani
      • Mwananyamala
      • Mzimuni
      • Ndugumbi
      • Tandale
      • Wazo
    • Muundo wa Taasisi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Fukwe na Visiwa
    • Sehemu za kitamaduni, ngoma za asili na sanaa za mikono
    • Matukio ya Utalii
  • Huduma zetu
    • Biashara
    • Huduma za Elimu
    • Ujasiriamali
    • Ushauri katika Kilimo
    • Vituo vya Ukusanyaji Mapato
    • Vibali vya Ujenzi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Uongozi
      • Mipangomiji na Mazingira
      • Maadili
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhibiti UKIMWI
    • Ratiba ya Vikao
    • Ratiba ya Meya
  • Miradi
    • Iliyopangwa
    • Inayoendelea
    • Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Sera
    • Makala
    • Mpango mkakati
    • Taarifa mbalimbali
    • Mkataba wa huduma
    • Fomu za maombi
    • Vibali vya Ujenzi
    • Nyaraka za Elimu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video
    • Habari
    • Matukio

DC CHONGOLO ASIMAMA KIDETE NA WANAOZURUMU NYUMBA , ATOA ONYO KALI KWA WAHUSIKA, BI SHARIFA ARUDISHIWA NYUMBA YAKE

Tarehe iliyowekwa: November 11th, 2019

Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni, Mhe. Daniel Chongolo amesimamia haki na hivyo kuwezesha kurudishwa kwa  Nyumba ya mkazi wa Magomeni Mzimuni,Bi  Sharifa Mbaruku aliyenyang’anywa kwa muda wa miaka mitatu iliyopita.

Mhe. Chongolo alichukua maamuzi hayo leo alipofika kwenye nyumba ya Bi Sharifa ikiwa ni baada ya bibi huyo kupeleka malalamiko ya kudai kuzurumiwa na Bi Magrethi ambaye kwa sasa inadaiwa kuwa anaishi nje ya Nchi.

Akizungumza na wandishi wa habari mara baada ya kufika katika nyumba hiyo ,Mhe. Chongolo amesema kuwa aliyemuondoa kwenye nyumba hiyo mwaka 2016 alifanya makosa na kwamba hakuwa na haki ya kumiliki nyumba hiyo.

Amefafanua kuwa kazi ya serikali ya awamu ya tano ni kutetea wanyonge wanaozurumiwa haki zao na kwamba akiwa Mkuu wa Wilaya hiyo amerudisha umiliki wa nyumba hiyo kwa mhusika ambaye ni Bi Sharifa.

 “kuanzia hivi ninavyozungumza unarudi kwenye nyumba yako rasmi, wewe ndio mmiliki wa nyumba hii, kwahiyo nendeni mkaondoe mabati yote ambayo yamezungushiwa na sisi kama serikali tutawachukulia hatua wote waliohusika na mchezo huu" Amesisitiza Mhe Chongolo

Katika hatua nyingine Mhe. Chongolo ametoa agizo na kuwataka wote wenye tabia ya kupora nyumba za watu hasa masikini na wanyonge kuacha mara moja kwani hatamuonea haya mtu yeyote aliyekuwa kwenye manispaa yake.

Kwaupande wake Bi Sharifa aliyezurumiwa nyumba hiyo,  amesema kuwa Disemba 27 mwaka 2016 akiwa amelala ilikuja gari ya polisi wakiwa na diwani wa Kata ya Magomeni wakati huo Ally Kondo pamoja na Kuruthumu Ramadhani walimtolea vitu nje na kumtaka kuondoka katika nyumba hiyo bila kutoa maelezo yoyote.

 “ Mhe. Mkuu wa Wilaya nakupongeza sana baba kwakutujali masikini, mungu akubariki na akupe maisha marefu , hata Mahakama pia inachangia kwakuwa awali ilikuja toleo la kwanza  lilionyesha 159 Block four, toleo la pili 159 Block eigth, toleo la tatu halikuwa na namba ya nyumba kwakweli huu ni uonevu” amesisitiza Bi Sharifa.

 

Imetolewa na

Kitengo cha Habari na Uhusiano

Manispaa ya Kinondoni    


ReplyForward

Matangazo

  • KUFUTA TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI March 14, 2023
  • TANGAZO LA AJIRA YA MKATABA March 13, 2023
  • TANGAZO KWA WASIOLIPIA VIWANJA BOKO DOVYA (KWA SOMJI) NA SALASALA February 15, 2023
  • MABADILIKO YA SIKU YA MAFUNZO YA WASIMAMIZI WA MAUDHUI, WASIMAMIZI WA TEHAMA NA MAKARANI WA SENSA YA WATU NA MAKAZI 2022 July 28, 2022
  • Tazama zote

Habari mpya

  • JAPAN YAIPATIA MSAADA MZIMUNI SEKONDARI

    March 15, 2023
  • VIKUNDI VYAASWA MATUMIZI SAHIHI YA MIKOPO

    February 18, 2023
  • "HAKUNA TIMU KUBWA ZAIDI YA KMC FC"

    February 18, 2023
  • ULINZI NI KIPAUMBELE KINODONI-DC SAAD

    February 12, 2023
  • Tazama zote

Picha Jongefu

VIKUNDI VILIVYOSEPA NA BILIONI 11 VYAKALIWA KOONI MANISPAA YA KINONDONI. REJESHENI...
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • TARATIBU ZA KUPATA KIBALI CHA UJENZI
  • MKATABA WA HUDUMA KWA MTEJA
  • UJASIRIAMALI NA UTOAJI MIKOPO
  • VITUO VYA KUKUSANYIA MAPATO
  • ORODHA YA WAHESHIMIWA MADIWANI
  • RATIBA YA MSTAHIKI MEYA
  • TAARIFA KWA UMMA
  • MIRADI ILIYOKAMILIKA

Viunganishi Linganifu

  • TOVUTI KUU YA IKULU
  • TOVUTI YA UTUMISHI
  • TOVUTI YA OR-TAMISEMI
  • TOVUTI YA OFISI YA TAKWIMU YA TAIFA
  • TOVUTI YA IDARA YA HABARI MAELEZO
  • TOVUTI KUU YA SERIKALI

Idadi ya Wasomaji

world map hits counter

Waliotembelea tovuti

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    2 Barabara ya Morogoro, 14883 Dar es Salaam

    Anuani ya Posta: S.L.P 31902

    Simu ya mezani: +255 22 2170173

    Simu ya mkononi:

    Barua pepe: md@kinondonimc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya tovuti

Hatimiliki © 2017 Halmashauri ya Manispaa ya Kinondoni. Haki Zote Zimehifadhiwa.