• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa mara |
    • Barua pepe |
Kinondoni Municipal Council
Kinondoni Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Kinondoni

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Wasifu wa Halmashauri
  • Utawala
    • Idara
      • Idara ya Utumishi
      • Afya na Usafishaji
      • Mipangomiji na Maendeleo ya Makazi
      • Kilimo na Mifugo
      • Elimu Sekondari
      • Elimu ya Awali na Msingi
      • Fedha na Biashara
      • Mipango na takwimu
      • Maendeleo ya Jamii
    • Vitengo
      • sheria
      • Manunuzi
      • Ukaguzi wa ndani
      • Tehama
    • Kata
      • Kinondoni
      • Magomeni
      • Makumbusho
      • Mwananyamala
      • Kijitonyama
      • Wazo
      • Bunju
      • Mbezi juu
      • Ndugumbi
      • Msasani
      • Kawe
      • Mzimuni
      • Mabwepande
      • Tandale
      • Kigogo
      • Mikocheni
      • Hananasif
      • Kunduchi
      • Makongo
      • Mbweni
    • Muundo wa utawala
  • Fursa za uwekezaji
  • Huduma zetu
    • Biashara
    • Elimu
    • Afya
    • Maji na Usafishaji
    • Ujasiriamali na utoaji wa mikopo
    • Ushauri katika Kilimo
    • Elimu ya ufugaji mifugo na nyuki
    • Vituo vya Ukusanyaji Mapato
  • Madiwani
    • Baraza la madiwani
    • Kamati za kudumu
    • Ratiba za vikao
    • Ratiba ya Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyopangwa kutekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Sera
    • Makala
    • Mpango mkakati
    • Taarifa mbalimbali
    • Vipeperushi
    • Mkataba wa huduma kwa mteja
    • Fomu za maombi
  • Kituo cha Habari
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Umma
    • Maktaba ya Video
    • Maktaba ya Picha

KUELEKEA NANE NANE : BANDA LA KINONDONI LASHANGAZ WENGI.USIPITWE NA WEWE.

Posted on: August 3rd, 2017


 NI KUHUSIANA NA UTAALAMU ADIMU NA WA KISASA WA JINSI YA? KUZALISHA MALISHO YA HYDROPHONIC .

 Kuelekea kilele cha Nane nane Mkoani Morogoro Manispaa ya Kinondoni imejipanga vema katika maswala ya Ufugaji. 

 Leo inakuletea Technolojia ya kitu kinaitwa Hydrophonic Fodder. 

 Technolojia hii ya Hydrophonic fodder ni mbinu ya kukuza mimea kwa kutumia mchanganyiko wa vurutubisho vya madini katika maji bila kutumia udongo. 

 Mchakato huu huchukua muda wa siku 5-7 kukamilika. Unachotakiwa kufanya ni kuchukua Kilo moja ya mbegu za ngano au mtama au shayiri au mahindi na kuziotesha kisha kumwagiliwa virutubisho maalum(Hydrophonic Nutrients). 

 FAIDA ZA CHAKULA CHA HYDROPHONIC FODDER KWA MIFUGO. 

 Ni nafuu sana ukilinganisha na gharama za chakula cha madukani. 

 Kina virutubisho na vitàmini mara 3 zaidi ya chakula cha kawaida. 

 Hupunguza magonjwa ya mfumo wa hewa kama vile mafua kwa mifugo na mfugaji kwani hakina vumbi. 

 Kina Protein ya kutosha, chakula chake ni laini, mifugo hukua kwa haraka Sana na hupunguza gharama za ufugaji kwenye manunuzi ya chakula kwa asilimia 50-75.

 HATUA KATIKA KUZALISHA HYDROPHONIC.
 Mfugaji anaweza kuzalisha malisho yake mwenyewe nyumbani. Mambo muhimu ya kufuata ni haya hapa :

 Chagua mbegu ambazo hazijaanza kuchipua, na hazina kemikali ama dawa ya aina yeyote. 

 Loweka mbegu katika mchanganyiko wa maji na chlorine kwa masaa mawili kuepusha kuvunda, ama vimelea vya magonjwa kumea na kukua kwenye malisho. 

 Zitoe mbegu kwenye maji, kisha zioshe, ziloweke kwenye maji safi kwa masaa 24 kuwezesha mbegu kufyonza maji vema. 

 Katika kupanda mbegu, pima  kilo mbili za mbegu kwa kila trei yenye urefu wa cm 80 kwa upana wa cm 40.

 Sambaza mbegu kwenye trei kwa usawa, (zisizidi cm 3kimo)  ili kuwe na nafasi ya kutosha kwa kila mbegu kuchipua. 

 Hakikisha trei zinamatundu kwenye kitako(chini) ambayo yamesambaa kwa usawa kuwezesha maji ya ziada kutoka. 

 Hamishia trei kwenye chanja ulizotengeneza. Mbegu zitaanza kuota katika hatua hii. Fanya hii ni siku ya kwanza. 

 JINSI YA KULISHA. 

 KUKU: kwa kuku 100 wanaotaga (Layer) wape kilo 8 za hydrophonic na waongezee kilo 4 za chakula cha layer.(Layer Mash) kwa siku. 

 Nguruwe: Katika unenepeshaji wake kilo 2 za hydrophonic na 1.5 za chakula kikavu (Nafaka)  kwa nguruwe mmoja kwa siku. 

 Ngombe, Mbuzi :wanaweza kutegemea majani haya tu na kuwa na uzalishaji mzuri bila nyongeza ya mchanganyiko wa nafaka.

 Sungura :wanaweza kutegemea majani haya tu lakini ni vema kuwapa nyongeza ya mchanganyiko. 

 Kwa elimu zaidi juu ya technolojia ya Hydrophonic, usikose kutembelea banda la Manispaa ya Kinondoni ukutane na wataalamu wa Mifugo wapate kukujuza mengi zaidi. 

 Imetolewa na
 Kitengo cha Uhusiano
 Manispaa ya Kinondoni.

Matangazo

  • TANGAZO KUHUSU VIBANDA VYA MWENGE February 22, 2021
  • TAARIFA KUHUSIANA NA WASTAAFU WANAOLIPWA NA HAZINA February 18, 2021
  • TANGAZO KUHUSU WAMILIKI WA KUMBI ZA BURUDANI, SHEREHE NA BAA January 22, 2021
  • HAWA HAPA WADAIWA SUGU WA LESENI ZA BIASHARA MANISPAA YA KINONDONI December 04, 2020
  • Tazama zote

Habari mpya

  • WATENDAJI WA KATA NA MITAA KINONDONI TIMIZENI WAJIBU WENU

    April 08, 2021
  • ZIARA YA KATA KWA KATA WILAYA YA KINONDONI YAANZA LEO

    April 01, 2021
  • MSTAHIKI MEYA MANISPAA YA KINONDONI MHE. SONGORO MNYONGE AKIFAFANUA JAMBO WAKATI WA BARAZA LA MADIWANI

    March 17, 2021
  • UWASILISHWAJI WA TAARIFA ZA KAMATI ZA KUDUMU-BARAZA LA MADIWANI.

    March 17, 2021
  • Tazama zote

Picha Jongefu

DCChongolo akemea vikali wakandarasi wazembe
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Ilala Municipal website
  • Ubungo Municipal Council
  • Kigamboni Municipal
  • Temeke Municipal

Viunganishi Linganifu

  • TAMISEMI
  • eGoverment Agency
  • Manispaa ya Kinondoni yaongoza katika Makusanyo kufikia Dec.12,2017, 2017.
  • TUME YA UTUMISHI.Tangazo la nafasi za Kazi.

Idadi ya Wasomaji

world map hits counter

Waliotembelea tovuti

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Dar es salaam, Tanzania

    Postal Address: P.O.BOX 31902 ,2Morogoro Road

    Namba za simu: +255 22 2170173

    Namba ya simu :

    Barua pepe: md@kinondonimc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Privacy Policy
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa mara
    • Ramani ya tovuti
    • Service

Hatimiliki